Ng'wamapalala
JF-Expert Member
- Jun 9, 2011
- 6,811
- 6,506
Mwaka 2008 baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu nafasi yake. Mizengo Pinda aliyeshika nafasi yake alitarajiwa kuja na moto mkali zaidi wa kiutendaji. Kuna baadhi ya Watanzania walishangilia sana ujio wa Mizengo Pinda.
Itakumbukwa kuwa Lowassa aliyeangushwa na kashfa ya mradi tata wa umeme wa Richmond, alishaanza kuonyesha machachari yake hasa katika kusimamia suala la elimu ambapo alihamasisha ujenzi wa shule za sekondari za kata na miradi mingine.
Pinda aliingia akiwa amevaa ngozi ya kondoo, huku akijiita mtoto wa mkulima. Leo ni miaka zaidi ya saba imepita, tunamwona Pinda halisi alivyo. Kuna kila dalili kwamba amepwaya katika nafasi hiyo.
Tofauti na walivyokuwa mawaziri wakuu wengine, Pinda hajaonyesha ubunifu katika mambo mbali mbali na kuyasimamia. Badala yake amekuwa mtu wa kuonekana wakati wa matukio huku ukitaka uongozi wake tuupime katika mzani wa upole na umasikini. Uongozi wa Tanzania hauwezi kupimwa pekee katika mzani wa upole na umasikini. Hatuwezi kuwa na kiongozi anayejivunia umasikini katika Taifa lenye mazingira ya market economy. Umasikini si turufu ya uongozi, bali kiongozi mzuri ni yule anayekerwa na umasikini badala ya kuutukuza na kuuenzi, ndiyo maana kila siku watanzania wengi wanatafuta njia ya kupambana na umasikini.
Kukitokea vurugu, wananchi wa Mtwara wameandamana, Waziri Mkuu Pinda anakwenda kutuliza, madaktari wamegoma, anakwenda kuzungumza nao, wenye malori na mabasi wamegoma, anakwenda kuwabembeleza.
Nchi hii ilipofika, hatuhitaji kiongozi atakayeridhisha watu bali kiongozi atakayetoa dira ya Taifa inayojari Taifa ili tuvuke na kufika salama kule wananchi wanataka Taifa lifike. Mchekeshaji maarufu duniani, Bill Cosby, aliwahi kusema; ''I don't know the key to success, but the key to failure is trying to please everybody''. Kwa lugha ya mashuleni kijijini Bariadi, alimaanisha kuwa, hajui njia ya kuyafikia mafanikio, lakini njia ya kutofanikiwa ni kumridhisha kila mtu.
Huu ni udhaifu, haiwezekani kiongozi ashughulikie matukio tu wakati anaweza kuboresha utendaji ili mambo yasiharibike. Kutokana na udhaifu huo, hata mawaziri walio chini yake hawawajibiki ipasavyo na wale wachache wanaowajika, anajitokeza na kuwapiga stop. Ndiyo maana hivi karibuni, Wabunge walimtaja kuwa mmoja kati ya mawaziri wanaopaswa kuwajibika kutokana na kushindwa kusimamia kazi zao.
Nilipatwa na mshangao baada ya kukutana vichwa vya habari vinavyosema ''WAZIRI MKUU PINDA AMUONYA VIKALI MAGUFULI'', vingine vilisema, '' SERIKALI YAMZIMA MAGUFULI''.
Ndani yake kulikuwa na habari inayosema,
Kilichonifanya kuduwaa na kushangaa zaidi ni pale Pinda aliponukuliwa akisema,
Mizengo Pinda amesomea sheria na lazima aelewe kuwa sheria inapotungwa na kupitishwa, hakuna tena majadiliano. Kwa macho ya Mizengo Pinda, kosa la Magufuli ni kuilinda hiyo sheria bila kuwashirikisha wanaoivunja. Jamani, unapomkamata mwizi unamshirikishaje? Unashauriana naye nini ili mpate uamuzi wa pamoja kama siyo kuanza kujenga mazingira ya rushwa?.
Huyu ndiyo eti anataka awe Rais ili aweze kupambana na ufisadi achilia mbali makampuni makubwa ya kimataifa ambayo mengine yana dictate foreign policy za mataifa ya Magharibi. This is fun to say the least.
Kikubwa zaidi, Mizengo Pinda alishatamka hana nia ya kuwa Rais wa Tanzania kama alivyonukuliwa na Januari 25, mwaka 2012 akisema,
Ni nini tena kimemtuma/kimemkuta atake kuwa mgombea Urais?. Watanzania tusikubali kufanywa wajinga na wanasiasa aina ya Mizengo Pinda. Lazima tuwakatae kwa nguvu zote.
Wanasiasa wa aina ya Mizengo Pinda hawafai, hawatufai na hawalifai Taifa. Ni bora waende kuangalia na kuendeleza mashamba yao ya zabibu na kuchunga ng'ombe.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaongoza viongozi wa Kanisa la Anglican kutembelea shamba la zabibu na malisho ya ng'ombe kwenye shamba lake lililopo Zuzu Dodoma Februari 9, 2015. Baadhi ya viongozi hao ambao walikwenda kujifunza kwa lengo la kuanzisha shamba linalofanana na hilo Dodoma ni Askofu Dickson Chilongani wa Dayosisi ya Dodoma (wapili kushoto), Askofu Maimbo Mndolwa wa Dayosisi ya Tanga (kulia kwake) na kulia ni Re. Canon, Johnson Chinyongole ambaye ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo
Itakumbukwa kuwa Lowassa aliyeangushwa na kashfa ya mradi tata wa umeme wa Richmond, alishaanza kuonyesha machachari yake hasa katika kusimamia suala la elimu ambapo alihamasisha ujenzi wa shule za sekondari za kata na miradi mingine.
Pinda aliingia akiwa amevaa ngozi ya kondoo, huku akijiita mtoto wa mkulima. Leo ni miaka zaidi ya saba imepita, tunamwona Pinda halisi alivyo. Kuna kila dalili kwamba amepwaya katika nafasi hiyo.
Tofauti na walivyokuwa mawaziri wakuu wengine, Pinda hajaonyesha ubunifu katika mambo mbali mbali na kuyasimamia. Badala yake amekuwa mtu wa kuonekana wakati wa matukio huku ukitaka uongozi wake tuupime katika mzani wa upole na umasikini. Uongozi wa Tanzania hauwezi kupimwa pekee katika mzani wa upole na umasikini. Hatuwezi kuwa na kiongozi anayejivunia umasikini katika Taifa lenye mazingira ya market economy. Umasikini si turufu ya uongozi, bali kiongozi mzuri ni yule anayekerwa na umasikini badala ya kuutukuza na kuuenzi, ndiyo maana kila siku watanzania wengi wanatafuta njia ya kupambana na umasikini.
Kukitokea vurugu, wananchi wa Mtwara wameandamana, Waziri Mkuu Pinda anakwenda kutuliza, madaktari wamegoma, anakwenda kuzungumza nao, wenye malori na mabasi wamegoma, anakwenda kuwabembeleza.
Nchi hii ilipofika, hatuhitaji kiongozi atakayeridhisha watu bali kiongozi atakayetoa dira ya Taifa inayojari Taifa ili tuvuke na kufika salama kule wananchi wanataka Taifa lifike. Mchekeshaji maarufu duniani, Bill Cosby, aliwahi kusema; ''I don't know the key to success, but the key to failure is trying to please everybody''. Kwa lugha ya mashuleni kijijini Bariadi, alimaanisha kuwa, hajui njia ya kuyafikia mafanikio, lakini njia ya kutofanikiwa ni kumridhisha kila mtu.
Huu ni udhaifu, haiwezekani kiongozi ashughulikie matukio tu wakati anaweza kuboresha utendaji ili mambo yasiharibike. Kutokana na udhaifu huo, hata mawaziri walio chini yake hawawajibiki ipasavyo na wale wachache wanaowajika, anajitokeza na kuwapiga stop. Ndiyo maana hivi karibuni, Wabunge walimtaja kuwa mmoja kati ya mawaziri wanaopaswa kuwajibika kutokana na kushindwa kusimamia kazi zao.
