Tusaidiane kuwasemea askari magereza

Jul 23, 2018
46
66
Mhe. Esther Matiko (MB) amekuwa kiungo mzuri sana katika kuwasemea Askari Polisi na hasa askari wa Magereza kabla na baada ya kwenda gerezani Segerea. Baada kwenda Gerezani kuna mambo mengi aliyabaini tofauti na yale aliyokuwa nayo awali.

MAY 24, 2019 aliuliza maswali kwa Waziri Mkuu juu ya hali ya Polisi hawa, na hasa suala la Polisi kupungukiwa sare za jeshi ambapo ni jukumu la serikali kuwahudumia sare kama vile; Suruali, Shati, Sketi, Mikanda ya suruali, filimbi, mikanda ya filimbi, nembo za cheo, soksi, kofia, sweta, viatu, ambavyo majeshi haya hasa Askari Polisi na hili la Magereza wamekuwa wakijinunulia hizi sare kwa vitambaa vinavyopatikana pale kwa Premji, ambapo kuna baadhi ya askari wameamua kuchukua tenda za kushona kwa 70,000 kwa pair kwa gharama zao.
Lakini pia, hata viatu wengi wa Polisi hawa wananunua kwa fedha zao {50,000/=}kwa kuwa Serikali haijawapelekea sare za kazi kwa muda mrefu sana.
Swali hili halikujibiwa kwa undani wake mbele ya Bunge badala yake yalitoka majibu ya kawaida sana.

Ndani ya Kitengo cha Askari Magereza kuna tatizo lingine kubwa la kimfumo ukiachana na hili la sare ambalo karibia kila askari analisema.

Licha ya kwamba Askari Magereza, Askari wa Uhamiaji, Polisi wa ulinzi wa raia, na Askari wengine wote wapo chini ya Wizara moja, ambayo ni Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi lakini kuna utofauti mkubwa sana wa malipo ya mishahara yao pamoja na utofauti wa Elimu zao.
Askari Magereza ndio Askari wanaolipwa mishahara ya chini sana kuliko Askari wengine ndani ya Idara hii ya Usalama.
Bila kujali utofauti wa viwango vyao vya Elimu. Jeshi la Magereza linateseka sana kwa mshahara huu mdogo na hasa ikizingatiwa kuwa katika kipindi hiki hali ya maisha imepanda sana.

Iko hivi; Polisi wa Usalama wa raia, mwenye Elimu ya Shahada (Degree Level of Education) analipwa mshahara wa Tsh. 860,000/= kama BASIC SALARY.
Pia anapata 15% ya mshahara wake kama Posho ya ujuzi ambayo ni sawa na Tsh. 129,000/=. Hivyo pesa ya (Grand Total) anayopokea Askari wa Usalama wa raia ni Tsh. 989,000/=.

Tangu mwaka 2015 Polisi wa Magereza wa Elimu ya Shahada (Degree Level of Education) wamekuwa wakilipwa Tsh. 400,000/= tu kama BASIC SALARY Sawa na askari Magereza mwenye elimu ya Kidatu Cha Nne.
Ukiondoa makato na pengine kama Askari huyu amekopa Benki, kwa mwezi Askari wa Magereza anaweza kujikuta amepokea Tsh. 180,000/=.
Kiwango hicho apange Nyumba, nauli na matumizi mengine.

Mishahara ya askari wa Magereza haiendani na Elimu zao tofauti na Askari wa kada zingine licha ya kuwa wote wapo chini ya Wizara moja.

Madai ni mengi ambayo serikali ameayaacha na kuwa mzigo ambayo kwa nyakati tofauti Mhe Matiko amekuwa akayasemea ili serikali ishughulikie kama Fedha za likizo, kupandishwa madaraja, wanatumia Fedha zao kusafirisha mahabusu/ wafungwa, Fedha za kuhamishwa n.k

Je, kwanini Serikali imepuuza kilio hiki cha Askari wa Magereza?
Ni wakati sasa wa kuwasaidia askari hawa, ili kuiomba Serikali iwasikilize na kufanyia kazi vilio vyao kwani wote hawalali usiku na mchana katika kutekeleza majukumu yao ya msingi.

Tumsaidie Mhe. Esther Matiko katika hoja zake juu ya Jeshi la Polisi kwa kulifanya jambo hili kuwa lenye sura ya Kitaifa. Asiachiwe mtu mmoja, kwakuwa ndugu zetu ndio wanaoteseka.

MOHONIA JOSEPH
 
Namba moja anataka mkitoka gerezani mlaani Askari magereza kwa ukatili wao, kinyume chake mnatoka na kuanza kuwatetea.

Hili swala linamkera Sana na kuona Kama Askari magereza hawafanyi kazi yao ipasavyo.

Siku mkitoka na kuanza kuwalalamikia kwa ukatili ndio atawaongezea misharara na kusikiliza kero zao.
 
Mhe. Esther Matiko (MB) amekuwa kiungo mzuri sana katika kuwasemea Askari Polisi na hasa askari wa Magereza kabla na baada ya kwenda gerezani Segerea. Baada kwenda Gerezani kuna mambo mengi aliyabaini tofauti na yale aliyokuwa nayo awali.

MAY 24, 2019 aliuliza maswali kwa Waziri Mkuu juu ya hali ya Polisi hawa, na hasa suala la Polisi kupungukiwa sare za jeshi ambapo ni jukumu la serikali kuwahudumia sare kama vile; Suruali, Shati, Sketi, Mikanda ya suruali, filimbi, mikanda ya filimbi, nembo za cheo, soksi, kofia, sweta, viatu, ambavyo majeshi haya hasa Askari Polisi na hili la Magereza wamekuwa wakijinunulia hizi sare kwa vitambaa vinavyopatikana pale kwa Premji, ambapo kuna baadhi ya askari wameamua kuchukua tenda za kushona kwa 70,000 kwa pair kwa gharama zao.
Lakini pia, hata viatu wengi wa Polisi hawa wananunua kwa fedha zao {50,000/=}kwa kuwa Serikali haijawapelekea sare za kazi kwa muda mrefu sana.
Swali hili halikujibiwa kwa undani wake mbele ya Bunge badala yake yalitoka majibu ya kawaida sana.

Ndani ya Kitengo cha Askari Magereza kuna tatizo lingine kubwa la kimfumo ukiachana na hili la sare ambalo karibia kila askari analisema.

Licha ya kwamba Askari Magereza, Askari wa Uhamiaji, Polisi wa ulinzi wa raia, na Askari wengine wote wapo chini ya Wizara moja, ambayo ni Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi lakini kuna utofauti mkubwa sana wa malipo ya mishahara yao pamoja na utofauti wa Elimu zao.
Askari Magereza ndio Askari wanaolipwa mishahara ya chini sana kuliko Askari wengine ndani ya Idara hii ya Usalama.
Bila kujali utofauti wa viwango vyao vya Elimu. Jeshi la Magereza linateseka sana kwa mshahara huu mdogo na hasa ikizingatiwa kuwa katika kipindi hiki hali ya maisha imepanda sana.

Iko hivi; Polisi wa Usalama wa raia, mwenye Elimu ya Shahada (Degree Level of Education) analipwa mshahara wa Tsh. 860,000/= kama BASIC SALARY.
Pia anapata 15% ya mshahara wake kama Posho ya ujuzi ambayo ni sawa na Tsh. 129,000/=. Hivyo pesa ya (Grand Total) anayopokea Askari wa Usalama wa raia ni Tsh. 989,000/=.

Tangu mwaka 2015 Polisi wa Magereza wa Elimu ya Shahada (Degree Level of Education) wamekuwa wakilipwa Tsh. 400,000/= tu kama BASIC SALARY Sawa na askari Magereza mwenye elimu ya Kidatu Cha Nne.
Ukiondoa makato na pengine kama Askari huyu amekopa Benki, kwa mwezi Askari wa Magereza anaweza kujikuta amepokea Tsh. 180,000/=.
Kiwango hicho apange Nyumba, nauli na matumizi mengine.

Mishahara ya askari wa Magereza haiendani na Elimu zao tofauti na Askari wa kada zingine licha ya kuwa wote wapo chini ya Wizara moja.

Madai ni mengi ambayo serikali ameayaacha na kuwa mzigo ambayo kwa nyakati tofauti Mhe Matiko amekuwa akayasemea ili serikali ishughulikie kama Fedha za likizo, kupandishwa madaraja, wanatumia Fedha zao kusafirisha mahabusu/ wafungwa, Fedha za kuhamishwa n.k

Je, kwanini Serikali imepuuza kilio hiki cha Askari wa Magereza?
Ni wakati sasa wa kuwasaidia askari hawa, ili kuiomba Serikali iwasikilize na kufanyia kazi vilio vyao kwani wote hawalali usiku na mchana katika kutekeleza majukumu yao ya msingi.

