Tumetoka mbali Sana, lakini hanithamini!

Tumetoka mbali Sana, lakini hanithamini!

Mama yangu alipatwa na kisa kama chako. Mwenyewe anasema katika maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya kwenye maisha yake ni kuamua kuachana na Baba yangu bila hata ya mzee kusema rasmi waachane. Walikuwa wameshanileta duniani na mama mpaka kesho nadhani atakuambia kwamba mzee wangu ndo mtu aliyepanga kuolewa naye lakini ndo hivyo, mwenyewe anasemaga "ndo maisha hayo utafanyaje?". Japokuwa anakiri kuwa mzee wangu hakuwahi kumuahidi kwamba atamuoa lakini mwenyewe anasema baada ya kuwa na mahusiano na mtu kwa muda wa miaka minne na kuzaa nae mtoto alifikiria kwamba wataoana. Kumbe mwenzake alikuwa anafikiria vingine.

Sio siri maisha yetu wakati nakua yalikuwa magumu kinoma ila Mungu anajua yule mwanamke alipigana kadri ya uwezo wake. Nakumbuka siku moja mama alirudi nyumbani na mshahara wake akatuita mimi na wadogo zake na ndugu na zangu tuliokuwa bado tunasoma akagawa ile hela yote kwenye ada na tuition na madeni ya chakula. Jioni ilipofika mama inabidi aende kazini (shift ya usiku hospitalini) ikabidi akope tena ili apate nauli ya kwenda kazini, wakati huo nauli ya kwenda mji unaoitwa Pongwe kutoka Tanga mjini ilikuwa shilingi 100 nadhani.


Long story short, hamna mtu ninae mthamini kwenye maisha yangu kama Mama yangu. Naomba sana Mungu aniweke duniani na anipe mafanikio ili nimtimizie Mama yangu ndoto zake zote za maisha.Kwa kweli hata kwenye maisha naheshimu sana wanawake haswa wa kiafrika maana wengi wao wanapitia hizi changamoto kwenye maisha yao.


Sina ushauri wa kukupa lakini labda unaweza kurelate with your situation. Keep your head up, fight, and do what's best for your child, trust me we never forget.

P.S. - Mimi na mzee wangu tupo cool tu, alikuja kuniomba radhi baadae kwa kutokuwepo kwake kwenye udogo wangu.
 
Asanteni kwa ushauri;kwa wale waliotaka kujua Nina umri ni miaka 25 naninafanya kazi ya secretary katika kampuni moja mjini
 
ndio matatizo hayo kuanza mapenz na kapela akija kupata anatafuta wanawake wanaojua matumiz, we si ndio unajua kuvumilia shida kwahiyo humfai tena kwa kipindi hiki. Baki hivyohvyo mpaka uje utimuliwe ndani ndio ujue kuwa hutakiwi. we km ni mtu mzima na mwelewa, mwanaume akishakuambia hayo basi ujue tu kashaanza michepuko
 
Fanya yako shost, jiamini, maisha yanawezekana bila yeye.
Mimi mwenyewe yalinisibu kama yako, mtu nimemvumilia weeee kaja kupata kazi akaanza kunionyesha vituko vya kila rangi. piga moyo konde fanya yako.
Pia usisahau kuomba Mungu akupe mwenye kheri na wewe.
Kumbe ni kilio cha wengi....Mama S fata ushauri kwa waliokutangulia na majanga haya..
 
Mama yangu alipatwa na kisa kama chako. Mwenyewe anasema katika maamuzi magumu aliyowahi kuyafanya kwenye maisha yake ni kuamua kuachana na Baba yangu bila hata ya mzee kusema rasmi waachane. Walikuwa wameshanileta duniani na mama mpaka kesho nadhani atakuambia kwamba mzee wangu ndo mtu aliyepanga kuolewa naye lakini ndo hivyo, mwenyewe anasemaga "ndo maisha hayo utafanyaje?". Japokuwa anakiri kuwa mzee wangu hakuwahi kumuahidi kwamba atamuoa lakini mwenyewe anasema baada ya kuwa na mahusiano na mtu kwa muda wa miaka minne na kuzaa nae mtoto alifikiria kwamba wataoana. Kumbe mwenzake alikuwa anafikiria vingine.

Sio siri maisha yetu wakati nakua yalikuwa magumu kinoma ila Mungu anajua yule mwanamke alipigana kadri ya uwezo wake. Nakumbuka siku moja mama alirudi nyumbani na mshahara wake akatuita mimi na wadogo zake na ndugu na zangu tuliokuwa bado tunasoma akagawa ile hela yote kwenye ada na tuition na madeni ya chakula. Jioni ilipofika mama inabidi aende kazini (shift ya usiku hospitalini) ikabidi akope tena ili apate nauli ya kwenda kazini, wakati huo nauli ya kwenda mji unaoitwa Pongwe kutoka Tanga mjini ilikuwa shilingi 100 nadhani.


