Naona kuna propaganda mnaeneza mitandaoni kuwa mlisaidia CCM kupata ushindi 2015 na baada ya uchaguzi mkuu hayati JPM alipokamata madaraka aliwatenga na kuwaona hamfai wakati mlimuweka madarakani.
Acheni kupindisha maneno. Kila mtu anajua mlishazoea masuala ya kihuni ya kupora mali za umma kama mlivyofanya wakati ule kupitia Epa, Escrow, Kagoda na ufisadi mwingi bila aibu.
Mlitaka hayati Magufuli awakubalie uhuni wenu kisa tu mlifanya kampeni basi mfanye ufisadi mnavyotaka?
Sasa hivi kila mtanzania anawafamu vizuri na ndio maana mnapanga safu yenu ili mfanye uhuni wenu vizuri.