chamalee
Senior Member
- Jan 17, 2014
- 181
- 110
Nipo nasikiliza kipindi cha usiku wa Millenia kupitia Radio Free Africa mi ni mpenzi sana wa nyimbo za zamani Mtangazaji wa kipindi hiki ni Wambura Mtani nimeshtushwa na taarifa aliyoisema Hussein Jumbe hali yake sio nzuri wiki ya pili sasa yupo kitandani anaumwa, akisumbuliwa na sukari pamoja na kifua, hii ni baada ya kupata taarifa kutoka kwa mdau wa muziki wa zamani Jimmy Chika ambaye alienda kumtembelea nyumbani kwake Temeke kwa wale wasiomjua Hussein Jumbe ni mwanamuziki maarufu kwa miaka ya nyuma miaka ya 80, aliwahi kuimbia DDC Mliman Park na Msondo, Tabora Jazz.
Vibao vyake alivyowahi kuvitunga na kuviimba ni kama vile;
1.Nachechemea
2.Siri ya nini
3.Mume wangu Jerry
4.Isaya
5.Ajali n.k
Vibao vyake alivyowahi kuvitunga na kuviimba ni kama vile;
1.Nachechemea
2.Siri ya nini
3.Mume wangu Jerry
4.Isaya
5.Ajali n.k