Tumshauri Dr. Joyce Ndalichako

Be serious sometimes! am bored stiff with your none sense comments herein.
 

Hilo tatizo mkuu ni changamoto, linafanana na waliojiendeleza fani tofauti na walioajiriwa nayo, ila ni suala la muda tu litapatiwa ufumbuzi, ila hujatoa alternative maana kwa grade A mtu alipandishiwa mshahara ipasavyo kulingana na muda aliokuwepo kazin, sasa Degree ndio umeipata sasa huwez ukasema uchukue wa Grade uliyofikia then ujumlishe na wa Degree ni ngumu pia inategemea na uhitaji kwenye halmashauri wakati unaenda kusoma labda wao walihitaj huyo wa Grade A.
 

nilimaaanisha wamlipe mshahara kama mtumishi mwenye degree lakini aliekaa muda mrefu kazini nafkiributakua umeelewa nilimaanisha nn mkuu
 
askari kila katikati ya mwezi wanalipwa laki tatu na ushee. kwanini waalimu hawalipwi posho kama hiyo? hata kama mimi nipo sector mbaya/risky, hata wasiponilipa mimi basi wawalipe waalimu...
 
askari kila katikati ya mwezi wanalipwa laki tatu na ushee. kwanini waalimu hawalipwi posho kama hiyo? hata kama mimi nipo sector mbaya/risky, hata wasiponilipa mimi basi wawalipe waalimu...
Upo katika idara/sekta gani mkuu ambayo hauhitaji kulipwa posho hata kama mazingira yako ya kazi ni hatarishi?
 
Pamoja na yote hayo tunamuomba mh waziri ahakikishe anawaondoa katika ofisi za elimu na katika kata (waratibu elimu kata) wote wasiokuwa na sifa na kuwaweka wale wenye sifa stahiki. Kwa mfano hakuna sababu kwa hali ya sasa kuwa na afisa katika ofisi ya elimu au mratibu elimu kata mwenye ngazi ya cheti au stashahada wakati kuna walimu wengi wenye Shahada au Shahada ya uzamili waliopo darasani. Hivi kiuhalisia mratibu mwenye cheti anawezaje kusimamia elimu katika shule ya sekondari iliyopo ktk kata yake? Au mratibu mwenye cheti anawezaje kumsimamia mwalimu mkuu au mkuu wa shule mwenye shahada au Shahada ya uzamili? Tukumbuke kuwa ualimu ni professional na siyo cheo cha kisiasa.
 
Sina shaka na Joyce Ndalichako ni mchapa kazi kweli na hapa Mh. Rais Dr. J.J.Magufuli hajakosea kabisa. Walimu ondoeni wasiwasi.
 
Kwasasa imekuwa kawaida watu waliopata grade hafifu kwenye mitihani ndo wanakwenda ualimu. Na hata wanapokwenda vyuo wengi hupitishwa tu bila kuwa na weledi wa masomo wanayofundisha. Imefika wakati waalimu wapande madaraja kulingana na uwezo wao katika masomo wanayofundisha.

Kwa wale wa sekondari nashauri walimu wafanye mitihani ya kitaifa ya sekondari pamoja na wanafunzi wao kwa masomo wanayofundisha. Kigezo cha kupanda daraja iwe ni ufaulu katika masomo wanayofundisha kwa alama ya A maana mwalimu anatakiwa kuwa mbele ya mwanfunzi. Haina maana mwalimu kulalamika hajapanda daraja kwasabu eti kafundisha miaka fulani. Hii itasaidia maana hawa walimu walishatoka vyuo hawajiangaishi kujiendeleza binafsi kwa kujisomea vitabu. Watu wanajali kupata kazi na mshahara basi tu.

Naomba hili pia lifanyike kwa shule za msingi na walimu wafaulu masomo yote ya msingi kwa alama ya A. Mi nimeona hii njia inatumika kwenye shule binafsi kwa walimu wanaotafuta ajira. Mwalimu anapewa mtihani waliopewa wanafunzi wake na kisha anaambiwa akawasaidie wanafunzi kufanya masahihisho ya mtihani. Walimu wengi hupata maksi ndogo kuliko wanafunzi wanaotaka kuwafundisha. Walimu wengi waliishia kuchekwa na wanafunzi na wakati mwingine kujiondoa wenyewe. Sioni njia nyingine maana watu wakipata ajira hawana mufa wa kujiendeleza wenyewe.
 
Unashauri walimu wafanye mitihani ya wanafunzi ndiya wapandishwe madaraja?
 

Msonda nimesoma naye masters, najua alikuwa mtu wa aina gani. Naomba unyamaze kama unahusudu mtu anayeitwa dr.
 
Tatizo la walimu in walimu waenyewe hivyi kwel kabisa kama wana umoja haswa hii teaching allowance ilipaswa iwepo kitambo tuu,bt bado muda upo wadau wa elimu tuhamasishane sekta ya elimu iboreshwe tupate maendeleo ya kweli tz.
 

Awashuhulikie maafisaelimu wakatili wanowaadhibu walimu ovyoovyo na kuwavunja moyo wa kufanya kazi.Alama 100 za kuwapeleka wanafunzi kiadato cha kwanza ni za chini sana zifike 200.waende sekondari wenye uwezo.Walimu wapandishwe madaraja na kulipwa mapunjo kwa wakaati.Mishahara ya walimu iongezwe kwa 60% ya mishahara ya sasa.Walimu wote waishi karibu na shule.
 
Bro. NECTA hawahusiki na malipo YA wasimamizi mitihani, mhusika ni wakurugenzi wa halmashauri, manispaa na majiji.

Hiyo michango ya Tsh.50,000 ya watahiniwa kama gharama ya mtihani, huwa anaiweka nani mfukoni?
 
kwa ukitaka kuchukua uafisaelimu wa mtu watu wakachukue masters tu, wenye masters wakimaliza vyeo watapelekwa wapi. Watu wanasoma kuboresha utendaji wao sio kuangusha vyeo vya watu!
Mkuu ndioo maana wana mawazo finyuu saana hatakutoa maamuzii yaoo, kazi kuwatisha walimu na kuwa nyanyasa pasipoo sababu, yotee hayoo ni elimu ndogoo, . Wakasomee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…