Mkuu usizunguke sana, tatizo la siasa za nchi yetu kwa sasa ni rais Magufuli, yeye ndiye asiyeweza siasa za ushindani hivyo anaamini akijenga miradi kadhaa na kuitangaza, basi watu wote watamkubali yeye au chama chake cha ccm.
Kwakuwa ana madaraka makubwa anayoyapata kupitia katiba outdated, basi anayatumia madaraka hayo kufurahisha nafsi yake, na kulazimisha atakacho yeye na genge lake na wanaofaidika na madaraka yake.
Hata wale wanaojua fika afanyacho sio sawa wako kimya kwa hofu. Ukitaka kujua Magufuli analazimsha kurudisha watu usingizini huku wakiwa wameshaamka, angalia idadi ya watu wanaoenda kujiandikisha kupiga kura ilivyo ndogo.
Nakuhakikishia atakapotoka madarakani rais Magufuli kila kitu kitabadilika na katiba mpya itapatikana. Kwa sasa watu washikilie msimamo wa tume huru ya uchaguzi, ambayo ni lazima ipatikane au uchunguzi uwe sio halali. Kutoka hapo kila kitu kitabadilika.