Tumuamini Nani, Chadema Au Zitto Kabwe?

Tumuamini Nani, Chadema Au Zitto Kabwe?

Mchange

Senior Member
Joined
Jul 21, 2009
Posts
158
Reaction score
326
Kwa kipindi cha siku kadhaa sasa tumekuwa tukishuhudia maneno makali kutoka kwa wanachama na viongozi wa Chama cha CHADEMA kwenda kwa kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO ndugu Zitto Kabwe.

Njia mbalimbali zimetumika kufikisha mashambulizi hayo huku mitandao ya kijamii ikishika hatamu sambamba na makala za magazetini wakimuita Zitto kabwe ni Msaliti, wengine Kinyonga na wengine Mamluki huku Leo nikisoma makala nyingine ikimuita Zitto Kabwe ni Uyoga kwamba uyoga unaweza kutumiwa kama chakula na kadharika sumu.

Licha ya wanachama na viongozi hawa kujisahau pengine kuwa Zitto sio mwanachama wa chama chao na kwamba yeye ni mwanachama wa chama kingine kinachojitegemea chenye Sera, katiba na miongozo yake, lakini ni Dhahiri Viongozi na wanachama wa CHADEMA hawawezi kumsahau Zitto Kabwe.

Kama kuna jambo CHADEMA na viongozi wake nahisi linawauma na kuwanyima usingizi, basi kuendelea kuwepo kwa mwanasiasa huyu waliyemfukuza chama chao kwa matusi na kejeli nyingi mwaka 2015 mwanzoni.

Naam, ukisoma makala na maandiko yanayomshambulia Zitto kisa tu kakosoa kauli ya mwanasheria wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu kuhusu kutaka nchi inyimwe misaada na ushirikiano wa kimataifa, hauna utakachojifunza dhidi ya Chuki dhahiri za wanachadema kwa Zitto.

Kwa Lugha nyepesi tu unaweza ukasema CHADEMA na wafuasi wake wanatamani sana Madini yanayotemwa na Zitto Kabwe wa ACT WAZALENDO yangekuwa yanatemwa Hata kwa asilimia 20 na mmoja kati ya wabunge wao, ndio maana Hata Zitto afanye jema lipi, CHADEMA wao wataacha kulijadili alilolifanya watamvaa Zitto, huu ni udhaifu wa kiwango kikubwa sana.

CHADEMA wameumia sana Zitto kumsifia Rais Dkt Magufuli pale Jukwaani Kigoma, imewauma kwa sababu Hawakujua kuwa Zitto hakumsifia tu Rais Magufuli, Bali pia Zitto amempongeza kwa dhati kiongozi wa nchi anayepeleka mbele maendeleo ya wana kigoma.

Wamekasirika kwanini Zitto aliwahi kuukosoa utawala wa Rais Magufuli hapo nyuma halafu juzi eti amempongeza na kuona kwamba Zitto ni kigeugeu, walitamani Zitto aendelee kukosoa tu na kupinga hata maeneo dhahiri, ama wamesahau kwamba chama alichopo Zitto kwa sasa sio kazi yake kupinga kila kitu, na ndio maana wameamua kujitanabaisha na Slogan ya Taifa kwanza wakimaanisha kuwa wao maslahi ya nchi kwao ni kitu cha msingi kuliko chochote.

Wamesahau kwamba moja kati ya vichagizo vya Zitto na chama chake ni Kuupinga ujinga popote ulipo bila kujali chama cha anayefanya huo ujinga?. Ni vigumu sana kumuelewa Zitto kama haujui mpaka unaingia kwenye chama cha siasa unataka nini zaidi ya kupinga.

TUWAAMINI CHADEMA?...

Kwa msingi wa hoja zao kuwa Zitto ni kigeugeu na kwamba haaminiki Leo anaweza akapinga jambo na kesho akageuka, nadhani CHADEMA ndio wanaongoza kwa kuwa na sifa hiyo.

Kama hiyo ndio Hoja, basi Kwa sasa, CHADEMA ndio chama ambacho hakipaswi na hakiwezi kuaminiwa Mara 1000 zaidi kulinganisha na Zitto alivyo.

