Chibike
JF-Expert Member
- Aug 16, 2024
- 4,897
- 7,526
Wala hakuna haja ya kutaka kusumbuka na hili lililojitokeza, waliosababisha haya wanajulikana sema sasahivi wamekaa kimya kama hawapo na zaidi wamewaruka watanzania kimanga kua hawakuambiwa warekebishe pitch. Matokeo watanzania maelfu kwa maelfu wamenyimwa fursa ya dhahabu ya kushuhudia tukio la kihistoria, kati yao wachache kwa idadi ya 15,000 ndio wataweza kusafiri. Tofauti ya mashabiki zaidi ya 45,000+, fursa ambayo pia wafanyabiashara mbalimbali kuanzia mama ntilie, migahawa, mahoteli, lodge, gesti, usafiri bodaboda bajaji teksi za mtandao kama Uber n.k wameikosa
Wala sio ishu ya makamu wa CAF kua kiongozi wa Berkane, wao wameona fursa wameitumia.
Sisi Wanasimba twendeni huko Zanzibar tukiwa na mashabiki wachache na tutakaowakuta huko Zanzibar kwa uchache wao wakiwa nje ya uwanja mana watakoingia ni 15,000 hapo ni pamoja na viongozi wa CAF delegates mbalimbali ..
Twendeni tukapambane, imeandikwa Simba atachukua ubingwa, basi itakua, imeandikwa tutabaki mshindi wa pili na kuambulia mabilioni na medali ya CAF, itakua..maisha mengine yaendelee. Kwa hapo tulipofikia tunamshukuru Mungu. Wakati mwingine lazima watu Fulani wajifunze kwa uchungu na maumivu makubwa sababu ni uzembe ufisadi na kutowajibika.
Wala sio ishu ya makamu wa CAF kua kiongozi wa Berkane, wao wameona fursa wameitumia.
Sisi Wanasimba twendeni huko Zanzibar tukiwa na mashabiki wachache na tutakaowakuta huko Zanzibar kwa uchache wao wakiwa nje ya uwanja mana watakoingia ni 15,000 hapo ni pamoja na viongozi wa CAF delegates mbalimbali ..
Twendeni tukapambane, imeandikwa Simba atachukua ubingwa, basi itakua, imeandikwa tutabaki mshindi wa pili na kuambulia mabilioni na medali ya CAF, itakua..maisha mengine yaendelee. Kwa hapo tulipofikia tunamshukuru Mungu. Wakati mwingine lazima watu Fulani wajifunze kwa uchungu na maumivu makubwa sababu ni uzembe ufisadi na kutowajibika.