Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,899
- 4,623
Wana jamvi kuna jambo linatatiza sana kichwa changu toka bajeti hii ya serikali isomwe. Kitakwimu deni la taifa linakisiwa kuwa trillion 20. Na uwezo wa pato letu la ndani ni wastani wa trillion 8 kwa mwaka huu. Hapa sasa ndipo shida yangu ilipo, ambapo naomba wasomi na wajasiriamali wote waliofanikiwa katika biashara zao bila hata ulazima wa elimu ya shule. Tutawezaje kulilipa deni letu kufikia zero huku matumizi ya kawaida yakizingatiwa achilia mbali miradi ya maendeleo? Hatujauzwa kweli? Hebu tueleweshane kwa kujaribu kuweka mbali itikadi za vyama vyetu zinazotupofusha katika masuala ya msingi yanayotuhusu. Nawakilisha.
.
.