Tusichanganye Dini na Siasa, ni hatari

Tusichanganye Dini na Siasa, ni hatari

Besta Mlagila

Senior Member
Joined
May 29, 2018
Posts
101
Reaction score
191
Hivi karibuni wafuasi wa CHADEMA wameanzisha utaratibu wa kwenda makanisani na sare za chama, Najiuliza Vipi CCM, ACT-Wazalendo, CUF au vyama vingine vikianza kwenda makanisani na sare za vyama vyao?

Makanisani watu wataanza kukaa kwa itikadi za vyama na itaibuka mijadala makanisani inayohusiana na vyama, viongozi makanisani wataanza kupingana kwa itikadi za vyama vyao na si dini.

Kama suala ni kumuombea MBOWE kwani maombi hayatasikika kama hawatavaa sare za vyama?

Mwisho makanisa yataanza kufanya siasa na tutajikuta tumeingia kwenye machafuko kama ya Rwanda ya mwaka 1994.
 
Akinya kuku sawa. Bata akinya kaharisha, unataka kusema CCM hawajawahi kuinigia kanisani na sare zao? Kwani sare zinazuiwa kanisani?
 
Sasa unaona chadema pana watu pale?
 
Kuna watu wazima wenye akili za kitoto sana ambao uwezo wao wa kufikiria unafifia na umri wao.

Inabidi uwe na akili za kipopoma sana kuishiwa mbinu na kuamua kutumia nyumba za ibada kama eneo la kupromote au kuzungumzia maswala na mijadala ya kisiasa.

I hope in the future days tutakuja na mwarobaini wa hili swala. Maana upuuzi ni mwingi sana unaendelea nyakati hizi.

Haiwezekani wazee na vijana wachache watuharibie miiko ya taifa letu.
 
Back
Top Bottom