Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,944
- 18,654
Tanzania hatujaanza kutumia chanjo leo kutoka kwa wazungu. Hivi sasa mpaka mtoto anakuwa, anachomwa chanjo mbalimbali sio chini ya mara 5. Taanzania haijawai hata kutengeneza chanjo yoyote toka ipate uhuru.
Leo tunaanzaje kukataa chanjo ya covid 19 kwa maamuzi au fikra ya mtu fulani ambaye unaweza kuta nyuma ya pazia kashajipiga iyo chanjo ya covid 19.
Nini maana ya kuwa na mamlaka ya kudhibiti viwango na maabara kuu ya taifa?
Ni wajibu wa serikali kupima na kudhibitisha viwango vya hizi chanjo kwanza kabla ya kuwapa wananchi wake na sio kuja na kauli ya kibaguzi, kishamba na kejeli wakati hata uwezo wa kutengeneza dawa hatuna.
Tunaelewa chanjo hazitolewi bure. Ni jukumu la serikali kununulia Wananchi wake chanjo.
Hata hivyo, kama serikali imegoma kununulia wananchi wake chanjo, Iweke huru kwa hospitali binafsi kuleta chanjo na wenye uwezo kujinunulia.
Hatuwezi kufa kwa uzembe wa kijinga namna hii. Chanjo ni muhimu kuliko mandege na mamiradi anayojenga. Kama chanjo wanataka kuua Waafrica wengine acha tutake risk. Bora kufa huku unapigania kusurvive kuliko kubweteka tu et Mungu wetu yupo hai. Kwani Mungu wa nchi nyingine ni marehemu?
Leo haamini chanjo za Mzungu ila yupo tayari kununua bombadia kutoka kwa mzungu kwa cash.
Leo tunaanzaje kukataa chanjo ya covid 19 kwa maamuzi au fikra ya mtu fulani ambaye unaweza kuta nyuma ya pazia kashajipiga iyo chanjo ya covid 19.
Nini maana ya kuwa na mamlaka ya kudhibiti viwango na maabara kuu ya taifa?
Ni wajibu wa serikali kupima na kudhibitisha viwango vya hizi chanjo kwanza kabla ya kuwapa wananchi wake na sio kuja na kauli ya kibaguzi, kishamba na kejeli wakati hata uwezo wa kutengeneza dawa hatuna.
Tunaelewa chanjo hazitolewi bure. Ni jukumu la serikali kununulia Wananchi wake chanjo.
Hata hivyo, kama serikali imegoma kununulia wananchi wake chanjo, Iweke huru kwa hospitali binafsi kuleta chanjo na wenye uwezo kujinunulia.
Hatuwezi kufa kwa uzembe wa kijinga namna hii. Chanjo ni muhimu kuliko mandege na mamiradi anayojenga. Kama chanjo wanataka kuua Waafrica wengine acha tutake risk. Bora kufa huku unapigania kusurvive kuliko kubweteka tu et Mungu wetu yupo hai. Kwani Mungu wa nchi nyingine ni marehemu?
Leo haamini chanjo za Mzungu ila yupo tayari kununua bombadia kutoka kwa mzungu kwa cash.