Tusipofanya hili wenyewe, wazungu watatupunguza kwa nguvu!

Kuna kitu unapaswa ukielewe ambacho ninahisi haukielewi, ni hivi swala zima za overpopulation siyo tu namba ya watu HAPANA, bali ni uwiano wa ukuaji uchumi na ongezeko la watu yaani uchumi wa nchi husika lazima uendane na ongezeko la idadi ya watu kwa mfano angalia nchi zote tajiri Dunia hii popote pale zilipo ziwe Ulaya, Marekani au Asia kuna kitu kimoja utaona zote zinafanana nazo ni kwamba ongezeko la watu halibadiliki sana yaani watu wanaokufa na wanaozaliwa wanalingana au karibia wanalingana hivyo hii inapelekea idadi ya watu kuwa constant au karibia na constant kwa mfano ukiangali labda Ufaransa utakuta ina watu milioni 60 kwa miaka 30 iliyopita au Ujapan ina watu milioni 120 kwa miaka 30 iliyopita vivyo kama kuna kuna ongezeko basi ni la asilimia ndogo sana ambalo linazidiwa na ukuwaji wa Uchumi au hata uchina ina watu 1.3 bilion kwa miaka 40 iliyopita ni constant!

Sasa sisi kwetu ni kinyume chake, ongezeko la watu siyo constant kwa maana wanaozaliwa ni wengi sana klk wanaokufa na hivyo basi ukuwaji wa uchumi wetu hauendani na ongezeko la watu matokeo yake hakuna kazi za kutosha, hakuna huduma za msingi za kutosha hospitali zinazidiwa kama wewe ni mkazi wa Dar utaliona hili wakati mimi nakuwa mambo ya kulala chini Temake Hospitali au M'mala yalikuwa hayapo leo ni kawaida, Shule hazitoshi, Miundo mbinu michache iliyopo inazidiwa kwa maana watu wameongezeka lkn Miundo ni ile ile, Maji ya kunywa hayatoshi kwa maana Bwawa lililojengwa kuhudumia wakazi milioni 1 leo wako milioni 4 lkn Bwawa ni lile lile, Mabomba ya kusafirishia maji ni yale hivyo yanazidiwa!

Sasa tofauti na nchi ulizozitaja hapo juu TanZania miaka 50 iliyopita tulikuwa milioni 18 leo hii milioni 48 hili ni ongezeko kubwa sana lkn kila kitu ni kile kile, kama ni shule zile zile, br. zile zile, mashamba yale yale, uzalishaji wa chakula ni ule ule na hapo ndipo tatizo lilipo sasa, tufanye nini?

Hakuna njia nyingine isipokuwa kufanya population control kwa uzazi wa mpango ili ongezeko letu la watu liendane na uwezo wetu wa kujihudumia!
Mkuu naomba ukafanye utafiti wa uliyoyaandika hapo juu then utapata jibu mwenyewe.
Nchi zilizoendeleo kama UK, USA na nchi nyingine za Ulaya na Asia zina kawaida ya kuwa na GDP growth rate ndogo kati ya 0.1 na 4 lakini population growth rate huwa juu ya hapo na sio sawa kama unavyodai wewe. Mfano population growth rate ya UK ni 5.4, Ufaransa ni 4.5 na Ujerumani ni 5 tukija upande wa GDP growth rate ya UK ni1.8 na Ufaransa ni 2. Sasa hapa ukiangalia bado population growth ni kubwa kuliko GDP growth rate na haiwezekani idadi ya watu wanaozaliwa na wanaokufa kuwa sawa. Nchi zote population inaongezeka na uchumi pia unakua
Kuhusu kuongezeka kwa miundombinu ni swala serikali kuangalia hilo barabara hazijengwi na watu binafsi hiyo ni kazi ya serikali na miundombinu ya afya kama hospitali ni uwekezaji wa serikali na secta binafsi sasa kama hatuwekezi ndio tusizae?
Hivi ni kweli kuwa miundombinu iliyoko sasa ndio hiyo hiyo iliyokua miaka ya 90?
Tuwe wawazi tu kuwa serikali zetu zilizopita hazikua makini katika kupanga na kutekeleza mipango wanayopanga, idadi ya watanzania iliyopo sasa sio bahati mbaya serikali ilishajua kwa kufanya projection hivyo ilikua ni swala la kuandaa miundombinu mapema.
 
