Tupe uzoefu wako!!!!

Pole kwa uliyopitia na hongera kwa kupita salama. Nijuavyo mimi wanawake hatufanani hata kwenye mambo ya kawaida sasa inawezekana hata tuwapo wajawazito pia hatufanani kwani kila mmoja wetu ana experience ya peke yake . Kuna wengine hulia sana wakati wa kujifungua na wengine huwa kimya kabisa kama kwamba hana maumivu na wengine kipindi cha ujauzito huwa na nguvu ya kufanya kila kitu wengine hapana. Ninachoweza tu kusema tuko tofauti hata sijui kwanini labda malezi na koo tunazotoka .

Namshukuru mkwe wangu na mume wangu kwani daima walikua pamoja nami hata kwa mtoto wa mwisho. Ni kweli kuna wamama wanapitiliza lkn bado tuwahurumie ule mziki mnene. Sisi wamama wa sasa tujitahidi kuwafundisha uvumilivu watoto wetu wa kike na wa kiume .Kama ulivyoeleza maelezo haya akiambiwa kila mara mtoto wa kike naamini hawezi kujiachia kipindi chake kitakapofika. Na mtoto wa kiume pia tusimwache nyuma tumfundishe namna ya kubehave wakati mkewe awapo kwenye hali hii. Hapo tutapata mazao bora.
 

there you are talking now!!
ni kweli kuna kila sababu ya kuwafunza watoto wetu kuwajibika kila mtu kwa nafasi yake na pia kuwafundisha nidham kwenye maisha yetu ya kila siku. uvumilivu ni msingi wa kila jambo.

na katika mafunzo haya watoto wote wapatiwe si wa kike tu bali hata wa kiume.
 
kuna wanawake wana kera wewe haswa wakiwa na mimba usipime, tena huwaga kama vile wana nuia kwamba mimbaq hii nambebea baba fulan
Hahahahahaha nafikiri haya yote yanatokana na utaratibu wa maisha waliojiwekea. Kama huwa hakuna upendo hapo lazima mama atumie nafac ya ujauzito kumkomesha baba. Nampenda sana mume wangu na kipindi nahangaika na mambo haya nilijizuia mengi na alinisaidia sana kupita salama . Sikutaka kumuumiza hata kidogo ingawa nafsi yangu ilimchukia vibaya mno kwa ujauzito wa kwanza.
 
mambo ya saikolojia bwana ni kitu cha ajabu sana mi kuna mimba za wadada kibao huwa zinanipenda mpaka huwa najishangaa nna nini lakini sina namna
 
Unajua mimba inatofautiana kuna ambayo unakuja na kisirani hasa miez y mwanzo n nyingine unakuwa na hamu mume wako unatamani uwe nae kila saa sa mie ilikuwa ya kutaman kukaa na mme wangu lakini kwake ikawa tofauti akaon kama nambana au natumia mimba kutka awe nyumbani matokeo yake akawa jeuri no support tunaweza tukaaa week nzima hatuongei nikaona isiwe shida nikahamia kwetu nitunze mimba yangu Vizuri nilivyojifungua nilirudi kwangu so wanaume muwe mnajaribu kuwasoma wake zenu ni kweli wengine wanatumia mimba kuwacontrol Waume zao bt sio wote
 
mambo ya ujauzito .ni magumu sana, nakumbuka, ujauzito wa kwanza kwa wife ulikuwa mgumu sana, kwanda Ndio nilikuwa tunaanza maisha ya pamoja baada miezi 6 ya ndoa, nilikuwa nalazimishwa kula ubuyu hata sasa .za manane, chumba chote kilijaa mbegu .za ubuyu.

ukifika wakati wa clinic ikiwa sipo mtu haendi lazima niwepo.

Leo hii nipo tanga kikazi lakini tunasubiria mgeni mwingine, niko nae hapa, asubuhi nilivyomwambia nakwenda tanga nae akitoka moshi kwenda Dar,akazimisha kushuka segera, ikabidi nikubali kumsubiri....
ukweli .ni raha sana naona kulea mimba kisha mtoto ...
 
kudeka ukiwa mjamzito ni muhimu lakini 🙂..halafu,kukomesha deko la mke ndo utafte mwanamke mwingine? tena umlete jirani na unapoishi,mlishane bila kujali? inawezekanaje kweli?
 
yaani mwallu we acha tu, dunia hii ina watu wakatili hadi unashindwa kuelewa huwa wanawaza nini. ni leo tu nimetoka kusikia kwenye redio huko chalinze mwanamke ameuawa na kushindiliwa chupa katika sehemu za siri zote mbili, nyuma chupa ya bia na mbele chupa ya soda, yaani nikabaki nimeduwaa.
 
Last edited by a moderator:
how lovely
wish wote wangekua kama wewe au kama mume wa Ablessed
 
Last edited by a moderator:
naanza kuwaelewa sasa
 
naekuelewa saiv da gfsonwin...na hapo kwenye kuvumiliana nadhani ndo muhimu zaidi
 
Last edited by a moderator:
how lovelyaka
wish wote wangekua kama wewe au kama mume wa Ablessed
Hahahaha umenifanya nifurahi. Unajua huyu niliye nae nilifanya maombi ya dhati kwa Bwana naye akanijibu sawasawa na nilivyoomba nakumbuka Enzi hizo nilikua nafanya kazi kukawa na wengi walionifuata lkn moyoni nilisita sana. Namshukuru sana Mungu kwa hili na natoa ushauri kwa wadada wanaotaka mume mwema wamuombe Bwana kwa dhati kwani alishaga sema mke/mume ni wajibu wake kukupatia na daima atoacho Bwana huwa chema lkn mpaka umuombe.
 
ni kweli ukatili umejaa sana ila sisemi sana neno i dont want to get emotional here.nina binti na huwa nampenda sana for what i went through
 
kumbe humu wengi wamama eeh.shauri yenu mnaotafuta wachumba hapa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…