Tumlazimishe Mhe. Magufuli awe Rais hadi 2035

Abby Newton

JF-Expert Member
Nov 12, 2017
1,227
2,197
Mwaka 2018 Jamuhuri ya China walirekebisha Katiba yao na kumfanya Rais wao wa sasa Xi Jiping kuwa Rais wa maisha. Hawajafanya marekebisho haya kwa bahati mbaya bali ni kwa sababu Rais Jiping kaifanya China kupiga hatua kubwa kimaendeleo hali inayopelekea kukaribia kuipita Marekani na kuwa Taifa la kwanza kiuchumi Duniani.

Urusi nao watapiga kura siku chache zijazo kumuongezea muda Rais Putin ili aongoze hadi 2036. Urusi na China ni mataifa makubwa yaliyoendelea kila nyanja lakini wanafanya haya kwanini sisi tusifanye hasa baada ya kumpata Rais mwenye sifa tuliyoitaka kwa muda mrefu?

Wajerumani wenyewe Kansela wao bi Anjela Merkel ameongoza kwa miaka takribani 14. Tujiulize kwanini wao na sio sisi?

"Great people are not born every day". Baada ya kuondoka Nyerere sote tunajua ni jinsi gani nchi yetu iliparaganyika. Leo tuna Rais Jasiri, asiyependa Rushwa, ana hofu na Mungu, Mkali, anasimamia maadili ya watumishi, Ana maono, anapenda maendeleo,haogopi mabeberu, Mungu atupe nini Watanzania halafu eti tukubali kumuachia? Kwanini hatutaki kufundishwa na historia?

Wazungu kamwe hawatapenda kuona kiongozi kama Magufuli anaongoza kwa mda mrefu,kwani kawashika pabaya. Hawapi mda wa kupumua walizoea kutugeuza shamba la bibi. Nilazima tuwaonyeshe kwamba sio yeye anaetaka madaraka kwa nguvu bali ni sisi wananchi ndio tunamtaka atuongoze.

Magufuli ni lulu kama ilivyo kwa Xi Jiping, na Putin. Hawa ni viongozi wenye uzalendo wa hali ya juu na ni vigumu kuwapata wa namna hiyo kwa karne hii ya d.com.

Magufuli kafanya mengi mno kwa mda mfupi bado tunahitaji vingi kutoka kwake. Kumuacha aondoke ni sawa na kutema "Bublish" ikiwa bado na utamu.
 
KAMA WAZEE (ruksa /utandawazi /, za kuambia changanya na zako ) WAKISEMA TU LOLOTE KUHUSU HILO, (hapa kazi tu) hawezi kataa, maana wao waliacha marafiki zao (RICHMOND-FIXER, ex-TISS) wakamchagua wao, so kama unataka hii kitu ifaulu basi wazee wa3 ndo waseme.
 
Hints: Zingatia komment yangu hapo juu, maana (hapa kazi tu) HAWEZI PINGA LOLOTE KUTOKA KWA WAZEE.
 
Kwanini msifanye kuwa mungu wenu kabisa?
Kama mnaamini na yeye anaamini anaweza kuongoza hata malaika, kwanini msimteue kuwa mungu wenu?
Kwanini kuna tatizo?
 
Abby Newton,

Mkuu CCM inawanachama wangapi? Yaani wote hao mwenye sifa ya kuwa rais CCM ni mmoja tu? Mbaya zaidi mwenyewe kasema hataki.
 
Usifananishe nchi zilizoendelea na sisi ambao wao hawategemei tena kiongozi fulani abadilishe nchi ila ni mikakati na ilani za mda mrefu hivyo hata aje kiongozi gani zinafuata.

Africa viongozi wengi ni wapenda madaraka na kujilimbikizia mamlaka, tumesahau juzi tu wamepitisha sheria ya kutoshitakiwa huku wakiacha vitu muhimu kama katiba na sheria ya dhamana, hivi hawa wakiongozewa mda watafanya nn tena? Ikiwa wanaonyesha wapo kwa masirahia ya wenyewe.
 
Wewe u miongoni mwa watu wenye fikra duni, umaskini na ukosefu wa elimu kwa watu maskini ni mambo yanayoratibiwa na CCM ile ile ya Magufuli halafu leo unaleta wazo JPM aendelee kuwa rais?

Damn you!!
 
Mkuu nianze kuandika kwamba huo mtizamo wako ni sahihi kwa uchambuzi wa miaka5 ya uongozi wake. Kwa nnavyoelewa Tanzania ni inchi ya Demokrasia huru na inaongozwa na katiba yake kwa maswala yote yq uongozi, inapokuja juu ya wananchi na viongozi wetu wakuu ni wapenda matukio nd9 huchochea maamuzi ya kumweka madarakani au kumpigia kura mhusika.

Mh Rais kwanza alipita katika mçhujo ndani ya chama tawala kutokana na hali ulivyokua wakat huo 2015 kua wa mvurugano na alisoma alama ya nyakati ndo maana kwa shinikizo la wakati huo amefanikiwa kuyafanya haya kwa miaka5.

Kila kitu na wkt wake binafsi siamini ktk kumuongezea zaidi ya miaka 10 kikatiba ya sasa sababu ni nyingi ikiwemo katiba kutokuruhusu pia sie ni binaadamu mkuu ana utashi wake sitqk kuamini ana uwezo kubaki hivi kwa miaka15-20 zaid ya hapo. Pia ameshasema hana mpango wa kyongeza zaidi ya miaka yake kikatiba, lawama ni nyingi pia hivyo isije baadae kutaka badiliko ambàlo kimsingi litatugharimu zaidi.

Namuunga mkono kwa haya anayofanya na pia bado inatubidi kusonga zaidi ya hapa nakwa nyakati tofauti lkn bado tutahitqji tofauti ya viongozi wetu na vyama tofsuti kufika tunapotaka, hayo ya mataifa mengine tuwaachie wao kwan hatuwezi kuongoza kwa kufuata wao. Mwisho hongera kwa Taifa la Malawi na tume zao kwa uchaguzi safi bila kumsahau Raisi aliepita kwa ukomavu wake kisiasa na kutuaminisha inawezekana kwa inchi kua na utawala bora kwa maendeleo ya taifa zima kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom