Tumshauri huyu kijana Mwenzetu

Tumshauri huyu kijana Mwenzetu

ukwama

Senior Member
Joined
Aug 6, 2014
Posts
136
Reaction score
83
Kwanza kabisa natanguliza samahani kwa mhusika kama yumo humu JF maana nimeona niiseme ili hasirudie na nyie wenzangu mmshauri coz nimeona anasmart phone( Samsung S2 nyeupe) sijui ndo katoka kuinunua au kaazimwa au kaiokota maana sio kawaida kwa mtoto wa mjini kama nilivomwona kutumia style kama hiyo kuwasaka warembo wa hapa town.

Leo hii mida ya saa tano asubuh nikiwa kwenye mizunguko yangu hapa na pale nimekutana na kioja kwenye daladala za Ubungo-M/Mbusho via C/Kikuu.Kama ilivyo ada watoto wengi wanapanda huku Mlimani si unajua september conference inawadia? sup ndo muda wake hivo wanaenda kudiscuss na wengine library na wengine huwa wanatumia hii barabara kwenda M/city Kuchukua mahitaji,appointment na wengine wengi kula kiyoyozi cha bure na kuuza sura kwenye hiyo Mall ya Kaburu.

Da mtoto mzuri(rangi maji ya kunde,mrefu wastani.kajazia jazia. .linganisha na wale watoto wa Embassador Choir labda utapata picha) kapanda kunako hiyo daladala yetu na alikuwa ametupia sketi fupi kiaina ya kaki na kivest cheupe akaketi mbele yangu upande wa pili hivo nikawa nampimia vizuri.du,me nikajisemea moyoni Jamani Mungu Fundi,ningekuwa jogoo....

Kumbe wakati huo nafikiria hivo jamaa mmoja bahati nzuri walikaa siti moja na huyo mtoto alikuwa na mawazo yake ila kashindwa kuyapangilia,yule jamaa akampa hi Maskini mtoto wa watu bila shida akaitikia kwa sura ya upole ,jamaa akachomoa msimu wake huo na kuanza kuubonyeza,bonyeza mara aweke sikion mara autoe i na simu. Mara jamaa kajitambulisha "am Bryan,nasoma COET mwaka wa nne,naishi hall 7 na wewe JE?.demu akacheka kidogo. m nae akajb "vizuri unaishi wapi vile? " jamaa tena hall 7 dada akajib OK ,dem akakata stori, jamaa sasa akaanza kuomba contact kwa kumpa huyo dem simu yake ili aandike namba,dem akamwambia siku nyingine ntakupa coz nami naishi hall 7 ,nadhani jamaa hakuelwa. jamaa kuona hivo akaomba email "unajua sisi watu wa huku Mlimani mara nyingi huwa tunatumia email kuwasiliana basi naomba email yako tafadhari ,demu akachomoa, jamaa akaona hisiwe taabu akaanza kumtia voko live unajua Mungu katukutanisha hivo sio vizuri kuachana hvi hvi bila mawasiliano unajua nilipokuona roho yangu imeripuka kwa furaha na bashasha tafadhali naomba unipe mawasiliano , jamaa machozi kama yanamlengalenga machoni hv , demu akachomoa tena.da jamaa muda huo anaangaika mara ajishike kichwa,mara ajishike pua, mara atingishe kichwa kama kasikitika hv hajui atumie mbinu gani coz daladala lishafika utawala na dem anaonekana anataka kushuka jamaa nae akataka aliunge ikiwezekana akawa anamwabia mbona watu wengine hamna hata chembe ya huruma? dem kimya. Mara simu ya huyo dem ikaita(bonge la simu nadhani ni Iphon 7) akapokea na kujibu kama hivi"baby wait for the moment ndo nashuka hapa utawala si upo hill park?".Dem huyo akashuka zake na kuondoka da jamaa akabaki anamtizama yule dada akipotea.

Sasa naombeni tumshauri huyu kijana wetu maana nia anayo ila njia anazotumia ni za zamani na inaonekana atapata taabu sana kuwapata watoto wazuri wa kariba kama ya huyu.

"Watu wangu mnapigwa chini kwa kukosa maarifa"
 
Ina maana alikuwa anatongoza gari zima mnasikia?
 
Mnatabu sana mnaozani wanawake wanapenda hivyo vitu. Usilolijua usiku wa giza majuzi huko kenya kuna binti wa familia ya kitajiri mwenye asili ya kihindi katokea kumpenda jamaa wa familia ya kimaskini. Sasa wewe shindwa kutunza ka boom ufanye maendeleo ukalie kubadilisha smartphone na pamba kali. Mapenzi sio mathematics au physics kwamba kuna fomular kila mtu ana formula zake we kalili tu.
 
Kakuomba umuuombee ushaur humu ndani au kiherehere chako tu???nahisi ww ndo mtongozaji
 
Kama wewe ni mdada' basi your expression sound like a man!! And I guess you are female in JF but your Male in reality.

Story yako It's interesting lakin haina uhalisia kiufipi it's cooked story!!
 
Mxiuuuuuu! HUYO DEMU ANGEKAA HALL 4 SI INGEKUWA BALAAAA? Tena hall 4 masters block!

Sawa the guy alikuja mjini na malory ya kibichi, inshort wakuja haeleweki but yet still angeweza kuwa na nia nzuri sanaa tu! Tena a very noble man with best intentions. Ila kile kuchelewa mjini ndo kumemcost. Japo wakuja he is still a man, tena anatamani warembo vile vile

Afu wadada wana tabia hii mnoo ya kujudge kwa kuangalia first impression. Lile lile bozo akitokea mwanamke akamjali akamrekebisha weeee wanaanza kumgombania. Nyooooo! Angemkataa tu kiutu uzima.

Mi mwenzenu kumkataa mwanaume mbele za watu namuonea imani, na nawaza lingekua bozo kaka yangu back in the days anaingia mjini angejisikiaje? Unamnyongonyeza mjue, vira vyote vinalegea nakujaa upepo! Hahahaaaaa! Unamkataa tu kiutu uzima kama kumgea namba thwn hupokei simu sms hujibu baadae huko ila ushamsitiri mbele za watu. Au unamgea email la kutunga tu kumfichia aibu binadamu mwenzio.
 
kwa uzoefu wangu hapo sioni shida labda kitendo chake cha kuji show up na simu ya kizamani ila anahitaji marekebisho kidogo sana he(boy) is Good kwa sababu
1.Ametangaza nia yake atleast mtima wake hata baada ya kukataliwa umekua mweupe....(formula no 1 ya mabazazi)
2.Ni Jasiri wachache sana wanaweza kutongoza mbele za watu kibaoo(kadamnasi) especially daladala so he got Guts hata huyo mdada aliyetongozwa anajua hiki ni kidume
3.Jamaa hajishtukii anajiamini na anachokifanya remember kukataliwa ni sehemu ya kutongoza duniani kote na formula ya mabazazi ,sipati picha kwa style yake hiyo hiyo anageinasa tu hata hiyo namba ya huyo chick lazima angemuangusha
 
Mxiuuuuuu! HUYO DEMU ANGEKAA HALL 4 SI INGEKUWA BALAAAA? Tena hall 4 masters block!

Sawa the guy alikuja mjini na malory ya kibichi, inshort wakuja haeleweki but yet still angeweza kuwa na nia nzuri sanaa tu! Tena a very noble man with best intentions. Ila kile kuchelewa mjini ndo kumemcost. Japo wakuja he is still a man, tena anatamani warembo vile vile

Afu wadada wana tabia hii mnoo ya kujudge kwa kuangalia first impression. Lile lile bozo akitokea mwanamke akamjali akamrekebisha weeee wanaanza kumgombania. Nyooooo! Angemkataa tu kiutu uzima.

Mi mwenzenu kumkataa mwanaume mbele za watu namuonea imani, na nawaza lingekua bozo kaka yangu back in the days anaingia mjini angejisikiaje? Unamnyongonyeza mjue, vira vyote vinalegea nakujaa upepo! Hahahaaaaa! Unamkataa tu kiutu uzima kama kumgea namba thwn hupokei simu sms hujibu baadae huko ila ushamsitiri mbele za watu. Au unamgea email la kutunga tu kumfichia aibu binadamu mwenzio.

Hahahaa
 
mbona hiyo ndio stail bora kabisa ya kuwin basi imekuwa bahati mbaya kwa mshikaji
 
Kila mwanamke angeweza kujitazama 20 years later maringo yangekwisha....wanaokesha kwa waganga now ili watongozwe na wao wali ringa mno enzi zao
 
Back
Top Bottom