PSEUDOPODIA
JF-Expert Member
- Aug 9, 2020
- 376
- 735
Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kumuepusha ndugu Tundu Lisu na Kifo kilichokuwa kimepangwa na wabaya wake. Naamini kabisa Lisu hana ubavu wowote wa kupambana na risasi 16 zilizompata. Naamini Mungu alituma malaika zake wakaja kumfunika kiasi kwamba zile risasi hazikuwa na madhara makubwa.
Nirudi kwenye mada. Kwanini nasema Lisu ni Nyerere anaeishi. Kwanza tukumbuke kidogo hapo nyuma kulikuwepo na kizazi flani hivi ambacho kwa sasa ni nadra sana kukipata. Kizazi cha watu flani wapenda haki, wasiopenda kuonea au kuona wengine wakionewa, kizazi cha watu waliokuwa radhi kuupoteza uhai wao ili tu kupigania haki za wengine.
Watu hawa walikwepo kipindi cha nyuma, walikwepo wengi ila mimi nawajua wachache, ila kama na wewe unawajua wengine basi utaongezea. Kizazi cha kina J.K.Nyerere, Nelson Mandela, Kwame Nkuruma, Jomo Kenyatta , Abed Aman Karume na wengine wengi kwa sasa kimepotea kabisa na ni nadra sana kupata watu wenye hulka kama hizi.
Mimi toka nimezaliwa sijasikia habari kuhusu Mwalimu Nyerere kumdhulumu mtu, au alinyakua Mali ya mtu au ya serikali kwa dhuluma, au kumnyima mtu haki yake. Mwalimu alikuwa mpenda haki, asiyependa kunyanyaswa wala kunyanyasa wengine. Haki kwake ndo lilikuwa jambo la msingi sana, Uhuru wa watu ndicho alichopigania maisha yake yote.
Nikirudi kwa Tundu Lisu naona ana vinasaba vinavyoshabihiana kabisa na vya Mwalimu. Tangu nianze kumskia huyu bwana sijawahi sikia ana kashfa yoyote ya kumdhulumu mtu, rushwa au ufisadi, au kumdhulumu mtu haki yake. Zaidi naona yeye ndo mpambanaji anayetafuta haki za watu wengine.
Hata ulemavu alionao sasa ni kwa sababu ya kutafuta haki za watu, alikuwa akiwatetea watu mahakamani bure bila malipo. Tena anajigharamia na kutoa pesa zake ili zisaidie watu wapate haki zao. Yaani neno haki na Uhuru ndio misingi mikuu ya huyu bwana. Sawasawa na Mwalimu Huyu bwana amejengwa na kujijenga kwenye misingi ya haki, Uhuru na Utu. Yaani kwake watu wote ni sawa, haijalishi ni maskini ama tajiri.
Kingine alichonacho ambacho kinafanana kabisa na Mwalimu ni uwezo wake wa kujenga hoja zenye mantiki. Mwalimu alikuwa na uwezo wa kujenga hoja kiasi kwamba hata nchi za magharibi zilikuwa zina muheshimu. Tundu Lisu nae anauwezo huohuo wa Mwalimu.
Tundu Lisu pia anafanana na Mwalimu katika uwezo wake wa kupambanua mambo, upeo wa kuliona jambo hata kabla halijatokea, uwezo wa kuja na suluhisho la mambo mbalimbali kwa haraka na bila kufikiri sana.
Mwalimu pia alikuwa jasiri, si mwoga, anauwezo wa kuhoji mtu yeyeyote bila kujali cheo chake, sifa zote hizo anazo Tundu Lisu.Lisu anahoji chochote, popote na yoyote pale tu anapoona mambo hayaendi kama yalivyopangwa ama kama sheria zinavyosema.
Uwezo pia wa kushawishi watu ni sifa kuu ya Mwalimu ambayo Tundu Lisu utadhani ameikopi vile. Mwalimu akihutubia au akiongea na watu hutataka amalize, vivyohivyo kwa Bwana Lisu, hutatamani amalize. Uwezo pia wakujua na kuhifadhi mambo mengi kichwani, historia nyingi kichwani,yaani unaweza kudhani hawa mabwana wanasoma mahali kumbe vipo kichwani, kwa hili namwona Mwalimu kupitia Lisu.
Pia uwezo binafsi wa kupangilia mada hata kama utamwamsha usingizini, Nadra sana kumkuta mwalimu anasoma hotuba iliyokwisha andaliwa, au ana kikaratasi anasoma baadhi ya mambo. Vivyo hivyo kwa Tundu Lisu, yaani ukimwalika aje aongelee jambo flani, akija utadhani kama vile hayupo tayari au hajajiandaa maana hana kitu mkononi, kumbe vyote vipo kichwani.