Long story short, hamna mtu ninae mthamini kwenye maisha yangu kama Mama yangu. Naomba sana Mungu aniweke duniani na anipe mafanikio ili nimtimizie Mama yangu ndoto zake zote za maisha.Kwa kweli hata kwenye maisha naheshimu sana wanawake haswa wa kiafrika maana wengi wao wanapitia hizi changamoto kwenye maisha yao.


Sina ushauri wa kukupa lakini labda unaweza kurelate with your situation. Keep your head up, fight, and do what's best for your child, trust me we never forget.

P.S. - Mimi na mzee wangu tupo cool tu, alikuja kuniomba radhi baadae kwa kutokuwepo kwake kwenye udogo wangu.
Imenigusa sana.....
 
Asanteni kwa ushauri;kwa wale waliotaka kujua Nina umri ni miaka 25 naninafanya kazi ya secretary katika kampuni moja mjini

Mama yangu alikuwa na umri huo huo ulionao wakati ananizaa mimi kwa bahati mbaya zaidi yeye bado alikuwa chuo na nyumbani kwao wakulima, afu yeye ndo alikuwa mtoto wa kwanza. Haikuwa rahisi lakini alijitahidi hivyo hivyo.
 
Imenigusa sana.....


We acha tu. Kuandika tu hiyo comment nimejisikia kulia. Sidhani kama kuna kitu chochote naweza kufanya dunia hii kumlipa. Anyways enough of that, I don't wanna get too emotional now, it's uncomfortable for us guys.
 
Pole sana mkuu wengine wakipata kidogo huwa wanabadilika kitabia. Sasa anza maisha yako jishughulishe Mungu atakubariki na wewe utatoka kwa wakati wako. Ijapokua unampenda hakufai tulia.
 
Asanteni kwa ushauri;kwa wale waliotaka kujua Nina umri ni miaka 25 naninafanya kazi ya secretary katika kampuni moja mjini
Kumbe bado mdogo. Usiwe na wasi wasi wala usijilazimishe kuishi na huyo ndugu kumbuka umri wako una mengi waweza kufanya na haya mengine yakabaki historia. Usiendelee kupoteza muda wako jipange upya na umuombe Mungu akubariki na naamini utafanikiwa na hii itakua hadithi.
 
Dada ni ulimbuken wa huyo mtu baada ya kupata pesa mpotezee tu siku akisimamishwa kazi atakutafuta
 
We acha tu. Kuandika tu hiyo comment nimejisikia kulia. Sidhani kama kuna kitu chochote naweza kufanya dunia hii kumlipa. Anyways enough of that, I don't wanna get too emotional now, it's uncomfortable for us guys.
Its true
 
mama S wewe unajishughulisha na nini!!!!!!!!!!!!!!!

Swali zuri , kama ana kazi inayomuingizia kipato aendelee na mambo yake. Jamaa atakapogundua aliokuwa anawafuata wanamchuna atarudi mwenyewe tu.!
 
Last edited by a moderator:
Haya wamekusikia watajifunza madhara ya kuanza kugawa tunda kabla ya kuolewa,ungemnyima tunda angekuwa bado anakupenda maskini!...basi we achana naye ila uachane na huu mchezo wa kugawa kabla, Mungu ni mwingi wa rehema atakusaidia.
 
Asanteni kwa ushauri;kwa wale waliotaka kujua Nina umri ni miaka 25 naninafanya kazi ya secretary katika kampuni moja mjini

Jipende sana. Bado una umri mdogo na maisha marefu Mungu akikujaalia.
Fanya kazi kwa bidii na umtegee Mungu siku zote. Mwishoni kitaeleweka tu, kama ni kurudi basi atakuja akiwa na heshima au unaweza ukakutana na mwingine akawa tofauti na mkapendana vizuri tu.
Vyovyote itakavyokuwa, usiruhusu akuumize na kukuburuza buruza kihisia. Hiyo huwa inaharibu sana kujiamini kwako na unaweza ukashindwa kufanya mambo mengine. Ndio maana tunakushauri umpe muda afanye mambo yake kwanza.
 
Hapo ndipo mapenz yanapogeuka kero ukiona mwanaume anapata hela anasahau umaskini wake wala usipige nae kelele mpe macho ni limbukeni na ucdhani atakuelewa kwa ss hpn subir akiishiwa ndo atakukumbuka ndo pakumnawa ss yanamwisho hayo
 
Swali zuri , kama ana kazi inayomuingizia kipato aendelee na mambo yake. Jamaa atakapogundua aliokuwa anawafuata wanamchuna atarudi mwenyewe tu.!

kazi anayo kumbe na still ndo yuko 25 bado ana long way to go kuanza kijistress na huyo mwanaume

AKIAMUA anaweza
 
Back
Top Bottom