Nitatoa mifano Michache.

Mwaka 2013/2014, Freeman Mbowe akiwa kiongozi wa upinzani na mbunge wa Hai, aliwaongoza wabunge wenzake kupinga bajeti ya wizara ya Ujenzi iliyokuwa ikiongozwa na Dkt. Magufuli, mbowe aliipinga bajeti hiyo na kupiga kura ya hapana pale Bungeni, na kusema hawezi kuunga mkono serikali ya CCM.

Mungu si Athumani, mwaka huo huo Dkt Magufuli akaenda jimboni kwa Mbowe Hai, kisha au kabla alikwenda jimboni Rombo kwa Joseph Selasini, huwezi amini aisee,

Sifa alizozipolomosha Mbowe kwa Magufuli na Kikwete (aliyekuwa Rais) hazifikii hata Robo ya zile alizozitoa Zitto Kigoma, ndio maana ilimbidi mpaka Magufuli achukue link ya YouTube na kwenda nayo Bungeni katika bajeti iliyofata na kuwaambia wabunge na watanzani jinsi serikali ya CCM inavyochapa kazi kiasi cha kusifiwa hadharani na Freeman Mbowe. - NANI Tumuamini sasa, CHADEMA au Zitto?.

Naongeza, Kabla ya tarehe 15-09-2007, msamiati wa neno FISADI haukuwa maarufu hapa nchini Tanzania.

Unamjua aliyeuibua sawa sawa?.

Ni CHADEMA kupitia Tundu Lissu,

Ndio, Tundu Lissu akiwa Mwanachadema na mwanasheria machachali, tarehe 15-00-2007 pale viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es salaam, akishirikiana na Mbowe, na viongozi wengine wa upinzani akiwemo Dkt. Slaa, Maalim Seif , Mbatia na Wengine. Lissu alisoma Orodha ya Watanzania kumi na moja wanaolifilisi Taifa hili la Tanzania, tena akasema watu hawa hawanastaha ya kuitwa jina lingine zaidi ya MAFISADI, Lissu akasoma Orodha ya Mafisadi akisindikizwa na vifungu kibao vya Sheria.

Katika Timu ya watu 11 waliotajwa na Lissu kama mafisadi wanaoliumiza Taifa mtu NAMBA 9 aliyetajwa na Lissu na CHADEMA ni EDWARD LOWASSA Kwamba kwa mujibu wa Lissu na CHADEMA LOWASSA ni miongoni mwa Wafilisi 11 wa nchi hii, Leo LOWASSA yuko wapi, na Lissu yuko wapi na anasemaje?. - Tuwaamini CHADEMA ?.

Naongeza, Mwaka 2011/2012 kule Arumeru palikuwa na Uchaguzi wa Marudio, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema, alisimama Jukwaani na Kuwashukuru wananchi kuwa walimzomea Mzee LOWASSA. Nitayarejea baadhi ya maneno yake

"Jana mmemzomea LOWASSA, ni Heshima kubwa kwa Mungu Kumzomea Mwizi, LOWASSA ni FISADI" Huyo ni God bless lema wa CHADEMA , Leo LOWASSA yuko wapi na Lema yuko wapi?, anasema nini?..- TUWAAMINI CHADEMA?.

Niongeze?... Msigwa alimtukana LOWASSA, akasema atakayemnadi na kumshabikia LOWASSA akapimwe akili yake, nani alimnadi LOWASSA 2015, ni Zitto au Msigwa?. - Tuwaamini CHADEMA ?

Mwaka 2010 katika kampeni za Uchaguzi mkuu Moja kati ya Sera za CHADEMA ilikuwa ni kurudisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa na kugeuzwa maghala, CHADEMA wakasema watavirudidha kwa wananchi, Mbowe akasema lazima virudi, Leo mwaka 2017 Mbowe yule yule anasema serikali imekosea kutoa tamko la kuvirudisha viwanda vile vile walivuotaka kuvirudisha wao mwaka 2010. Tuwaamini CHADEMA?...

Mwaka 2010 mpaka 2013 mwanzoni, CUF waliitwa CCM B na CHADEMA, Nccr wakaitwa Washirika wa CCM, miezi michache mbele CCM B na washirika wa CCM wakaungana wakaitwa UKAWA. tuimini CHADEMA?

Mifano iko mingi mingi mingi sana.

USHAURI

Nawashauri viongozi na wanachama wa CHADEMA waachane na Zitto, wajenge CHADEMA yao, wamuache Zitto na ugeu geu wake na chama chake, watu makini wanafahamu kwamba CHADEMA ni kikundi cha watu wasaka madaraka tu na sio chama cha siasa.

Chama makini chochote cha siasa hakivunji wala kukiuka misingi yake iliyojiwekea,

Chama makini cha siasa hakiwezi badili Gia angani, lakini kikundi cha wasaka madaraka kinaweza Fanya lolote lile ilimradi tu kipate madaraka.

Wamuache Magufuli afanye kazi ya kuleta maendeleo aliyoahidi, maendeleo hayana chama, maendeleo hayana dini maendeleo hayana Kabila.

Kama Zitto alimpinga Magufuli Jana, sio kigezo cha kpongeza Leo kama amefanya vizuri na wala sio kizingizi cha kutokumkosoa kesho akifanya vibaya, hiyo ndio huitwa siasa ya masuala.

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lissu aliyemwita Fisadi namba Tisa hapa nchini,

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lema aliyekesha akimtukana katika mikutano ya kisiasa

Ndio maana LOWASSA hamsimangi msigwa, hamsimangi Mbowe aliyemkejeli kuwa ni dhaifu na baadae kumpokea wala hamsimangi yeyote, anafanya siasa zenye kukipigania anachokiamini atakipata ama anataraji kukipata.

Vijana, viongozi na wanachama wa CHADEMA kuhangaika na kina Zitto, Kitila mkumbo na Anna Mgwira ni kujidharirisha kwa kuonyesha kiwango kidogo cha uelewa wa masuala ya siasa.

Nawapongeza sana baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA wanaojikita kila uchao kuhangaika kutafuta suluhu ya changamoto za wananchi wao kama MEYA Boniface Jacob, John Mnyika, David Silinde Mwita Waitara nakadharika.

Muhimu kujua ni kwamba Zama zimebadilika, siasa zimebadilika, siasa za Leo si sawa na siasa za miaka mitano iliyopita.

Siasa za Leo zinahitaji wanasiasa wanaoleta majawabu kwa wananchi wao kuliko kutukanana kila uchao. Mmeshatukanana imetosha sasa wapeni majawabu wananchi.

Ndimi,
Habibu Mchange
0762178678
Mwananchi wa kawaida.
 
Mchange, nawe mbona ulikuwa ukimpigia kampeni Lowassa mwaka 2015 kule Kibaha ilihali ukiwa ni Mgombea wa ACT-Wazalendo na chama chako kilikuwa na mgombea Urais-Mama Mghwira?

Hivi kuna tapeli kijana wa kisiasa kama wewe Mchange? Umehamahama vyama kwa kusaka madaraka. Ulipoyakosa, hata Zitto aliyekuleta mjini na kukulea ukamuacha mkono.

Naona unaanza kutaka kujirudisha kwa Zitto. Dogo wewe ni tapeli wa kutupwa wa kisiasa.
 
Mchange bin Habib Mchange,kibaraka wa Zitto si ulihamia CCM kimya kimya na ukawa unashirikiana na kina Juliana Shonza na Mtela Mwamfamba?!

Uko CCM ila bado unaweka vitambulishi vya CHADEMA kama profile yako inavyoonekana,uaminiwe na nani?! Ama ndio umalaya wa siasa na tumbo limezidiwa na njaa?!!!
 
Endeeleni Tu utaratibu wenu, halafu umeandika gazeti mno.
 
Mchange Habibu karibu tena jukwaani , ni vema kabla hujamlinda Zitto , ieleze dunia kichokukimbiza ACT WAZALENDO , bila kuficha chochote , ukiendelea na vijineno vyako TUTAWEKA HADHARANI KILA KITU .
 
Mkuu Pambana na hali yako.. So ulisema umestaafu Siasa?