Mkuu naomba ukafanye utafiti wa uliyoyaandika hapo juu then utapata jibu mwenyewe.
Nchi zilizoendeleo kama UK, USA na nchi nyingine za Ulaya na Asia zina kawaida ya kuwa na GDP growth rate ndogo kati ya 0.1 na 4 lakini population growth rate huwa juu ya hapo na sio sawa kama unavyodai wewe. Mfano population growth rate ya UK ni 5.4, Ufaransa ni 4.5 na Ujerumani ni 5 tukija upande wa GDP growth rate ya UK ni1.8 na Ufaransa ni 2. Sasa hapa ukiangalia bado population growth ni kubwa kuliko GDP growth rate na haiwezekani idadi ya watu wanaozaliwa na wanaokufa kuwa sawa. Nchi zote population inaongezeka na uchumi pia unakua
Kuhusu kuongezeka kwa miundombinu ni swala serikali kuangalia hilo barabara hazijengwi na watu binafsi hiyo ni kazi ya serikali na miundombinu ya afya kama hospitali ni uwekezaji wa serikali na secta binafsi sasa kama hatuwekezi ndio tusizae?
Hivi ni kweli kuwa miundombinu iliyoko sasa ndio hiyo hiyo iliyokua miaka ya 90?
Tuwe wawazi tu kuwa serikali zetu zilizopita hazikua makini katika kupanga na kutekeleza mipango wanayopanga, idadi ya watanzania iliyopo sasa sio bahati mbaya serikali ilishajua kwa kufanya projection hivyo ilikua ni swala la kuandaa miundombinu mapema.


Nitakuuliza swali moja ambalo ukilijibu ndiyo tuanze kujadili, niambie kwa miaka 20 iliyopita Uingereza ilikuwa na watu wangapi na leo hii ina watu wangapi? Au kuongeza wigo wa swali chukuwa nchi yoyote ile iliyoendelea kama Ujerumani (Ujerumani usisahau muungano wao), Ufaransa, Ujapani, Uswisi, Uswidi, Uholanzi , Kanada, New Zealand, Korea Kusini, Singapore, Taiwani au hata Afrika Kusini na nyinginezo halafu useme miaka 20 au hata 50 iliyopita ilikuwa na idadi ya wakazi wangapi kulinganisha na leo hii?
 
Mkuu labda unataka nikukusanyie data tu! mi nimeishia hapo maana sijaona logic ya kuendelea na hii mada nimekupa mifano ya kutosha kabisa kwa kila hoja, we endelea na mawazo yako hayo.
 
Hoja yako bado sio nzito kiasi hicho kwa sababu chanzo cha umaskini sio idadi kubwa ya watu, nchi zenye watu wengi kama Marekani, China na Urusi ni nchi kubwa Kiuchumi na zina watu matajiri sana na hii inatokana na ari kubwa ya watu kufanya kazi kwa bidii na hasa kujiingiza katika shughuli za uwekezaji na ujasiriamali. Watu ni rasilimali muhimu sana kwa uchumi wa taifa lolote lile.

Kwa nchi za Afrika kuwa na population kubwa ni liability na sio asset tofauti na nchi ulizotolea mfano za Marekani na China. Utafiti unaonyesha kadiri familia (household) inavyokuwa kubwa katika nchi za Afrika ndivyo zinapokuwa masikini zaidi. Kwa maneno mengine, kuna positive relationship kati ya family size na umasikini. Kwa maana hiyo theory yako inagoma kuwa justified kwa nchi zetu. Kwa kuwa empirical studies zimeonyesha hivyo, nadhani ni muhimu kuwa na checks za population growth ili kuto zalisha mizigo zaidi kwa ngazi ya familia na taifa kwa ujumla.

Aidha, ukifuatilia hizo nchi ulizozitaja angalia size ya households zao kama zipo kwenye average ya kwetu ya 5.6! China maximum ni watoto 2 kwa kila familia (though sheria hii wameifanyia mapitio siku za karibuni). Pia unaweza hata ku-google ukaona familia za kimarekani zina family members wangapi kwa kaya.

Indicator nzuri ya kama kuwa population ni asset ama ni liability angalia family size na sio overall population. Kama mtizamo wako ungekuwa sahihi basi China ndio ingeongoza mapinduzi ya viwanda, ikifuatiwa na India, nk. Kwa upande wa Africa Nigeria ilitakiwa iongoze kwa maendeleo, ikifuatiwa na nchi kama Misri, nk.
 
Mkuu labda unataka nikukusanyie data tu! mi nimeishia hapo maana sijaona logic ya kuendelea na hii mada nimekupa mifano ya kutosha kabisa kwa kila hoja, we endelea na mawazo yako hayo.


Nilikuuliza hivyo kwa makusudi kabisa ili kuona kama unaelewa hata kinachojadiliwa, ni hivi nchi zote zilizoendelea hakuna ongezeko kubwa la watu yaani wamebalance au wanakaribia kubalance watu wanaokufa na wanaozaliwa na ndio maana ukiangalia idadi ya watu ya Ujapani ni milioni 120 na iko hivyo tangia miaka 50 iliyopita au ukingalia Uswidi au Uswisi idadi yao iko karibia constant kwa tangia miaka 50, iliyopita kama kuna ongezeko basi ni la asilimia ndogo sana, lkn ukija kwetu TZ miaka 50 iliyopita tulikuwa milioni 18 leo hii tunakaribia milioni 50 hili ni ongezeko la zaidi ya mara mbili ndani ya miaka 50 tu yaani tumeongeza watu milioni 30 ina maana tusipochukuwa hatua mwaka 2050 tutakuwa watu milioni 80-100 sasa kazi zitatoka wapi kwa watu wote hawa? maji ya kunywa, umeme, br., Shule, nyumba za kuishi hivi vitu vyote tutavitoa wapi?

Wakati Ujapani mwaka 2050 watakuwa bado wanacheza hapo hapo milioni 120 kama nchi nyingine zilizoendelea, ukingalia nchi tajiri utakuta kwa miaka 50 iliyopita labda wameongeza watu milioni moja hivyo basi hata uchumi ukikuwa unawanufaisha wote lkn kwetu hata kama Uchumi ukikuwa kama leo hii ni kazi bure kwa maana watu wanaongezeka pia, na ndiyo maana unasikia watu wanasema tunasikia uchumi unakuwa lkn hatuoni mabadiliko, hiyo ndiyo moja ya sababu kubwa na ndicho nilichomaanisha!
 
Sisi tunazalisha wacheza pool, waendesha boda boda, wazee wa betting, mateja, nk. Wachache sana wanaokuwa na tija kwa jamii. Sina maana ya kuwatukana ila ninachojaribu kuonyesha ni kwamba tunazalisha watu wasio na tija kwa taifa. Wenzetu wanazalisha wagunduzi wa technolojia mbali mbali ambazo ni ingredients kwa maendeleo ya nchi zao na dunia kwa ujumla. Jiulize, kwanini ugunduzi wote unafanywa na mabara mengine na sio Afrika? Binafsi, naona bora tuzalishe mzigo mdogo wa familia na taifa kuliko kuzalisha mzigo mkubwa ambao ni net consumer badala ya kuwa net producer.

Over 60 per cent ya watanzania ni watoto. Wengi wao wanaenda kuwa mzigo kwa taifa kwa kuwa hawatapata elimu bora, hawatakuwa wazalishaji wazuri ktk nyanja tofauti tofauti, serikali zetu hazina ubunifu wa kutengeneza fursa kwa ajili ya ku-absorb sehemu kubwa ya hii increasing at an increasing rate of population growth, nk. Aidha, wasomi wengi hata katika nchi masikini kama Tanzania wanaujua ukweli huu ndio maana wanafamilia ndogo kuliko familia masikini. Wanazaa idadi ya watoto watakao weza kuwapa elimu bora na fursa mbali mbali za kiuchumi. Hivyo, kuwa na familia kubwa ingemaanisha utajiri basi tungekuwa tunaoa wake wengi ili tuwe matajiri zaidi lakini ukweli ni kinyume chake.
 
Utajiri wa maskini ni watoto.

Hahahaha uko sahihi mkuu. Hadi karne hii mtu anazaa matoto 7, 8, 9, nk huku hana kazi ya uhakika inayomuingizia kipato. Hali hii ni tofauti kwa wasomi na makundi mengine yenye vipato vya uhakika. Yaani mkulima anakuwa na familia kubwa kuliko professor wa chuo kikuu.
 
Nikushukuru Barbarosa kwa uzi mzuri ulionzisha na mpaka sasa mjadala unaenda vizuri; Ni ukweli usiopingika kuwa ni vigumu sana (kama ngamia kupenya katika tundu la sindano) kwa nchi kujiletea maendeleo huku ikiwa na idadi kubwa ya uwiano wa namba ya watoto kwa mwanamke (Tanzania kwa wastani kila mwanamke mmoja ana watoto 5.2, kiwango cha juu zaidi katika ukanda huu ni sudani kusini watoto 7: mwanamke).

Kwa hali ilivyo sasa lazima watanzania wahimizwe/wasaidiwe kupanga uzazi; hebu tazama takwimu hizi:

1. Idadi ya watu Tanzania inakuwa kwa asilimia 2.7; maana yake idadi ya watanzania kama mambo yakibaki ilivyo sasa itaongezekea mara mbili na kufikia watu millioni 100 ndani ya miaka 25 tu! Kumbuka mwaka 1967 sensa ya kwanza, watanzania walikuwa 12 milioni leo ndani ya miaka karibu 50 idadi imeongezeka mara nne! Ukilinganisha na nchi zilioendelea, mfano Finland itachukua miaka 130 ku-double idadi ya watu wao. Hili Barbarosa amelieleza sana lakini naona wengi hawajalielewa.

2. Idadi kubwa ya watoto wanaozaliwa, inalifanya taifa kuwa na watoto wengi na watu wengi wasiofanya kazi, dependants kuliko wanaofanya kazi, kitaalamu inaitwa age dependency ratio. Tanzania, nusu ya wanachi wana miaka chini ya 18 na Age depency ratio kwa Tanzania ni 94% USA 50% na UK 54%. Unapokuwa na age dependency ratio kubwa maana yake ni kuwa serikali ina mzigo mkubwa wa kuhudumia jamii kwenye public service (shule, afya, maji n.k).

3. Idadi ya vifo vya watoto wachanga inapungua huku idadi ya watoto wanaozaliwa ikibaki pale pale, hii inachangia ongezeko kubwa la watu.

Watu wengi wanaopinga hoja ya Barbarosa wametolea mifano nchi za China n.k lakini hoja zilizotolewa ni nyepesi na hazina mashiko: Nchi nyingi za Asia mashariki zilifanana na Tanzania miaka ya 60 (idadi kubwa ya watu, watoto na wategemezi wakiwa wengi kuliko wanaofanya kazi = high age depency ratio) lakini walichukua hatua kubwa zifuatazo:

1. Walipunguza idadi ya watoto wanaozaliwa (China One child policy nk) na kwa nchi nyingine njia walizochukua zilikiuka haki ya binadamu lakini ilikuwa ni lazima wafanye hivyo kwakuwa walikuwa na viongozi walioona mbali na wenye dhamira ya kweli kuondoa umaskini.

