Bismack
JF-Expert Member
- Mar 12, 2018
- 387
- 487
Huyu mrembo kwa mara ya kwanza nilikutana naye jana Jumapili kwa lengo la kufahamiana mana tulikua hatjawahi kuonana, tumekua tukiwasiliana kwa njia ya simu tu.
Sasa mwanaume jana nikajikoki vizuri japo vyuma vimekaza nikampeleka sehemu nzuri yenye hadhi, tukaketi mhudumu akaja akatusikliza akatuleta vinywaji huku nyuma chakula kikiandaliwa tukaanza kupiga story za hapa na pale tukisubili chakula kiwe tayari.
Baada ya mda kidogo huyu mrembo akaniomba simu yangu nikampa alivoishika akaniambia kwanini una simu ya gharama hivi wakati mimi mchumba wako ninatumia tochi? Akaendelea kusema, ninahitaji simu nimechoka kutumia tochi.
Kiukweli yale maneno yalinikera ingawa Mungu alinipa hekima ya kuyajibu vizuri ili asione kama nimeyapokea vibaya, ingawa nilijiuliza maswali kadhaa kichwani kwangu nikajiuliza kwanini asingevumilia siku ya leo ikapita then siku nyingine ndo akaniambia shida zake?
Halafu ndo kwanza tumefika kwanini asingevumilia ukapita hata mda? Inamana kilicho mleta ni kupata simu tu? Sikupata majibu. Baada ya mda chakula kikaja tukala japo nilikula huku kichwa changu hakiko vizuri kabisa.
Kifupi nisiwachoshe wakuu ila nawaomba wadada mjaribu kua wavumilivu, mwanaume rijari lazima atajua unahitaji nini hata kabla hujasema ila siyo kulazimisha kama vile unamkomoa mtu.
Nawasilisha, asanteni.
Sasa mwanaume jana nikajikoki vizuri japo vyuma vimekaza nikampeleka sehemu nzuri yenye hadhi, tukaketi mhudumu akaja akatusikliza akatuleta vinywaji huku nyuma chakula kikiandaliwa tukaanza kupiga story za hapa na pale tukisubili chakula kiwe tayari.
Baada ya mda kidogo huyu mrembo akaniomba simu yangu nikampa alivoishika akaniambia kwanini una simu ya gharama hivi wakati mimi mchumba wako ninatumia tochi? Akaendelea kusema, ninahitaji simu nimechoka kutumia tochi.
Kiukweli yale maneno yalinikera ingawa Mungu alinipa hekima ya kuyajibu vizuri ili asione kama nimeyapokea vibaya, ingawa nilijiuliza maswali kadhaa kichwani kwangu nikajiuliza kwanini asingevumilia siku ya leo ikapita then siku nyingine ndo akaniambia shida zake?
Halafu ndo kwanza tumefika kwanini asingevumilia ukapita hata mda? Inamana kilicho mleta ni kupata simu tu? Sikupata majibu. Baada ya mda chakula kikaja tukala japo nilikula huku kichwa changu hakiko vizuri kabisa.
Kifupi nisiwachoshe wakuu ila nawaomba wadada mjaribu kua wavumilivu, mwanaume rijari lazima atajua unahitaji nini hata kabla hujasema ila siyo kulazimisha kama vile unamkomoa mtu.
Nawasilisha, asanteni.