[h=3]
Uhuru wako...............[/h]
Hamu ya kumpenda mpenzi wako muda wote na wewe kupendwa kwa namna hiyo hiyo kwa muda wote ni kitu kinachofurukuta kwa kila moyo wa binadamu yeyote, vinginevyo kuna tatizo kubwa ambalo ni wewe tu unalijua au ni karama uliyopewa na Muumba.
Ingawa ni kweli tunastahili aina hiyo ya upendo (kupendwa na kupenda kunakofukuta ndani ya moyo muda wote na kufurahia na kujiona ni kweli kupendwa ni raha) si kweli kwamba hali kama hiyo inaweza kuja yenyewe au kutokea yenyewe bila kufanya chochote.
Kuwa na mapenzi ambayo yanaridhisha, yanachangamsha na kusisimua ndani ya moyo ni matokeo ya
extra ordinary achievement.
Ni hata kama ni rahisi kupata mapenzi ya aina hii haina maana kwamba watu hawana uwezo (
capacity) wa kupenda bali hawajui jinsi ya kuendelea kupendana tena na tena tangu kupendana kwa mara ya kwanza (
fall in love).
Inawezekana unaamini kwamba kutunza upendo ule wa kwanza na kuendelea nao miaka na miaka ni kitu kisichowezekana, si kweli kwani inawezekana.
Au inawezekana umeshaumizwa kutokana na mahusiano ya kwanza na moyo wako umevunjwavunjwa na una maumivu makali na hata kama upo kwenye mahusiano mazuri bado unajikuta upo bored na umekwamba pia inawezekana kwa sasa upo kwenye penzi lenyewe unajiona upo top of the world na kwa mbali unahisi upendo unaanza kuchuja na kupotea na unawasiwasi mambo yanaweza kuwa tofauti.
Kumbuka kuishi maisha marefu, katika penzi la kweli na muunganiko mzuri wa kimapenzi na mpenzi wako (mume au mke) siyo kitu ambacho ni complicated ni kitu rahisi na kipo ndani ya uwezo wako.
Unachotakiwa kugundua na kuendelea kuunganisha ni vitu vine tu
MWILI
Amsha senses, kuona, kusikia, kuonja na feelings za upendo. Fahamu mwili wako kuwa ni hekalu takatifu la upendo, zawadi ya muumba kwako, mwili wako hubeba nafsi yako, udhihirisho wa matendo ya Mungu kwako.
Mwili ni nyumba yako na uwe na amani hata katika ngozi yako. Jiweke tayari wakati wote kujisikia raha na mwili wako.
Upe mwili wako mapenzi, mguso wa kimwili.
Wewe ni mwili na mwili wako ni uhuru.
AKILI
Hakuna kikomo katika kufikiria, kila kikomo cha kufikiria kimewekwa na wewe. Unao uwezo wa kila unafikiria na unaweza kuamua kufikiria mambo mazuri kwa ajili ya maisha yako.
Hakuna anayeweza kuondoa furaha yako isipokuwa uamue mwenyewe.
Wewe ni akili na akili zako ni uhuru wako.
MOYO
Ponya moyo wako uliovunjika.
Fungua moyo wako ulioponywa.
Toa na pokea upendo kirahisi, kiasili (
naturally), ghafla, na
unconditionally.
Vumbua upendo ndani yako na jipende mwenyewe kwanza.
Jikubali mwenyewe kwanza na jisamehe kwa yale unakosea.
Fahamu kwamba unastahili kupokea upendo.
Tambua na karibisha upendo kutoka kwa wengine.
Tamani kuwa mtu wa kupenda kuliko mtu yeyote (
the greatest lover).
Wewe ni moyo na moyo wako ni uhuru.
NAFSI
Mwili wako, akili zako na moyo wako ni madirisha ya nafsi yako.
Unapowasiliana na Mungu ni nafsi yako inawasiliana na Mungu.
Nafsi yako ina mwili wako, akili zako, moyo wako ndani yake.
Wewe ni nafsi na nafsi yako ni uhuru