Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,346
- 26,138
Tangu kwenye kuanza kwa Bunge hili la kumi,Wakili Msomi Tundu A.M.Lissu (Mbunge wa Singida Mashariki-CHADEMA) amekuwa akizungumzia suala la Muungano mara kwa mara. Amekuwa akitoa wito,kwa nyaraka na shahidi mbalimbali, wa kurekebishwa makosa mbalimbali yaliyopo katika Muungano tulionao ili kusonga mbele kama Taifa. Lissu aliendelea kulichambua suala la Muungano kwenye Bunge Maalum la Katiba na hata leo katika Bunge la Bajeti linaloendelea Dodoma.
Kumekuwa na 'mradi' wa wapinzani wake wa kutaka watanzania wampuuze Lissu.Kwamba eti anayoyaongea ni ya kichochezi na hayana maana na msingi kwa Tanzania tuliyonayo. Mimi naamini kuwa Lissu hapuuziki katika hili. Anavyoonekana, amefanya utafiti wa kutosha katika suala hili. Anachokisema popote awapo anakijua,anakiamini na ana uhakika nacho. Hoja hii kwa Lissu sasa imekuwa nyepesi na anaimudu vyema.
Aitwe mchonganishi na mkorofi lakini ataendelea kusema. Kwakuwa anajua anachosema na kumaanisha. Ifike mahali,Serikali itumie hoja za Lissu katika kuuboresha Muungano huu uliopo kwa kurekebisha kasoro anazozitanabaisha Lissu. Kwa vijembe,kejeli,kelele,makofi na vigelegele hoja za Lissu zitabaki na zitaendelea.
Kumekuwa na 'mradi' wa wapinzani wake wa kutaka watanzania wampuuze Lissu.Kwamba eti anayoyaongea ni ya kichochezi na hayana maana na msingi kwa Tanzania tuliyonayo. Mimi naamini kuwa Lissu hapuuziki katika hili. Anavyoonekana, amefanya utafiti wa kutosha katika suala hili. Anachokisema popote awapo anakijua,anakiamini na ana uhakika nacho. Hoja hii kwa Lissu sasa imekuwa nyepesi na anaimudu vyema.
Aitwe mchonganishi na mkorofi lakini ataendelea kusema. Kwakuwa anajua anachosema na kumaanisha. Ifike mahali,Serikali itumie hoja za Lissu katika kuuboresha Muungano huu uliopo kwa kurekebisha kasoro anazozitanabaisha Lissu. Kwa vijembe,kejeli,kelele,makofi na vigelegele hoja za Lissu zitabaki na zitaendelea.