Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 576
Mkuchika na Wasira kwa nyakati tofauti wamenukuliwa na vyombo vya habari wakipumua kwamba "Wale wanaodhani Uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha utarudiwa wasahau kwani uchaguzi ulishafanyika kwa kufuata kanuni zilzopo, CCM ndio wameshinda. Mwenye kutengua matokeo haya na mahakama tu, serikali haina uwezo wa kutengua"
Inaashiria kuwa ni kauli rasmi ya serikali na kwamba serikali hiyo inaenzi uchakachuaji. Sasa serikali ikishasema hayo raia ufanyeje? Maana mahakama inaagizwa kufuata kilichoamuliwa na serikali. Rejea kesi ya Mtikila kudai mgombea binafsi. Pamoja na Mtikila kushinda mahakamani bado serikali ikakata rufaa na hatimaye wakaamua kugoma kabisa kuruhusu, badala yake wakaandika mswada mpya wa kuzuia hilo.
Serikali yetu ipo kulinda mabavu ya watawala na sio haki za wanyonge. Lugha zao nzuri wakati wa uchaguzi na ni chungu ghafla uchaguzi ukiisha.
Inaashiria kuwa ni kauli rasmi ya serikali na kwamba serikali hiyo inaenzi uchakachuaji. Sasa serikali ikishasema hayo raia ufanyeje? Maana mahakama inaagizwa kufuata kilichoamuliwa na serikali. Rejea kesi ya Mtikila kudai mgombea binafsi. Pamoja na Mtikila kushinda mahakamani bado serikali ikakata rufaa na hatimaye wakaamua kugoma kabisa kuruhusu, badala yake wakaandika mswada mpya wa kuzuia hilo.
Serikali yetu ipo kulinda mabavu ya watawala na sio haki za wanyonge. Lugha zao nzuri wakati wa uchaguzi na ni chungu ghafla uchaguzi ukiisha.