Turekebishe sheria za dawa za kulevya

Nanren

JF-Expert Member
May 11, 2009
2,438
2,136
Wanajukwaa,

Kwa maoni yangu ni kwamba sheria zilizopo kuhusu dawa za kulevya zinapoteza muelekeo wa mapambano dhidi ya dawa hizo.
Kitendo cha kuiweka mirungi na bangi katika level moja na Cocaine na Heroin, kinapelekea nguvu kubwa kuelekezwa kwenye mashamba ya bangi na mirungi wakati tungeweza kukomaa kwanza na "unga" (Cocaine na Heroin). Ni vigumu sana kupambana na bangi ambayo kiasili inalimwa kwa wingi hapa hapa nchini. Tungeanza kwanza na Heroin na cocaine ambazo huletwa kutoka nje ya nchi na ndizo zenye madhara zaidi kwa vijana, then bangi na Mirungi itungiwe sheria zake na kushughulikiwa kitofauti kidogo. Hii hata hivyo haimaanishi kwamba bangi na mirungi ndio iachwe tu, hapana. Ila isipewe kipa umbele kama ilivyo kwa aina nyingine ambazo ni hatari zaidi.

Karibuni kwa maoni.
 
Yote ni madawa ya kulevya hivyo yapigwe vita kisawasawa au bado unafaidika mtoa maada wewe.
Pombe si inalevya nayo? Mbona haipigwi vita? By the way, how many lives have been lost due to alcohol related incidences? And how many due to ganja smoking or mirungi chewing?

Ukiangalia kwa upana zaidi, pombe zinapaswa kupigwa vita kama vile coka inavyopigwa! Madhara ya unywaji wa pombe ni makubwa mno.
[HASHTAG]#saynotoalcohol[/HASHTAG]
 
1."I don't smoke weed to escape reality , I smoke weed to enjoy realty even more " Bush doctor
2. Herb is a healing of the nation , alcohol is destruction " Bob Marley
 
Yote ni madawa ya kulevya hivyo yapigwe vita kisawasawa au bado unafaidika mtoa maada wewe.

Nisome vizuri.
Bangi ikivutwa ni madawa ya kulevya lakini pia inatumika duniani kwa matibabu mbali mbali. Sina ninachofaidika nayo, hata sigara sivuti.
Ninachosema ni kuwa Heroin na coka ni hatari zaidi, tungekazania zaidi hizo, afterall zinaletwa nchini kutoka nje.
Kutumia nguvu nyingi kupambana na mirungi na bangi sio sahihi. Nguvu nyingi ipelekwe kwenye heroin na coka.
Unafahamu kuwa mirungi sio dawa ya kulevya Kenya na Somalia lakini hapa kwetu ipo kwenye kundi moja na Heroin?
 
Back
Top Bottom