Pamoja na serikali kutokuwa na uhusiano kama wa zamani na US balozi Masilingi anajitahidi sana kwa wakati mgumu. Watanzania wa US walishakata tamaa na balozi lakini kama mdau naomba tumpe ushirikiano huyu balozi maana inaelekea anajitahidi pale iwezekanapo kujua matakwa ya Watanzania wa US na Mexico, ni mtu wa watu, haweki siasa mbele na anajitahidi sana kusaidia Watanzania kwa uwezo wake. Kama nilivyosema uzalendo ni kupenda nchi yako wakati wote na kupongeza serikali yako kwa mazuri na kukosoa kwa mabaya. Nampongeza huyu balozi kwa moyo wote.