Hizi simu zina camera sio kwa sababu ya kupigia picha za insta. Wala hizi simu hazina mitandao kwa ajili ya kufanyia umbea kwenye What's Up.
Polisi wanachukua rushwa barabarani na simu mnazo. Wakimuita mtu pembeni wachukueni video. Kama ni kumuandikia mtu faini wamuandikie hadharani.
Na nyie wakuu wa polisi hakikisheni polisi wenu wanaelewa kuwa ukeshia sio kazi yao. Polisi hakusanyi hela yeyote barabarani. Anandika faini tu.
Tukio lolote la uhalifu piga video weka kwenye mtandao. Ndivyo wanavyofanya wenzetu nchi zilizoendelea.