Hakuna kitu kilichowauma chadema Zitto kumsifia rais.... Alishazoeleka hivyo toka kamati ya Bomani.

Zitto ndio maisha yake, chadema walimuanika tu..

Gia ya uwaziri aendelee kuisikilizia kwenye radio...

Maendeleo anayosifia Kigoma sijui hata ni yep....

Siasa za unafiki na u snitch hazina chama
 
Wameacha kujadili hoja zangu wananijadili mimi
Hamna hoja yeyote uliyotoa mashudu tu umeandika mchumia tumbo mkubwa wewe hela ulizohongwa na ccm zimeisha na nyingine mmeona mnataka kuzulumiwa kama Wale madiwani wanavyotapeliwa ndo unaanza kujipendekeza kwa zitto, kufa njaaa
 
Wameacha kujadili hoja zangu wananijadili mimi
Unataka tukutenge na hoja zako? Unadhani ni rahisi kumtenga tapeli na utapeli wake? Kimsingi, mdogo wangu Mchange, huna credibility ya kutoa hoja za kuikosoa CHADEMA. Kama ni kuwa na fisadi Lowassa, nawe ulimpigia kampeni Lowassa hasa maeneo ya Mailimoja, Kwa Mathias, Picha ya Ndege na hata nyumbani kwetu Visiga. Ulikuwa ukisema Ubunge upewe wewe, Urais apewe Lowassa. Si usaliti huo kwa chama chako?

Mdogo wangu Mchange, kama unataka kurudi kwenye siasa, jifunze uvumilivu wa Mnyika ambaye amevumilia ndani ya CHADEMA changamoto zote hadi sasa anaaminiwa. Usijiunge na vijana wanaokuwa vyamani halafu wanataka kuota mapembe haraka na kusahau kuwa kila chama cha siasa kina wenyewe. Vyama ni kama kampuni, zina waanzilishi wake. Unapojiunga navyo, uende taratibu kwakuwa wanachama wa kawaida wa mipaka yao.

Mchange, mdogo wangu, nakuasa kuacha siasa za tumbo zilizojaa utapeli, ulaghai na propaganda. Usisahau kuwa tupo tunaokujua kwelikweli kuanzia ulipokuwa unafanya biashara ndogondogo pale stendi ya mabasi Mailimoja Kibaha hadi kuibuka kugombea mara mbili Ubunge wa Kibaha Mjini. Kama mwenyeji wa Kibaha, nafahamu kuwa ni utapeli tu wa kisiasa ndio uliokupa vyote ulivyonavyo. Ni mweupe sana kichwani. Tetere vipi? Nenda taratibu bwanamdogo.
 
Umeelewa sasa?....
Kwamba hoja wanayoitumia Makamanda haina tena mashiko
Kuwa kigeugeu sio tena issue kwani Chadema wameonyesha ugeugeu kwa vitendo

Unataka tukutenge na hoja zako? Unadhani ni rahisi kumtenga tapeli na utapeli wake? Kimsingi, mdogo wangu Mchange, huna credibility ya kutoa hoja za kuikosoa CHADEMA. Kama ni kuwa na fisadi Lowassa, nawe ulimpigia kampeni Lowassa hasa maeneo ya Mailimoja, Kwa Mathias, Picha ya Ndege na hata nyumbani kwetu Visiga. Ulikuwa ukisema Ubunge upewe wewe, Urais apewe Lowassa. Si usaliti huo kwa chama chako?

Mdogo wangu Mchange, kama unataka kurudi kwenye siasa, jifunze uvumilivu wa Mnyika ambaye amevumilia ndani ya CHADEMA changamoto zote hadi sasa anaaminiwa. Usijiunge na vijana wanaokuwa vyamani halafu wanataka kuota mapembe haraka na kusahau kuwa kila chama cha siasa kina wenyewe. Vyama ni kama kampuni, zina waanzilishi wake. Unapojiunga navyo, uende taratibu kwakuwa wanachama wa kawaida wa mipaka yao.