2. Waliimarisha elimu (kujenga uwezo wa vijana kuingia kwenye soko la ajira, elimu ya afya ya uzazi ili kuwa na taifa la watu wanye kupanga uzazi nk)

3. Mambo mengine ni kuimarisha viwanda, kuwekeza kwenye kilimo kukuza ajira nk.



Ili nchi iweze kuoiga hatua lazima tuwe na uwiano mzuri kati ya watoto, wale wanaozaliwa na ambao hawajafikia umri wa kuajiriwa na wale wanaofanya kazi. Kwa wale wanaosema Tanzania tuendelee kuzaliana kwa kuwa tuna mapori mengi watupe mfano wa nchi yenye maendeleo popote duniani ambayo ina age dependency ratio ya kuanzia 60 na kuendelea kwa kupitia hapa Age dependency ratio (% of working-age population) | Data | Table
 
Suala la idadi ya watu unatakiwa uangalie na ukubwa wa eneo na resources zilizopo apa nchini.. Kwa Tanzania bado tuna idadi ndogo ya watu. Population density ni 47. Nikimaanisha kwamba eneo la kilometers za mraba moja wanakaaa watu 47. Hii inaonyesha kwamba kuna mapori makubwa sana katika nchi yetu ambayo bado haya Jawa na watu kwa iyo population yetu inatakiwa ikue mpaka angalau million 120.
Mfano mdogo Nigeria wana eneo kama la Tanzania lakini lakini sisi tumewapita kidogo lakini idadi yao ni kama 190 million
 
Suala la idadi ya watu unatakiwa uangalie na ukubwa wa eneo na resources zilizopo apa nchini.. Kwa Tanzania bado tuna idadi ndogo ya watu. Population density ni 47. Nikimaanisha kwamba eneo la kilometers za mraba moja wanakaaa watu 47. Hii inaonyesha kwamba kuna mapori makubwa sana katika nchi yetu ambayo bado haya Jawa na watu kwa iyo population yetu inatakiwa ikue mpaka angalau million 120.
Mfano mdogo Nigeria wana eneo kama la Tanzania lakini lakini sisi tumewapita kidogo lakini idadi yao ni kama 190 million


Tujifunze kutoka kwa nchi wanazopunguzana kwa nguvu, kuna PM mmoja aliwahi kwenda ughaibuni kusema kwetu tuna ardhi tele, tusije tukafanya makosa kama kwenye madini tumevuna rasilimali hovyo bila kujipanga, ni bora twende polepole kwa manufaa ya vizazi vijavyo

Anyway lakini tunaweza kuamua "kufyatua watoto kwa wingi kwakuwa atawasomesha bure" kama tunaona kesho itajisumbukia yenyewe
 
Kuna point hasi na chanya kulingana na mada,ngoja nianze na hasi kwanza.
1-Kuzaliana kwa wingi bila mpangilio kunaongeza umaskini kwa kias kikubwa mnooo,kutokana kwamba,watoto watashindwa kusoma,,kupata huduma nzur za afya na kupelekea madhara makubwa baadae kwa taifa(kuwa na kizazi cha wajinga-yaan wasio na elimu)

2-kuzaliana kwa wingi kunasababisha matatizo kwa jamii pia nchi kwa ujumla(vitendo vya kihalifu vinaongezeka,rushwa kuendelea,n;k)

3-kuzaliana kwa wingi Pia kunarudisha maendeleo ya nchi nyuma.

Chanya
1-endapo watoto wote wakisomeshwa itakua faida kubwa kwa jamii/taifa kwa ujumla.
. KWA KUMALIZIA NAWEZA KUSEMA KWAMBA ENDAPO KILA KAYA/FAMILIA IKIHUSIKA MOJA KWA MOJA KATIKA MALEZI BORA YA MTOTO,HATA KAMA TUKIZALIANA WENGI KIASI GANI BASI ITAKUA FAIDA,LAKINI KUZALIANA KWA WINGI BILA MALEZI YOYOTE KWA MTOTO BASI TUTAENDELEA KUWA MASKINI HADI YESU ATAKAPORUDI,jiulize ni kwanini wale viongozi wazalendo wanatokea familia duni???hzo ambazo wanazaliana lukuki?
 
Back
Top Bottom