Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
Toka raisi JK azomewe mwaka jana (2011) pale UDSM kwenye maadhimisho
ya miaka 50 ya kuanzishwa UDSM,kumekua na udikteta unao endelea kila kukicha
nchi nzima kwa vyuo takribani vyote.
Kwa mfano,UDSM walifukuzwa wanachuo 43,bila sababu za msingi,...sababu ya kiubabaishaji
ikiwa ni kufanya fujo na mikusanyiko isiyokuwa halali.
UDOM week iliyo pita,baada ya kuwa wame cheleweshewa hela zao takribani mwezi mzima waliamua
kuandamana kwenda utawala kujua hatma ya hela zao,waliambiwa wangepata kesho yake.
Lakini siku hiyo hiyo waliyo goma kidogo walipata hela zao,na kesho yake wanafunzi zaidi ya 15
walifukuzwa kwa sababu ya "kuchochea mgomo na uvunjifu wa amani"
St.John chuo walikua na matatizo kama ya vyuo vyote kwa wanafunzi wanaopata mkopo,walipo goma
kudai haki yao,walifukuzwa wote na kurudishwa kwa masharti magumu sana.
Yanayo endelea Muhimbili kila mtu anayajua,magazeti yameelezea kwa undani zaidi.
Seikali ya wanafunzi pale UDSM huwa na kikao kimoja cha bunge (kikao halali) mara moja kwa semester.
Jumamosi iliyopita 7/1/2012 walikaa na kuamua ku-question wenzao kufukuzwa bila sababu za msingi
wakidai ni uonevu.
Kikao kile alihudhuria dean of students,kwa hiyo kilikua halali na maazimio yake ilikua ni kuwa na shinikizo la kutaka wanafunzi walio
fukuzwa warudishwe,....utawala ulipata habari hizi na kwa haraka sana,prof.Mgaya akatoa karipio kali na vitisho
kwamba atakaye shiriki mara moja atarudishwa kwao,...na hakuna ruksa ya kukusanyika maana utakuwa defined kwamba
una hamasisha mgomo.
Viongozi wa serikali ya wanafunzi walitoa maazimio ya kikao chao cha bunge tarehe 9/1/2012 asubuhi,...wakiwa wana
tafuta uungwaji mkono wa 2/3 ya wanachuo wote katika kushinikiza walio fukuzwa kwa kuonewa warudishwe.
Usiku huu,wame pigiwa simu wakitakiwa kwenda kuchokua barua zao warudi makwao haraka sana....kwa style ya UDSM
ya sasa,hii ni 3/4 ya kufukuzwa mazima maaana utasubiri kuitwa chuo hadi Yesu arudi.
Uko wapi uhuru wa kujieleza,?
Iko wapi haki ya kukusanyika?
Je,hii ndio adhabu anayotoa JK kwa wanafunzi baada ya kudhalilishwa?
Hali itakuaje/ikoje mtaani watu wanapodai haki zao?
Huu ni udikteta.
ya miaka 50 ya kuanzishwa UDSM,kumekua na udikteta unao endelea kila kukicha
nchi nzima kwa vyuo takribani vyote.
Kwa mfano,UDSM walifukuzwa wanachuo 43,bila sababu za msingi,...sababu ya kiubabaishaji
ikiwa ni kufanya fujo na mikusanyiko isiyokuwa halali.
UDOM week iliyo pita,baada ya kuwa wame cheleweshewa hela zao takribani mwezi mzima waliamua
kuandamana kwenda utawala kujua hatma ya hela zao,waliambiwa wangepata kesho yake.
Lakini siku hiyo hiyo waliyo goma kidogo walipata hela zao,na kesho yake wanafunzi zaidi ya 15
walifukuzwa kwa sababu ya "kuchochea mgomo na uvunjifu wa amani"
St.John chuo walikua na matatizo kama ya vyuo vyote kwa wanafunzi wanaopata mkopo,walipo goma
kudai haki yao,walifukuzwa wote na kurudishwa kwa masharti magumu sana.
Yanayo endelea Muhimbili kila mtu anayajua,magazeti yameelezea kwa undani zaidi.
Seikali ya wanafunzi pale UDSM huwa na kikao kimoja cha bunge (kikao halali) mara moja kwa semester.
Jumamosi iliyopita 7/1/2012 walikaa na kuamua ku-question wenzao kufukuzwa bila sababu za msingi
wakidai ni uonevu.
Kikao kile alihudhuria dean of students,kwa hiyo kilikua halali na maazimio yake ilikua ni kuwa na shinikizo la kutaka wanafunzi walio
fukuzwa warudishwe,....utawala ulipata habari hizi na kwa haraka sana,prof.Mgaya akatoa karipio kali na vitisho
kwamba atakaye shiriki mara moja atarudishwa kwao,...na hakuna ruksa ya kukusanyika maana utakuwa defined kwamba
una hamasisha mgomo.
Viongozi wa serikali ya wanafunzi walitoa maazimio ya kikao chao cha bunge tarehe 9/1/2012 asubuhi,...wakiwa wana
tafuta uungwaji mkono wa 2/3 ya wanachuo wote katika kushinikiza walio fukuzwa kwa kuonewa warudishwe.
Usiku huu,wame pigiwa simu wakitakiwa kwenda kuchokua barua zao warudi makwao haraka sana....kwa style ya UDSM
ya sasa,hii ni 3/4 ya kufukuzwa mazima maaana utasubiri kuitwa chuo hadi Yesu arudi.
Uko wapi uhuru wa kujieleza,?
Iko wapi haki ya kukusanyika?
Je,hii ndio adhabu anayotoa JK kwa wanafunzi baada ya kudhalilishwa?
Hali itakuaje/ikoje mtaani watu wanapodai haki zao?
Huu ni udikteta.