Thomas Sankra Jr
JF-Expert Member
- Mar 14, 2013
- 418
- 128
Nachukua nafasi hii kwanza kuwapongeza wanajukwaa wote kwa umoja na michango yenu. Jamii forumu pamekuwa mahali salama, kwetu sisi wanajukwaa kutoa mawazo yetu, Dumu daima Jamii forum.
Rais John Pombe Magufuri kwa hili sitakuunga mkono katu , nikweli safari yako umeianza vizuri lakini umesahau Mungu ndio anajua mwisho wetu sote..
Mh Rais Juzi kupitia kwa waziri wa utumishi umeteua MDAS na kamaliza kuunda serikali yake kwa kuwateua Wakurungezi wa majiji, Miji,Manispaa na Halmashauri. Katika uteuzi huo wapo Watumishi halali waliohitumikia nchi hii kwa uaminifu mkubwa, pia wapo wanasiasa wengine waliokuwepo kwenye utumishi huu wa umma lakini waliona vyema wakaingie kwenye siasa na wengine hawajawahi kuwa watumishi wa umma na wala hawajuwi misingi ya utumishi wa umma. Hali hii imenifanya nikinai sana zoezi hii, najuwa wapo waliofurahia uteuzi wako ... Hakika ni mawazo yao yao ukweli Mh Rais umearibu misingi ya utumishi wa umma..
Mh Rais ndani ya utumishi wa umma kuna walimu, watawala, madaktari, na watu wenye Taaluma za weledi mbalimbali, ndani ya utumishi wa umma kuna watumishi waadilifu na wenye maadili ya kutosha, ndani ya utumishi wa umma wapo watendaji wasomi, ndani ya utumishi wa umma kuna watendaji waaminifu, wachapaka, na waliotumikia utumishi wa umma katika mazingira tofauti kila pembe ya nchi hii kila tatizo la nchii hii kila mipaka ya nchi hii wanaijuwa. Utumishi wao umetukuka na kupongezwa leo hii unawaacha nakwenda kuwachukuwa watu ndani ya chama chako ambao hawajuwi misingi ya utumishi wa umma, hawajawahi kuwa watumishi wa umma na wengine walishindwa kuwa watumishi wa umma ndio unawapeleka kwenye nafasi za UDAS na UDED Mh Rais hapana hii sio utashi wa hekima na misingi tuliyopita
Kwa jambo hili sitakuunga mkono aiwezekani mtu hajawai kuona machungu ya utumishi wa umma leo anatoka polini alipotoka na kuwa DAS au DED kuna Watendaji wengi waandamizi walio tumikia utumishi wa umma kwa uhaminifu.
Mwisho.
Hakuna, hao watu wengi tayari waneteuliwa na ambao hawajateuliwa wamechanganyikiwa kwa kutoswa, hawana hamu na JFPoint ya msingi lakini subiri uvune majibu ya post yako sasa hivi watakuja
Mimi ni supporter mkubwa wa Magu ila huu uteuzi nimeanza kuwa na doudt naye, aisee kajaza watu wa ajabu kweli kuna watu kama tisa nawajua hawajui chochote zaidi ya kuwa makada, nashindwa kuelewa huu uteuzi kafanya akiwa ofisi za chama mbona Mkapa teuzi zake zilikuwa za maana sio huu ujinga anaofanya....nimeanza kurudia hotuba zake naona kuna shidaHapa ndipo anguko lilipo...hawa ma DAS,DED,DC ndio msingi wa Nyumba......
Ndani ya miezi tutarajie mabadiliko ya Mara kwa Mara,kufukuzana(ili kupata kick kwamba hakuna mchezo)
Hata mimi bila kuficha, mwanzoni nilivyomuona Magufuli akitenda na hasa ile hotuba yake ya wazee wa Dar, nilijua tumepata Rais Mzalendo ambaye hakika nchi yetu itasogea. Kadri siku zinavyozidi kusogea napata ufahamu mpya kuwa huyu ndugu hiyo taasisi ya Urais anapwaya sana. Hajui lipi lifanyike vipi na wapi, nani anastahili nini na muda upi kifanyike kipi.
subiri kura zitapotosha kwenu, saizi zamu yao wacha waendelee kula sehemu ya mali iliyowaangukia.Nachukua nafasi hii kwanza kuwapongeza wanajukwaa wote kwa umoja na michango yenu. Jamii forumu pamekuwa mahali salama, kwetu sisi wanajukwaa kutoa mawazo yetu, Dumu daima Jamii forum.
Rais John Pombe Magufuri kwa hili sitakuunga mkono katu , nikweli safari yako umeianza vizuri lakini umesahau Mungu ndio anajua mwisho wetu sote..
Mh Rais Juzi kupitia kwa waziri wa utumishi umeteua MDAS na kamaliza kuunda serikali yake kwa kuwateua Wakurungezi wa majiji, Miji,Manispaa na Halmashauri. Katika uteuzi huo wapo Watumishi halali waliohitumikia nchi hii kwa uaminifu mkubwa, pia wapo wanasiasa wengine waliokuwepo kwenye utumishi huu wa umma lakini waliona vyema wakaingie kwenye siasa na wengine hawajawahi kuwa watumishi wa umma na wala hawajuwi misingi ya utumishi wa umma. Hali hii imenifanya nikinai sana zoezi hii, najuwa wapo waliofurahia uteuzi wako ... Hakika ni mawazo yao yao ukweli Mh Rais umearibu misingi ya utumishi wa umma..
Mh Rais ndani ya utumishi wa umma kuna walimu, watawala, madaktari, na watu wenye Taaluma za weledi mbalimbali, ndani ya utumishi wa umma kuna watumishi waadilifu na wenye maadili ya kutosha, ndani ya utumishi wa umma wapo watendaji wasomi, ndani ya utumishi wa umma kuna watendaji waaminifu, wachapaka, na waliotumikia utumishi wa umma katika mazingira tofauti kila pembe ya nchi hii kila tatizo la nchii hii kila mipaka ya nchi hii wanaijuwa. Utumishi wao umetukuka na kupongezwa leo hii unawaacha nakwenda kuwachukuwa watu ndani ya chama chako ambao hawajuwi misingi ya utumishi wa umma, hawajawahi kuwa watumishi wa umma na wengine walishindwa kuwa watumishi wa umma ndio unawapeleka kwenye nafasi za UDAS na UDED Mh Rais hapana hii sio utashi wa hekima na misingi tuliyopita
Kwa jambo hili sitakuunga mkono aiwezekani mtu hajawai kuona machungu ya utumishi wa umma leo anatoka polini alipotoka na kuwa DAS au DED kuna Watendaji wengi waandamizi walio tumikia utumishi wa umma kwa uhaminifu.
Mwisho.