Tumsaidie Mhe. Esther Matiko katika hoja zake juu ya Jeshi la Polisi kwa kulifanya jambo hili kuwa lenye sura ya Kitaifa. Asiachiwe mtu mmoja, kwakuwa ndugu zetu ndio wanaoteseka.

MOHONIA JOSEPH
Achieni Wanyoli one day waingie kitaa kufanya undava
Ndio Presence yenu itakuwa recognised
 
Namba moja anataka mkitoka gerezani mlaani Askari magereza kwa ukatili wao, kinyume chake mnatoka na kuanza kuwatetea.

Hili swala linamkera Sana na kuona Kama Askari magereza hawafanyi kazi yao ipasavyo.

Siku mkitoka na kuanza kuwalalamikia kwa ukatili ndio atawaongezea misharara na kusikiliza kero zao.
Hili nilikuwa sijalifikiri! Kumbe ndio maana polisi anawapenda sana mpaka kuagiza hata akiua kazini hakuna kushtakiwa sababu watu wanalalamikia polisi?
Bado Siku ile katembelea Ukonga hasira mwanzo mwisho hadi kawanyang'anya tenda ya kujenga!
 
Hili lingemfikia Mheshimiwa rais

Lool. Graduate kulipwa laki nne sio kabisa, sasa Askari anaeanza kazi atalipwa ngapi?

Mheshimiwa Rais tunakuomba uwaangalie hawa watu wa wizara ya mambo ya ndani
 
Kama ndio hivyo bora niende jeshi la polisi nikalinde raia na mali zao, siku moja nifudhu niwe afisa wa polisi wa kimataifa(interpol) niwe ninalipwa 'interm of dorali'.




Ila kiufupi wizara ya mambo ya ndani ni majanga tu maana hata polisi nao wanalia njaa, hata bajeti yao ni ndogo sana.
Nasikia hata mafuta ya magari ya doria wanajaza kwa hela zao(askari), hela ambayo ilibidi wakamlipie mtoto ada, wananunua mafuta kwa gari ya serikali ya 'sisiemu'
 
boss wao anakata viuno stejini,anacheza kisingeli.

hii nchi kuna watu wanamharibia sana mzee baba,ila sijui wamemroga!!!!!haoniiiii
 
Inamaana sie zimanimoto aka fire brigade hatuna wa kutusemea? Acheni upendeleo huku mkijua tunawokoa ktk majanga yawakumbayo km vile moto,mafuriko,vimbunga,tetemeko..

Sare,mishahara,vifaa vya kazi na makazi tunapambana na hali zetu...

(Kwa niaba.)
 
Namba Moja anataka Jeshi la Magereza lijiendeshe lenyewe kwa kutumia vyanzo vyake vya mapato bila kutegemea serikali kuu. Rasilimali wanazo (mashamba, nguvukazi, miradi, nk.).

OVA
 
Iseeh.. Nimeshtuka Sana kwa habari hii yaani askari anajinunulia sare kwa fedha zake mwenyewe na mishahara yenyewe ndo hiyo.

Hii nchi ni masikini Sana.

Sasa kwanini viongozi weyu wanajisifu nchi inafedha wakati watumishi Hawa muhimu wanadhalilika hivi..

God have mercy..!
 
Namba moja anataka mkitoka gerezani mlaani Askari magereza kwa ukatili wao, kinyume chake mnatoka na kuanza kuwatetea.

Hili swala linamkera Sana na kuona Kama Askari magereza hawafanyi kazi yao ipasavyo.

Siku mkitoka na kuanza kuwalalamikia kwa ukatili ndio atawaongezea misharara na kusikiliza kero zao.
Duuh
 
Namba Moja anataka Jeshi la Magereza lijiendeshe lenyewe kwa kutumia vyanzo vyake vya mapato bila kutegemea serikali kuu. Rasilimali wanazo (mashamba, nguvukazi, miradi, nk.).

OVA
Hizo akili watazitoa wapi kwa malipo hayo wanayopata hata morari ya kazi hapo haipo..

Mbona wenzao jkt wanaudumiwa vizuri tu ndio maana wanakuwa wabunifu.

Isee... Hii ni kuumiza watu kisaikologia.

Very sad !
 
Mleta mada kama ulikua kati ya maaskari wenye mishahara midogo wanaoongoza ni zima moto yani wakikaa askari kwa askari wanapiga stori anaechekwa ni askari wa zima moto fatilia ujue uwe na taarifa...
 
Nimeinuliwa
EBOUrm5XkAA4A50.jpeg
 
Back
Top Bottom