Tumeshinda ila tumeshindwa kusherekea ushindi

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
539
3,507
Waangalizi wengi wa uchaguzi hasa barani Afrika wanakuwa ni watumishi wa umma walioteuliwa na Serikali zao kuja kujifunza namna uchaguzi ulivyoendeshwa lakini pia kupata mbinu mpya za kuwashauri watawala namna ya kushindi chaguzi zijazo.

Ni mara chache sana waangalizi wa nje wasiotokana na mfumo wa serikali kuruhusiwa kuingia nchi yenye uchaguzi kwa shughuli za uangalizi. Kwa waangalizi wa ndani ambao wengi wao ni asasi za kiraia mara nyingi ufungwa na tamaduni, taratibu na misismamo ya kisiasa ya wagombea.

Kuwategemea waangalizi hawa kwenda kinyume na matakwa ya regime iliyopo ni vigumu kwa sababu kwa asilimia kubwa awalindwi na sheria bali ukingiwa kifua na watawala waliopo.

Kwa tafsiri hii, MWANGALIZI SAHIHI WA UCHAGUZI NA ANAYEWEZA AKAELEZA UKWELI WA KILICHOTOKEA NI MWANANCHI PEKEE.

Hivyo kwa anayetaka kujua uchaguzi ulikuwa huru na haki wauliza wapiga kura, angalia nyuso zao, sikiliza majadiliano yao, angalia mienendo yao ukiona wanajadili chini chini, ukiona awashangilii bali wanaendelea na shughuli zao basi jua hakukuwa na uhuru wala haki.
 
Tuliacha pesa za UNDP kwa sababu ukizichukua ni lazima uruhusu waangalizi wa kimataifa na pesa hizo ni free lakini tukatumia pesa zetu ambazo zingesaidia kutujengea vituo vya afya nk ili tu kusiwepo na waangalizi wa kimataifa na tuweze kufanya kile cha ajabu kilichotokea kwenye uchaguzi huu.

Kwa upande wa waangalizi wa ndani, taasisi kubwa kama ile ya Haki za Binadamu Tanzania ambazo zina nguvu ya uchumi kuweza kuweka waangalizi wengi Tanzania nzima, hazikupitishwa kuwa sehemu ya waangalizi wa ndani. Badala yake vikawekwa vitasisi vya makada ambavyo vimetoa kiripoti chao cha kurasa mbili na kusema kila kitu kilikuwa kizuri bila hata kuonesha changamoto zozote.
 
Inaitwa "connecting the dots and with hind sight". Ukingalia nyuma utaona kwa nini msaada wa UNDP/EU/ USA ulikataliwa. Walikuwa tayari wamekwisha amua mpango wa kupigia kura majumbani mwao na kuzileta vituoni kwenye mabegi na vikapu. Walijua kuwa ni kitu ambacho UNDP/EU/USA wangelipinga vikali.
Hakuna waangalizi Africa kuna wababaishaji
 
Back
Top Bottom