Mchange, mdogo wangu, nakuasa kuacha siasa za tumbo zilizojaa utapeli, ulaghai na propaganda. Usisahau kuwa tupo tunaokujua kwelikweli kuanzia ulipokuwa unafanya biashara ndogondogo pale stendi ya mabasi Mailimoja Kibaha hadi kuibuka kugombea mara mbili Ubunge wa Kibaha Mjini. Kama mwenyeji wa Kibaha, nafahamu kuwa ni utapeli tu wa kisiasa ndio uliokupa vyote ulivyonavyo. Ni mweupe sana kichwani. Tetere vipi? Nenda taratibu bwanamdogo.
 
Ukishafikia hatua ya hawa jamaa Habibu Mchange na Mpendazoe basi kilichobaki ni kuokota makopo tu. Uchizi hauji gafla bini vuu ni step by step. Hawa wapo step ya mwisho mwisho. Mara chadema Mara ACT mara siasa basi Mara CCM mara unasifia siafia tu na kuponda , who are you? Ungelikuwa unajua upinzani ni nini usingeliangaika hivyo, wewe tulia tuli , wenyekujua siasa wafanye siasa.
 
Wameacha kujadili hoja zangu wananijadili mimi
Hahahahahaha mchange unapima upepo??? We si ulishajiuzulu siasa na ukawakimbia wapinzani wenzako kipi umesahau hadi uanze tena kujihusisha na siasa au ndio unataka kucreate impact kabla hujarudi ccm???

Mmi ni kati ya vijana nliokuunga mkono sana enzi hizo unataka kugombea uenyekiti BAVICHA ila kubali brother ulipotea kabla hata hujafikia maturity ya kisiasa.... yule uliemtusi na kumdhihaki leo hii kawa mbunge Tarime huku wwe na matusi yote kwa chadema na lowasa leo umeishia kukata tamaa kwenye siasa hadi umejiuzuru baada ya kuanguka ubunge na kuona hamna future ACT kma ulivyotegemea awali

Kwa ushauri tu ni heri umfuate shonza na mwampamba CCM ili uonyeshe rangi yako halisi na urudi kwenye siasa ila kujificha upinzani huku hupapendi haitokusaidia lolote

Ni hayo tu ya kukushauri
 
Mchange, nawe mbona ulikuwa ukimpigia kampeni Lowassa mwaka 2015 kule Kibaha ilihali ukiwa ni Mgombea wa ACT-Wazalendo na chama chako kilikuwa na mgombea Urais-Mama Mghwira? Hivi kuna tapeli kijana wa kisiasa kama wewe Mchange? Umehamahama vyama kwa kusaka madaraka. Ulipoyakosa, hata Zitto aliyekuleta mjini na kukulea ukamuacha mkono. Naona unaanza kutaka kujirudisha kwa Zitto. Dogo wewe ni tapeli wa kutupwa wa kisiasa.
Kaka naona umeyatoa ya moyoni.
 
Kwa kipindi cha siku kadhaa sasa tumekuwa tukishuhudia maneno makali kutoka kwa wanachama na viongozi wa Chama cha CHADEMA kwenda kwa kiongozi wa chama cha ACT WAZALENDO ndugu Zitto Kabwe.

Njia mbalimbali zimetumika kufikisha mashambulizi hayo huku mitandao ya kijamii ikishika hatamu sambamba na makala za magazetini wakimuita Zitto kabwe ni Msaliti, wengine Kinyonga na wengine Mamluki huku Leo nikisoma makala nyingine ikimuita Zitto Kabwe ni Uyoga kwamba uyoga unaweza kutumiwa kama chakula na kadharika sumu.

Licha ya wanachama na viongozi hawa kujisahau pengine kuwa Zitto sio mwanachama wa chama chao na kwamba yeye ni mwanachama wa chama kingine kinachojitegemea chenye Sera, katiba na miongozo yake, lakini ni Dhahiri Viongozi na wanachama wa CHADEMA hawawezi kumsahau Zitto Kabwe.

Kama kuna jambo CHADEMA na viongozi wake nahisi linawauma na kuwanyima usingizi, basi kuendelea kuwepo kwa mwanasiasa huyu waliyemfukuza chama chao kwa matusi na kejeli nyingi mwaka 2015 mwanzoni.

Naam, ukisoma makala na maandiko yanayomshambulia Zitto kisa tu kakosoa kauli ya mwanasheria wa chama cha CHADEMA Tundu Lissu kuhusu kutaka nchi inyimwe misaada na ushirikiano wa kimataifa, hauna utakachojifunza dhidi ya Chuki dhahiri za wanachadema kwa Zitto.

Kwa Lugha nyepesi tu unaweza ukasema CHADEMA na wafuasi wake wanatamani sana Madini yanayotemwa na Zitto Kabwe wa ACT WAZALENDO yangekuwa yanatemwa Hata kwa asilimia 20 na mmoja kati ya wabunge wao, ndio maana Hata Zitto afanye jema lipi, CHADEMA wao wataacha kulijadili alilolifanya watamvaa Zitto, huu ni udhaifu wa kiwango kikubwa sana.

CHADEMA wameumia sana Zitto kumsifia Rais Dkt Magufuli pale Jukwaani Kigoma, imewauma kwa sababu Hawakujua kuwa Zitto hakumsifia tu Rais Magufuli, Bali pia Zitto amempongeza kwa dhati kiongozi wa nchi anayepeleka mbele maendeleo ya wana kigoma.

Wamekasirika kwanini Zitto aliwahi kuukosoa utawala wa Rais Magufuli hapo nyuma halafu juzi eti amempongeza na kuona kwamba Zitto ni kigeugeu, walitamani Zitto aendelee kukosoa tu na kupinga hata maeneo dhahiri, ama wamesahau kwamba chama alichopo Zitto kwa sasa sio kazi yake kupinga kila kitu, na ndio maana wameamua kujitanabaisha na Slogan ya Taifa kwanza wakimaanisha kuwa wao maslahi ya nchi kwao ni kitu cha msingi kuliko chochote.

Wamesahau kwamba moja kati ya vichagizo vya Zitto na chama chake ni Kuupinga ujinga popote ulipo bila kujali chama cha anayefanya huo ujinga?. Ni vigumu sana kumuelewa Zitto kama haujui mpaka unaingia kwenye chama cha siasa unataka nini zaidi ya kupinga.

TUWAAMINI CHADEMA?...

Kwa msingi wa hoja zao kuwa Zitto ni kigeugeu na kwamba haaminiki Leo anaweza akapinga jambo na kesho akageuka, nadhani CHADEMA ndio wanaongoza kwa kuwa na sifa hiyo.

Kama hiyo ndio Hoja, basi Kwa sasa, CHADEMA ndio chama ambacho hakipaswi na hakiwezi kuaminiwa Mara 1000 zaidi kulinganisha na Zitto alivyo.

Nitatoa mifano Michache.

Mwaka 2013/2014, Freeman Mbowe akiwa kiongozi wa upinzani na mbunge wa Hai, aliwaongoza wabunge wenzake kupinga bajeti ya wizara ya Ujenzi iliyokuwa ikiongozwa na Dkt. Magufuli, mbowe aliipinga bajeti hiyo na kupiga kura ya hapana pale Bungeni, na kusema hawezi kuunga mkono serikali ya CCM.

Mungu si Athumani, mwaka huo huo Dkt Magufuli akaenda jimboni kwa Mbowe Hai, kisha au kabla alikwenda jimboni Rombo kwa Joseph Selasini, huwezi amini aisee,

Sifa alizozipolomosha Mbowe kwa Magufuli na Kikwete (aliyekuwa Rais) hazifikii hata Robo ya zile alizozitoa Zitto Kigoma, ndio maana ilimbidi mpaka Magufuli achukue link ya YouTube na kwenda nayo Bungeni katika bajeti iliyofata na kuwaambia wabunge na watanzani jinsi serikali ya CCM inavyochapa kazi kiasi cha kusifiwa hadharani na Freeman Mbowe. - NANI Tumuamini sasa, CHADEMA au Zitto?.

Naongeza, Kabla ya tarehe 15-09-2007, msamiati wa neno FISADI haukuwa maarufu hapa nchini Tanzania.

Unamjua aliyeuibua sawa sawa?.