Naomba nimalizie maana ni mengi sana hawa watu wawili wanafanana kabisa ila siwezi kuyaandika hapa yote. Labda kwa ufupi nihitimishe tu kuwa Hawa watu wawili IQ zao zinalingana, kama hazilingani basi zinakaribiana sana ndio maana wanafanana kwenye mambo mengi.
By Mimi Pseudopodia
Nirudi kwenye mada. Kwanini nasema Lisu ni Nyerere anaeishi. Kwanza tukumbuke kidogo hapo nyuma kulikuwepo na kizazi flani hivi ambacho kwa sasa ni nadra sana kukipata. Kizazi cha watu flani wapenda haki, wasiopenda kuonea au kuona wengine wakionewa, kizazi cha watu waliokuwa radhi kuupoteza uhai wao ili tu kupigania haki za wengine.
Watu hawa walikwepo kipindi cha nyuma, walikwepo wengi ila mimi nawajua wachache, ila kama na wewe unawajua wengine basi utaongezea. Kizazi cha kina J.K.Nyerere, Nelson Mandela, Kwame Nkuruma, Jomo Kenyatta , Abed Aman Karume na wengine wengi kwa sasa kimepotea kabisa na ni nadra sana kupata watu wenye hulka kama hizi.
Mimi toka nimezaliwa sijasikia habari kuhusu Mwalimu Nyerere kumdhulumu mtu, au alinyakua Mali ya mtu au ya serikali kwa dhuluma, au kumnyima mtu haki yake. Mwalimu alikuwa mpenda haki, asiyependa kunyanyaswa wala kunyanyasa wengine. Haki kwake ndo lilikuwa jambo la msingi sana, Uhuru wa watu ndicho alichopigania maisha yake yote.
Nikirudi kwa Tundu Lisu naona ana vinasaba vinavyoshabihiana kabisa na vya Mwalimu. Tangu nianze kumskia huyu bwana sijawahi sikia ana kashfa yoyote ya kumdhulumu mtu, rushwa au ufisadi, au kumdhulumu mtu haki yake. Zaidi naona yeye ndo mpambanaji anayetafuta haki za watu wengine.
Hata ulemavu alionao sasa ni kwa sababu ya kutafuta haki za watu, alikuwa akiwatetea watu mahakamani bure bila malipo. Tena anajigharamia na kutoa pesa zake ili zisaidie watu wapate haki zao. Yaani neno haki na Uhuru ndio misingi mikuu ya huyu bwana. Sawasawa na Mwalimu Huyu bwana amejengwa na kujijenga kwenye misingi ya haki, Uhuru na Utu. Yaani kwake watu wote ni sawa, haijalishi ni maskini ama tajiri.
Kingine alichonacho ambacho kinafanana kabisa na Mwalimu ni uwezo wake wa kujenga hoja zenye mantiki. Mwalimu alikuwa na uwezo wa kujenga hoja kiasi kwamba hata nchi za magharibi zilikuwa zina muheshimu. Tundu Lisu nae anauwezo huohuo wa Mwalimu.
Tundu Lisu pia anafanana na Mwalimu katika uwezo wake wa kupambanua mambo, upeo wa kuliona jambo hata kabla halijatokea, uwezo wa kuja na suluhisho la mambo mbalimbali kwa haraka na bila kufikiri sana.
Mwalimu pia alikuwa jasiri, si mwoga, anauwezo wa kuhoji mtu yeyeyote bila kujali cheo chake, sifa zote hizo anazo Tundu Lisu.Lisu anahoji chochote, popote na yoyote pale tu anapoona mambo hayaendi kama yalivyopangwa ama kama sheria zinavyosema.
Uwezo pia wa kushawishi watu ni sifa kuu ya Mwalimu ambayo Tundu Lisu utadhani ameikopi vile. Mwalimu akihutubia au akiongea na watu hutataka amalize, vivyohivyo kwa Bwana Lisu, hutatamani amalize. Uwezo pia wakujua na kuhifadhi mambo mengi kichwani, historia nyingi kichwani,yaani unaweza kudhani hawa mabwana wanasoma mahali kumbe vipo kichwani, kwa hili namwona Mwalimu kupitia Lisu.
Pia uwezo binafsi wa kupangilia mada hata kama utamwamsha usingizini, Nadra sana kumkuta mwalimu anasoma hotuba iliyokwisha andaliwa, au ana kikaratasi anasoma baadhi ya mambo. Vivyo hivyo kwa Tundu Lisu, yaani ukimwalika aje aongelee jambo flani, akija utadhani kama vile hayupo tayari au hajajiandaa maana hana kitu mkononi, kumbe vyote vipo kichwani.
Naomba nimalizie maana ni mengi sana hawa watu wawili wanafanana kabisa ila siwezi kuyaandika hapa yote. Labda kwa ufupi nihitimishe tu kuwa Hawa watu wawili IQ zao zinalingana, kama hazilingani basi zinakaribiana sana ndio maana wanafanana kwenye mambo mengi.
By Mimi Pseudopodia