Mkuu,Acha uongo wewe na wachangiaji wako ambao wote mpo timu moja, ivi unafikiri Pibda utamlinganisha na huyo wa kwenu?
Kuna wale pia wanaodai kulinda/kutetea sheria kwa kuvunja sheria, hawa pia hawatufai!Kiongozi anayeona aibu kutetea sheria za nchi huku akiogopa kuliathiri kundi fulani hafai hata kidogo katika kutetea maslahi ya taifa.
Nafasi ya viongozi wa aina hii ni kwenye makanisa ni misikitini.
Mizengo Pinda hatufai na hafai kuliongoza taifa.
kiongozi makini ni yule anayefanya maamuzi kwa hekima. moja ya mawaziri wanaoitia hasara serikali kwa maamuzi yake ni dk magufuli kuna madeni makubwa ya fidia yaliyotokana maamuzi tata kiongozi makini ushirikisha wataalam na washauri katika maamuzi tatizo watu wengi wanaompinga mh pinda ni mafisadi wezi wa mali ya umma ambao wanakimbilia ikulu kwenda kufanya ujangili
Tangu uhuru nch hii haijawahi kupata waziri mkuu bomu kama mizengo kayanza pita pinda.CCM tumebaki na mtu makin mmoja tu nae ni stephen WASIRA
siku moja Wasira naye kwenye pati kaukasi alisema kama mbunge hawezi kumpinga rais kwasababu ni rais wake!!. pia ni mlalamishi sana. kwenye mchango wake mjadala wa escrow akasema ''kuna mtu tajiri anaetaka urais anatuvuruga''. juzi kavaa koti vibaya anamlalamikia membe. hii miwatu lalamishi na yakutia hurumahuruma ni yakuikataa kabisa.
Uchambuzi mzuri sana wa Ng'wamapalala.
Pinda ni furushi zito ambalo haliwezi kubebeka na jamii yoyote inayotaka maendeleo. Huwezi kuongoza na kupata mafanikio kama una compromise na sheria. Kwa ujumla uongozi wa Kikwete kwa kiasi kikubwa umeshindwa kwa sababu ya kutosimamia sheria na tamaa ya kutaka kumridhisha kila mtu.
Hakuna kiongozi anayeweza kumrudhisha kila mtu, ukiona kiongozi anaridhisha kila mtu yaani wanaoibiwa waridhike, wanaoiba waridhike, utambue kiongozi huyo ni mnafiki maana haiwezekani wewe mtu mmoja upende kuiba na uchukie kuiba.
Combination ya Pinda na Kikwete ilikuwa mbaya kabisa maana wote wana hulka zinazolingana, kutopenda kusimamia sheria na kupenda kumridhisha kila mtu.
Tanzania has lost nearly 8 years to no national direction and directional leadership.
Tumevumila udhaifu wa Pinda kwa karibia miaka 8, halafu eti anataka kuwa Rais. Kwa nchi zenye uongozi madhubuti, Pinda hakustahili kuwa hata Mkuu wa Mkoa.