Ni CHADEMA kupitia Tundu Lissu,

Ndio, Tundu Lissu akiwa Mwanachadema na mwanasheria machachali, tarehe 15-00-2007 pale viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar es salaam, akishirikiana na Mbowe, na viongozi wengine wa upinzani akiwemo Dkt. Slaa, Maalim Seif , Mbatia na Wengine. Lissu alisoma Orodha ya Watanzania kumi na moja wanaolifilisi Taifa hili la Tanzania, tena akasema watu hawa hawanastaha ya kuitwa jina lingine zaidi ya MAFISADI, Lissu akasoma Orodha ya Mafisadi akisindikizwa na vifungu kibao vya Sheria.

Katika Timu ya watu 11 waliotajwa na Lissu kama mafisadi wanaoliumiza Taifa mtu NAMBA 9 aliyetajwa na Lissu na CHADEMA ni *EDWARD LOWASSA* Kwamba kwa mujibu wa Lissu na CHADEMA LOWASSA ni miongoni mwa Wafilisi 11 wa nchi hii, Leo LOWASSA yuko wapi, na Lissu yuko wapi na anasemaje?. - Tuwaamini CHADEMA ?.

Naongeza, Mwaka 2011/2012 kule Arumeru palikuwa na Uchaguzi wa Marudio, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA ambaye pia ni Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema, alisimama Jukwaani na Kuwashukuru wananchi kuwa walimzomea Mzee LOWASSA. Nitayarejea baadhi ya maneno yake

*"Jana mmemzomea LOWASSA, ni Heshima kubwa kwa Mungu Kumzomea Mwizi, LOWASSA ni FISADI*" Huyo ni God bless lema wa CHADEMA , Leo LOWASSA yuko wapi na Lema yuko wapi?, anasema nini?..- TUWAAMINI CHADEMA?.

Niongeze?... Msigwa alimtukana LOWASSA, akasema atakayemnadi na kumshabikia LOWASSA akapimwe akili yake, nani alimnadi LOWASSA 2015, ni Zitto au Msigwa?. - Tuwaamini CHADEMA ?

Mwaka 2010 katika kampeni za Uchaguzi mkuu Moja kati ya Sera za CHADEMA ilikuwa ni kurudisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa na kugeuzwa maghala, CHADEMA wakasema watavirudidha kwa wananchi, Mbowe akasema lazima virudi, Leo mwaka 2017 Mbowe yule yule anasema serikali imekosea kutoa tamko la kuvirudisha viwanda vile vile walivuotaka kuvirudisha wao mwaka 2010. Tuwaamini CHADEMA?...

Mwaka 2010 mpaka 2013 mwanzoni, CUF waliitwa CCM B na CHADEMA, Nccr wakaitwa Washirika wa CCM, miezi michache mbele CCM B na washirika wa CCM wakaungana wakaitwa UKAWA. tuimini CHADEMA?

Mifano iko mingi mingi mingi sana.

USHAURI

nawashauri viongozi na wanachama wa CHADEMA waachane na Zitto, wajenge CHADEMA yao, wamuache Zitto na ugeu geu wake na chama chake, watu makini wanafahamu kwamba CHADEMA ni kikundi cha watu wasaka madaraka tu na sio chama cha siasa.

Chama makini chochote cha siasa hakivunji wala kukiuka misingi yake iliyojiwekea,

Chama makini cha siasa hakiwezi badili Gia angani, lakini kikundi cha wasaka madaraka kinaweza Fanya lolote lile ilimradi tu kipate madaraka.

Wamuache Magufuli afanye kazi ya kuleta maendeleo aliyoahidi, maendeleo hayana chama, maendeleo hayana dini maendeleo hayana Kabila.

Kama Zitto alimpinga Magufuli Jana, sio kigezo cha kpongeza Leo kama amefanya vizuri na wala sio kizingizi cha kutokumkosoa kesho akifanya vibaya, hiyo ndio huitwa siasa ya masuala.

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lissu aliyemwita Fisadi namba Tisa hapa nchini,

Ndio maana LOWASSA hamsimangi Lema aliyekesha akimtukana katika mikutano ya kisiasa

Ndio maana LOWASSA hamsimangi msigwa, hamsimangi Mbowe aliyemkejeli kuwa ni dhaifu na baadae kumpokea wala hamsimangi yeyote, anafanya siasa zenye kukipigania anachokiamini atakipata ama anataraji kukipata.