Nilipatwa na mshangao baada ya kukutana vichwa vya habari vinavyosema ''WAZIRI MKUU PINDA AMUONYA VIKALI MAGUFULI'', vingine vilisema, '' SERIKALI YAMZIMA MAGUFULI''.
Ndani yake kulikuwa na habari inayosema,
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amemuonya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli kwa mara nyingine tena kuacha tabia ya kufanya uamuzi wa jambo lolote bila kushirikisha pande zinazohusika.
Mbali ya karipio hilo, Waziri Mkuu amewataka viongozi wengine wa Serikali, kuepuka mfumo usio shirikishi katika uamuzi wao kwa kuwa unasababisha migogoro ndani ya jamii na usumbufu kwa Serikali.
Kilichonifanya kuduwaa na kushangaa zaidi ni pale Pinda aliponukuliwa akisema,
Yaani Magufuli anayezilinda barabara zetu kwa kutumia sheria zilizopo ili zisife mapema anampiga stop eti ashauriane kwanza na wale wanaotakiwa kufuata sheria. Sheria ikishatungwa na kupitishwa haiwezi tena kutaka mashauriano ili kuifuata. Huu siyo muswada wa sheria.''Hatua zilizochukuliwa na Dk. Magufuli kufuta vifungu vilivyokuwa vikiruhusu asilimia tano zilifuata sheria, lakini tatizo lililojitokeza ni kutoshirikisha pande zinazohusika ili kushauriana na kupata uamuzi wa pamoja. Mbali ya kutoshirikisha pande hizo, uamuzi wa Dk. Magufuli ulikuwa wa ghafla kwa wasafirishaji kitendo ambacho kimewapa wakati mgumu wa utekelezaji, kwa sababu wafanyabiashara walikuwa wameingia mikataba na wateja wao''
Mizengo Pinda amesomea sheria na lazima aelewe kuwa sheria inapotungwa na kupitishwa, hakuna tena majadiliano. Kwa macho ya Mizengo Pinda, kosa la Magufuli ni kuilinda hiyo sheria bila kuwashirikisha wanaoivunja. Jamani, unapomkamata mwizi unamshirikishaje? Unashauriana naye nini ili mpate uamuzi wa pamoja kama siyo kuanza kujenga mazingira ya rushwa?.
Huyu ndiyo eti anataka awe Rais ili aweze kupambana na ufisadi achilia mbali makampuni makubwa ya kimataifa ambayo mengine yana dictate foreign policy za mataifa ya Magharibi. This is fun to say the least.
Kikubwa zaidi, Mizengo Pinda alishatamka hana nia ya kuwa Rais wa Tanzania kama alivyonukuliwa na Januari 25, mwaka 2012 akisema,
Unaweza kusoma interview yake kupitia hapa,"Niliposema sitawania urais nilimaanisha hivyo na naomba watu wanielewe, urais si kazi ya kukimbilia kama kweli unataka kuwatumikia watu, kwa wale wanaotaka kwenda kuchuma sawa ni pazuri, lakini mimi naona ni mzigo, kuna wakati namwonea huruma Rais Kikwete maana kila kitu kigumu anaangushiwa yeye,"
Ni nini tena kimemtuma/kimemkuta atake kuwa mgombea Urais?. Watanzania tusikubali kufanywa wajinga na wanasiasa aina ya Mizengo Pinda. Lazima tuwakatae kwa nguvu zote.
Wanasiasa wa aina ya Mizengo Pinda hawafai, hawatufai na hawalifai Taifa. Ni bora waende kuangalia na kuendeleza mashamba yao ya zabibu na kuchunga ng'ombe.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaongoza viongozi wa Kanisa la Anglican kutembelea shamba la zabibu na malisho ya ng'ombe kwenye shamba lake lililopo Zuzu Dodoma Februari 9, 2015. Baadhi ya viongozi hao ambao walikwenda kujifunza kwa lengo la kuanzisha shamba linalofanana na hilo Dodoma ni Askofu Dickson Chilongani wa Dayosisi ya Dodoma (wapili kushoto), Askofu Maimbo Mndolwa wa Dayosisi ya Tanga (kulia kwake) na kulia ni Re. Canon, Johnson Chinyongole ambaye ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo