Tunakoelekea Walimu wataacha kuhangaika na mtoto wa mtu

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,050
144,456
Kwa walio katika taaluma ya ualimu wanaweza kunielewa ila kama sio mwalimu basi hutanielewa. Mimi sio mwalimu ila nimepita huko.

Kizazi cha sasa, malezi ya watoto wa siku hizi na kubadilika kwa life style yetu ni mambo yanayofanya kazi ya ualimu kuwa ngumu sana na alierudisha viboko mashuleni aliona mbali ila tuendako walimu wanaweza kuacha kabisa kuadhibu wanafunzi japo viboko vimeruhusiwa.

Watoto wa siku hizi wanalelewa tofauti na sana na zamani na wakienda mashuleni wanakuwa hivyo hivyo na mwalimu usieweza ku-control hasira zako utaishia jela kama sio kufukuzwa.

Utatumia mbinu zote za ualimu ila bado unaweza tu usifanikiwe ku-handle watoto wa siku hizi kwa mafanikio na hii ni moja ya sababu ya kushuka kwa kiwango cha elimu.

Baada ya kupitia baadhi ya comments, nimegungua kuna watu hawajanielewa ila naomba niweke ufafanuzi ufuatao juu ya hili tukio kulingana na mtazamo wangu.


Kwanza nianze kwa kusema binafsi siungi mkono tukio hili ila najaribu kuwa objective kulingana na hulka ya sisi binadamu(mimi na wewe).

Ukiangali ile clip ni wazi wale walimu walipandwa na hasira kupita kiasi na bila shaka si hivi hivi tu bali kuna sababu ingawa hakuna sababu inayohalalisha walichokifanya ila kwa nature ya sisi binadamu bado tu tunaweza kujikuta unafanya kitendo kama hicho bila kutarajia kutokana na hasira tu.

Kwa mfano,mtu anaweza kumchoma mtu kisu katika ugomvi kutokana na hasira na mtuhumiwa kufikishwa mahakamani lakini mwisho wa siku kwa mshangao wa wengi mtuhumiwa anaweza kupatikana na hatia ya kuua bila kukusudia na wala si kuua kwa kukusudia kutokana na mazingira ya tukio lenyewe.

Unaweza usiwe na nia ya kuua lakini mtu akakutibua na kutokana na hasira ukachukua kitu kama nondo au jiwe na kumpiga nacho na bahati mtu huyo akapoteza maisha na mahakamani ukahukumiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia na sio kuua kwa kukusudia.

Kwa kesi hii ya walimu hawa,bado tunahitaji kusikia kutoka upande wa pili ni nini hasa kilitokea na kuwafanya kufikia hatua ile ya kushangaza.Si ajabu tukisikia nini kilitokea baadhi mnaweza kujikuta mnabaki katikati.

Ni kweli taaluma na maadili ya ualimu hayaruhusu kabisa walimu kufanya walichokifanya ila niwaulize jambo moja.

Hivi mtu unapomfumania mkeo au mumeo au ukahisi anaku-cheat,kuna sheria inayokuruhusu kumpiga mpaka kumjeruhi,kumpa kilema na wakati mwingine hata kumuua?

Hamjawahi sikia mtu anachinja mkewe kwasababh ya wivu tu?

Ukishakuwa na hasira na ukashindwa kuzi-control akili inakuwa sio yako tena na hutakumbuka kuna maadili ya ualimu wala sheria za nchi bali utafanya kile akili yako inachokutuma kufanya kwa wakati huo ila mwisho wa siku wengi huishia kujuta na wengine hata kujiua.

Hivi mnafikiri haya matukio yameanza leo?Haya matukio yapo tu siku zote ila hapa teknolojia ndio imetufumbua macho na bila teknolojia hii tukio pengine lingepita kama yanavyopita mengine.

Tuwe objective na tusisahau hasira ni hasara
 
Kwa walio katika taaluma ya ualimu wanaweza kunielewa ila kama sio mwalimu basi hutanielewa. Mimi sio mwalimu ila nimepita huko.

Kizazi cha sasa, malezi ya watoto wa siku hizi na kubadilika kwa life style yetu ni mambo yanayofanya kazi ya ualimu kuwa ngumu sana na alierudisha viboko mashuleni aliona mbali ila tuendako walimu wanaweza kuacha kabisa kuadhibu wanafunzi japo viboko vimeruhusiwa.

Watoto wa siku hizi wanalelewa tofauti na sana na zamani na wakienda mashuleni wanakuwa hivyo hivyo na mwalimu usieweza ku-control hasira zako utaishia jela kama sio kufukuzwa.

Utatumia mbinu zote za ualimu ila bado unaweza tu usifanikiwe ku-handle watoto wa siku hizi kwa mafanikio na hii ni moja ya sababu ya kushuka kwa kiwango cha elimu.
Una matatizo gani kichwani ndugu? Hakuna mzazi anayepinga mtoto kuadhibiwa lakini ukatili kama huu.

Kumbuka hata wahalifu huko ng'ambo hawateswi bali zimetafutwa njia za kisasa ili watoe taarifa zinazohitajika.

Ukatili kama ule ukimfanyia mtoto wangu basi ujuwe nakushoot tu hakuna mjadala.
 
Duuu aiseee mimi ni mwalimu lakini lazima uangalie aina ya adhabu kwa mwanafunzi kulingana na kosa na kwa kuzingatia kuwa wote ni binadam aisee

Chukulia huyo mwanafunzi alipewa adhabu akakataa, katika kujibishana wakashikana mashati na Mwalimu, tahamaki mwanafunzi kampika kichwa Mwalimu na kumtemea kohozi usoni. Ungekuwa wewe ungefanya nini?
 
Una matatizo gani kichwani ndugu? Hakuna mzazi anayepinga mtoto kuadhibiwa lakini ukatili kama huu.

Kumbuka hata wahalifu huko ng'ambo hawateswi bali zimetafutwa njia za kisasa ili watoe taarifa zinazohitajika.

Ukatili kama ule ukimfanyia mtoto wangu basi ujuwe nakushoot tu hakuna mjadala.
Ndio maana nimesema mwalimu usiweza control hisia zako utaishia jela.
 
Chukulia huyo mwanafunzi alipewa adhabu akakataa, katika kujibishana wakashikana mashati na Mwalimu, tahamaki mwanafunzi kampika kichwa Mwalimu na kumtemea kohozi usoni. Ungekuwa wewe ungefanya nini?
ndivyo ilivyokuwa au unadhania?? Bila shaka maelezo yaliyotolewa na mkuu wa mkoa hayakukuingia mkuu!!
 
Chukulia huyo mwanafunzi alipewa adhabu akakataa, katika kujibishana wakashikana mashati na Mwalimu, tahamaki mwanafunzi kampika kichwa Mwalimu na kumtemea kohozi usoni. Ungekuwa wewe ungefanya nini?
Mfano wako hauna maana yoyote. Hapa tunajadili lililotokea Mbeya na si masuala ya mwanafunzi kumtemea mate mwalimu. Ishi katika uhalisia walimu wa Mbeya wametenda jinai na sheria itawakata kama msumeno. Kingine unatakiwa ufahamu hakuna anayepinga adhabu zinazoangalia UTU kwa wanafunzi. Acha kupotosha
 
Chukulia huyo mwanafunzi alipewa adhabu akakataa, katika kujibishana wakashikana mashati na Mwalimu, tahamaki mwanafunzi kampika kichwa Mwalimu na kumtemea kohozi usoni. Ungekuwa wewe ungefanya nini?
Angefukuzwa shulen au akaitwa mzazi wake
 
Salary slip kaka sijawahi kukupinga hoja zako zote kwa hili la Mbeya nakupinga MTU unapiga kama unapiga nyoka! hapana kaka wangeweza hata kuua kabisa. Wawachape hata fimbo 4 siyo mbaya lakini siyo hiyo ya Mbeya.
Mkuu naongea hivi from experience.Kuna mwalimu mmoja wa kike alifanyiwa vituko darasani na wanafunzi ikabidi aje kuripoti staff kutafuta msaada na kilichofuta ni hasira za walimu.

Ndio maana nasema mwalimu asieweza ku-control hisia zake kwa nyakati hizi ataishia kubaya.
 
Chukulia huyo mwanafunzi alipewa adhabu akakataa, katika kujibishana wakashikana mashati na Mwalimu, tahamaki mwanafunzi kampika kichwa Mwalimu na kumtemea kohozi usoni. Ungekuwa wewe ungefanya nini?
Hakuna mwenye haki ya kutenda uhalifu kama huo...sema shida inakuwa akifanya hivi mwalimu inakuwa jambo kubwa kwa kuwa ana nguvu na mamlaka na anapaswa kutumia elimu yake na kutenda mambo kwa weledi. Ni sawa na pale mzazi/ mlezi anapomwadhibu mtoto, hata kama mtoto ametenda kosa kubwa akiumia jamii itamlaumu mzazi tofauti na labda mtoto ikitokea akamuumiza au kumsababishia hasara mzazi/ mlezi.....ndo mana watetezi wa haki za binadamu hutetea raia wasio na silaha dhidi ya nguvu ya jeshi(polisi nk)
 
Kwa walio katika taaluma ya ualimu wanaweza kunielewa ila kama sio mwalimu basi hutanielewa. Mimi sio mwalimu ila nimepita huko.

Kizazi cha sasa, malezi ya watoto wa siku hizi na kubadilika kwa life style yetu ni mambo yanayofanya kazi ya ualimu kuwa ngumu sana na alierudisha viboko mashuleni aliona mbali ila tuendako walimu wanaweza kuacha kabisa kuadhibu wanafunzi japo viboko vimeruhusiwa.

Watoto wa siku hizi wanalelewa tofauti na sana na zamani na wakienda mashuleni wanakuwa hivyo hivyo na mwalimu usieweza ku-control hasira zako utaishia jela kama sio kufukuzwa.

Utatumia mbinu zote za ualimu ila bado unaweza tu usifanikiwe ku-handle watoto wa siku hizi kwa mafanikio na hii ni moja ya sababu ya kushuka kwa kiwango cha elimu.
Bora waache kuliko kushambulia wanafunzi.
Mimi ni mwalimu wa sekondari, shule ya serikali. Nina miaka 17 kazini sijawahi kuona shambulio kama hili la mbeya.
Note1: Division one inapatikana panapokuwepo mawasiliano mazuri kati ya mwalimu na mwanafunzi
Note2: shule ina regulations zenye maudhui ya rule of law, haina jela ya kuwafunga watoto wakorofi ila zile procedures za kumwadhibu mwanafunzi zinamrekebisha.
Eg . Viboko 3 mbele ya school baraza na mzazi akiwepo ni adhabu kubwa kuliko viboko 100 ofisini.
Suspension humweka mtoto katika mazingira ya kutengana na wenzake hivyo mzazi kuumia na kuanza kumuonya mwanae, nk...
 
Back
Top Bottom