Vijana, viongozi na wanachama wa CHADEMA kuhangaika na kina Zitto, Kitila mkumbo na Anna Mgwira ni kujidharirisha kwa kuonyesha kiwango kidogo cha uelewa wa masuala ya siasa.

Nawapongeza sana baadhi ya viongozi na wanachama wa CHADEMA wanaojikita kila uchao kuhangaika kutafuta suluhu ya changamoto za wananchi wao kama MEYA Boniface Jacob, John Mnyika, David Silinde Mwita Waitara nakadharika.

Muhimu kujua ni kwamba Zama zimebadilika, siasa zimebadilika, siasa za Leo si sawa na siasa za miaka mitano iliyopita.

Siasa za Leo zinahitaji wanasiasa wanaoleta majawabu kwa wananchi wao kuliko kutukanana kila uchao. Mmeshatukanana imetosha sasa wapeni majawabu wananchi.

Ndimi,
Habibu Mchange
0762178678
Mwananchi wa kawaida.
Bando ulilokuwa umepewa limekata nn ?ulitegemea ukishanunuliwa utaitumia hyo pesa maisha yote?...kijiweni hakukaliki sasa tumbo linasikia njaa tena uende wapi sasa...ACT kwenyewe ulishakimbia mwanaizaya wewe...unaanza kulamba miguu zito ili akukumbuke kwenye utawala wake.....pambana na hali yako msaliti mkubwa nyie ndo mnachelewesha ukombozi wa hii inchi kwa njaaa zenu
 
Umeelewa sasa?....
Kwamba hoja wanayoitumia Makamanda haina tena mashiko
Kuwa kigeugeu sio tena issue kwani Chadema wameonyesha ugeugeu kwa vitendo

Halafu ww dogo una siasa fulani za kipuuzi kupita kiasi. Mimi ni mshabiki wa cdm, pamoja na Zitto kuhitilafiana na cdm sikuwahi kumtusi au kumkejeli kutokana na kuuheshimu mchango wake kwa cdm. Ila ilibidi niwe na shaka naye kidogo nilipokuona siku moja ukimtetea Zitto kwa nguvu zako zote ukiwa star tv huku ukiongea siasa za chuki za wazi ambazo sikuwahi kutarajia kuziona kwa kijana kama ww. Kwenye kipindi hicho ulikuwa na Mnyika studioni. Siku ile ulidhani unamtetea Zitto, lakini kama Zitto anahitaji utetezi wa vile basi hata yeye atakuwa ana shida. Na nguvu ile ulikuwa unapewa na Mwigulu kuhusu ugaidi wa Lwakatare ambao mpaka leo haujawahi kuthibitishwa zaidi ya kuingia kwenye siasa chafu na kishenzi ambazo hazijawahi kutokea nchi hii.

Leo hii nikikuangalia huku ukisema hata siasa umeachana nazo ndio nimejua ww ni mtu wa aina gani. Hata hii post uliyoileta hapa ni ya mtindo uleule wa tabia zako za siasa chafu na kujipendekeza. Nadhani wakati unatusi na kukashifu cdm ulidhani kuendesha chama mpaka kupata mafanikio ni jambo rahisi. Ulienda ACT ukiwa na mihemko na ukadhani ACT ingekuwa chama kikubwa sana kuliko cdm kwa kipindi kifupi, lakini kinyume na matamanio yako imekuwa ngumu. Sasa kwa sababu ww ni mtu unayependa mafanikio tu bila kuyahangaikia na aina yako ya siasa chafu umeona aibu huku dhamira ikikusuta ndio ukajifanya umeachana na siasa. Ukweli ni kuwa hujaachana na siasa bali unataka mahali au chama utakachopata hela za bwerere, ukiangalia ni wapi unaweza kupata hizo hela ni ccm tu, na ccm ya sasa hawataki mtu kama ww. Aliyekuwa anashirikiana na ww huko ccm kwenye siasa chafu enzi za JK naye hana sauti enzi hizi za Magufuli.
 
Back
Top Bottom