Tupike chapati za maji (yaani za kumimina)

Tupike chapati za maji (yaani za kumimina)

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2022
Posts
33,586
Reaction score
66,282
Kwanza utaanda unga wako wa ngano kisha kitunguu na karoti kama una penda hoho uta weka, kitunguu kisage usikate na hoho saga kwenye vile vidude vinauvyo uzwa buku buku, baada ya hapo uta vichanganya na unga kisha uta weka maji polepole.

Baada ya hapo uta weka sukari kidogo na chumvi kisha yai kisha changanya mvhanganyiko wako hakikisha usiwe mwepesi uwe mzito kiasi

Baada ya kuona mchanganyiko ume kuwa mzito utaanza kupika chota kidogo kidogo weka kwenye flampeni na uanze kuzungusha ili litokee duara kama hivi
1761416869094.jpeg

Baada ya hapo utaweka kwenye sahani au poti ina tegemeana na unavyo penda wewe mimi nimeweka kwenye sahani kama hivi
1761416982625.jpeg

Una weza kula na kinywaji chochote mimi nimetumia mtindi na mboga za majani huo ndio mlo wa usiku

Wapenzi wa Man U leo tunalala na viatu kwa furaha
Kama wewe ni yanga na shabiki wa man u leo kula vizuri ushindi uko mikonon mwetu
1761417129136.jpeg
 
Hongera mwachi zinaonekana vizuri.

Mi sipendi hii kitu.

Huwa nawapikia, ile ya mwisho ndio najipikia mwenyewe naikaushaaaa naila ikiwa bado ya moto, zaidi ya hivyo siwezi 😅
 
Hongera mwachi zinaonekana vizuri.

Mi sipendi hii kitu.

Huwa nawapikia, ile ya mwisho ndio najipikia mwenyewe naikaushaaaa naila ikiwa bado ya moto, zaidi ya hivyo siwezi 😅
Aajahaha una penda zile zakuungua zinakuwa kama kau kau sio
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom