Kamwe, kamwe, kamwe tusikate tamaa. Ukombozi huwa haupatikani kwa njia ya mkato tu. Wakati mwingine ni process ndefu yenye milima na mabonde. Lililotokea leo kwenye kesi ya Tundu Lissu lisitukatishe tamaa, inawezekana ni hatua mojawapo ya kuelekea kwenye ukombozi kamili.
Niwaombe sana wale ndugu zetu wanaoendesha hili gari kuelekea kwenye ukombozi wasiachie usukani njiani ilhali bado wanapumua.
CHADEMA bado wana nguvu kubwa sana tena sana ndo maana watawala wetu hawalali usingizi. Kama CHADEMA kisingekuwa tishio kubwa kwa watawala, hata Mwenyekiti angekuwa huru mpaka leo.
Wiki hili kuelekea kesi ya Tundu Lissu watawala hawajapata usingizi kabisa ndo maana wanatumia nguvu kubwa sana kudhibiti viongozi wa CHADEMA. Mimi naamini, haya yanayotokea ni mpango mzima wa kuelekea kwenye ukombozi kamili.
Huku mtaani watu wamechukia sana, lakini hatua kwa hatua, huko mbeleni watu hawa watakuja kuwa na ujasiri usiomithilika. Bado kidogo sana.
John Heche, John Mnyika, Boni Yai, Godbless Lema na wengineo, please, msikate tamaa, naamini siku hadi siku Watanzania tutazidi kujengeka na kuwa majasiri wa pekee sana katika Nchi hii.
Mungu awabariki na awatie nguvu na uwezo wa ajabu.
Niwaombe sana wale ndugu zetu wanaoendesha hili gari kuelekea kwenye ukombozi wasiachie usukani njiani ilhali bado wanapumua.
CHADEMA bado wana nguvu kubwa sana tena sana ndo maana watawala wetu hawalali usingizi. Kama CHADEMA kisingekuwa tishio kubwa kwa watawala, hata Mwenyekiti angekuwa huru mpaka leo.
Wiki hili kuelekea kesi ya Tundu Lissu watawala hawajapata usingizi kabisa ndo maana wanatumia nguvu kubwa sana kudhibiti viongozi wa CHADEMA. Mimi naamini, haya yanayotokea ni mpango mzima wa kuelekea kwenye ukombozi kamili.
Huku mtaani watu wamechukia sana, lakini hatua kwa hatua, huko mbeleni watu hawa watakuja kuwa na ujasiri usiomithilika. Bado kidogo sana.
John Heche, John Mnyika, Boni Yai, Godbless Lema na wengineo, please, msikate tamaa, naamini siku hadi siku Watanzania tutazidi kujengeka na kuwa majasiri wa pekee sana katika Nchi hii.
Mungu awabariki na awatie nguvu na uwezo wa ajabu.