Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 780
- 1,831
Jeshi la Polisi limepiga mabomu na kumkamata Tundu Lissu muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wake huko Mbamba Bay mkoani Ruvuma sasa hivi.
TAARIFA KUTOKA CHADEMA
BreakingNews Mwenyekiti wa Chama wa Taifa Mhe. Tundu A. Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi wilaya Mbinga. Mhe. Lissu amekamatwa wakati alipomaliza mkutano wa hadhara uliofanyika leo tarehe 09 Aprili 2025 Jimbo la Mbinga, mpaka sasa haijulikani amepelekwa kituo gani cha Polisi. Mwenyekiti amekamatwa pamoja na wanachama wengine, kwa sasa Jeshi hilo linaendelewa kutawanya wananchi kwa mabomu uwanjani hapo.
--
VIDEO: Muda mchache kabla ya Lissu kukamatwa
Muendelezo Wa Taarifa Iliyotolewa Na Godbless Lema Kuhusu Kukamatwa Kwa Tundu Lissu
Baada ya mkutano leo jioni saa 12:00 wilaya ya Mbinga, wakati wa kufunga mkutano OCD alimfuata Mwenyekiti Tundu Lissu Jukwani akamwambia tafadhali ukishuka hapo jukwani Ingia kwenye gari ya Polisi nakutaka Polisi kwa mahojiano.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Mh Lissu alimwambia nimefanya nini ? Huku akiendelea kuchangisha fedha ktk hadhara ‘ Tone Tone. baada ya kuona hiyo zogo , Kamanda Sosopi alimfuata OCD nakumwambia kama Lissu analo jambo na nyie pls mnaweza kuja pale tulipofikia mkamchukua kwa utaratibu hapa mtazua tafrani kubwa maana halaiki hapa ni kubwa,
Pia Mimi nilisisitiza Ushauri huo kwa OCD na wasaidizi wake wengine, alionekana kama anaelewa lakini ghafla mabomu ya machozi mengi yalianza kurindima.
Mh Lissu amekamatwa na sasa yuko kituo cha Polisi Mbinga.
TAARIFA KUTOKA CHADEMA
BreakingNews Mwenyekiti wa Chama wa Taifa Mhe. Tundu A. Lissu amekamatwa na Jeshi la Polisi wilaya Mbinga. Mhe. Lissu amekamatwa wakati alipomaliza mkutano wa hadhara uliofanyika leo tarehe 09 Aprili 2025 Jimbo la Mbinga, mpaka sasa haijulikani amepelekwa kituo gani cha Polisi. Mwenyekiti amekamatwa pamoja na wanachama wengine, kwa sasa Jeshi hilo linaendelewa kutawanya wananchi kwa mabomu uwanjani hapo.
--
VIDEO: Muda mchache kabla ya Lissu kukamatwa
Muendelezo Wa Taarifa Iliyotolewa Na Godbless Lema Kuhusu Kukamatwa Kwa Tundu Lissu
Baada ya mkutano leo jioni saa 12:00 wilaya ya Mbinga, wakati wa kufunga mkutano OCD alimfuata Mwenyekiti Tundu Lissu Jukwani akamwambia tafadhali ukishuka hapo jukwani Ingia kwenye gari ya Polisi nakutaka Polisi kwa mahojiano.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Baadhi wa wananchi waliofika kwenye mkutano huo wadaiwa kujeruhiwa wakati polisi wakitawanya wananchi
Mh Lissu alimwambia nimefanya nini ? Huku akiendelea kuchangisha fedha ktk hadhara ‘ Tone Tone. baada ya kuona hiyo zogo , Kamanda Sosopi alimfuata OCD nakumwambia kama Lissu analo jambo na nyie pls mnaweza kuja pale tulipofikia mkamchukua kwa utaratibu hapa mtazua tafrani kubwa maana halaiki hapa ni kubwa,
Pia Mimi nilisisitiza Ushauri huo kwa OCD na wasaidizi wake wengine, alionekana kama anaelewa lakini ghafla mabomu ya machozi mengi yalianza kurindima.
Mh Lissu amekamatwa na sasa yuko kituo cha Polisi Mbinga.