Tumekuwa washabiki,hatufikiri tena

Tumekuwa washabiki,hatufikiri tena

swagazetu

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
4,253
Reaction score
1,475
Nimekuwa fb na jf sasa naona uwezo wa watanzania umefika ukomo japo si wote.ukiangalia mijadala mingi haijibiwi kwa hoja ila kwa ushabiki na uchama.hatufikiri tena,hatina mda wa kuhoji wala hatutaki kujua tena ukweli ila kama uongo unahusu upande usiokugusa unashabikia,ukweli unaokugusa unageuka kuwa muongo.tumefika pabaya.Huu si ushabiki ni ujinga.

Mfano:mada ikihusu ufisadi wa viongozi ukisapoti wewe ni chadem!
Mada ikikosoa viongozi wa chadema ukisapoti hata kama ni kweli unaitwa ccm tena lumumba au buk7 !!
Mada ikimsifia dr slaa hata kama anastahili kwa hilo jambo wanataka utukane ili usiitwe Lumumba au ccm.

mada ikiwa inamsifia jk unatakiwa uponde sana kuepuka kuitwa chadem!

Ndugu zangu watanzania huu ni ushabiki au ni UJINGA!

Tuzinduke.penye ukweli tuseme.ccm juuuuuu!
 
Thread thread.... na leo hupati posho
 
Wengine kwa majina yetu tu, tayari tunalazimishwa sisi ni CHADEMA. Sijui zile kura wanazopataga kule KASKAZINI ni za MARUHANI??
 
Nimekuwa fb na jf sasa naona uwezo wa watanzania umefika ukomo japo si wote.ukiangalia mijadala mingi haijibiwi kwa hoja ila kwa ushabiki na uchama.hatufikiri tena,hatina mda wa kuhoji wala hatutaki kujua tena ukweli ila kama uongo unahusu upande usiokugusa unashabikia,ukweli unaokugusa unageuka kuwa muongo.tumefika pabaya.Huu si ushabiki ni ujinga.

Mfano:mada ikihusu ufisadi wa viongozi ukisapoti wewe ni chadem!
Mada ikikosoa viongozi wa chadema ukisapoti hata kama ni kweli unaitwa ccm tena lumumba au buk7 !!
Mada ikimsifia dr slaa hata kama anastahili kwa hilo jambo wanataka utukane ili usiitwe Lumumba au ccm.

mada ikiwa inamsifia jk unatakiwa uponde sana kuepuka kuitwa chadem!

Ndugu zangu watanzania huu ni ushabiki au ni UJINGA!

Tuzinduke.penye ukweli tuseme.ccm juuuuuu!

Mkuu,

Tunahitaji kufanya utafiti rasmi, nimekuwa na wasiwasi sana nikisoma michango ya walio wengi kwenye mitandao.
Yawezekana wajinga pamoja na wapumbavu wanazidi 90%. Hii ni hatari kwa jamii.
Watu wanaweza hata kushabikia jambo linalowaletea mauti katika siku chache zinazofuata!
 
Nimekuwa fb na jf sasa naona uwezo wa watanzania umefika ukomo japo si wote.ukiangalia mijadala mingi haijibiwi kwa hoja ila kwa ushabiki na uchama.hatufikiri tena,hatina mda wa kuhoji wala hatutaki kujua tena ukweli ila kama uongo unahusu upande usiokugusa unashabikia,ukweli unaokugusa unageuka kuwa muongo.tumefika pabaya.Huu si ushabiki ni ujinga.

Mfano:mada ikihusu ufisadi wa viongozi ukisapoti wewe ni chadem!
Mada ikikosoa viongozi wa chadema ukisapoti hata kama ni kweli unaitwa ccm tena lumumba au buk7 !!
Mada ikimsifia dr slaa hata kama anastahili kwa hilo jambo wanataka utukane ili usiitwe Lumumba au ccm.

mada ikiwa inamsifia jk unatakiwa uponde sana kuepuka kuitwa chadem!

Ndugu zangu watanzania huu ni ushabiki au ni UJINGA!

Tuzinduke.penye ukweli tuseme.ccm juuuuuu!

Swagazetu, nimefarijika sana kuona kwamba si mimi peke yangu ambaye nimekuwa nikusumbuliwa sana na anguko hili, janga la kitaifa, kiasi kwamba ninaanza kuogopa hata kufungua na kusoma sledi za JF-siasa. Hapana shaka ni asilimia ndogo sana ya Wabongo tunaotumia mitandao, lakini pia hili ndio kundi linalowakilisha wale wanaotegemewa kuwa na fikira pevu, kuangalia mambo objectively , na hatimaye kuwa 'viongozi' (hawa ni wasomi). Inatisha sana na ni anguko jipya la jamii yetu. Unaona mtu mwenye akili ya kuingia FB na JF anatetea ufisadi, anatetea siasa za kuabudu binadamu badala ya kushikilia sera, anatetea fikira mgando za 'wapigwe tu', 'uvumilivu una kikomo', 'watoto wa shule wanapata mimba kwa sababu ya kiherehere chao' (mzazi mwenye mtoto wa aina hiyo unafikiri atakuonaje?), wanatetea the great 'bongoland' kubadilika na kuwa 'posholand'. nk
 
Naungana nawe katika hili. w
Wachangiaji wengi wameweka utaifa pembeni.
Mioyo yao imejawa na chuki za ukabila, ukanda, uvyama, udini.
Sasa hivi wengi kazi yao ni kuharibu mada tena zenye nia njema.

Hebu angalia hii mada baada ya kupostiwa tayari kuna watu wameingiza majina ya vyama vyao.
Kuna tatizo kubwa sana ktk kufikiri, nadhani uwezo wa kufikiri wa wachangiaji walio wengi umeanza kushuka ndiyo maana matusi hayawaishii ktk post zao nyingi
 
Tusilaumu sana kwani haya ndio matokeo ya BRN. Elimu ya vijana wengi ndio hiyo ya kudandia mada bila kuisoma na kuitafakari vizuri. Tutake tusitake lazima kutokee mageuzi katika elimu ya nchi hii kama tunataka tuwe na jamii iliyoenda shule. Hata kwenye usaili msailiwa anaomba kiswahili kitumike wakati kazi anayoomba inamhitaji ajue kiingereza kwa ufasaha! Nathubutu kusema miaka hamsini baada ya uhuru elimu yetu imeshuka sana.
 
Ujinga wa jukwaa hili unasababishwa na mods wenyewe;Nitatoa sababu; kwanza hawa mods wanafurahia matusi yanayotolewa humu,kwa sababu mtu ametoa mada nzuri,tunapoanza kuchangia,tunapaswa tusitoke nje ya mada,lakini hawa jamaa wanakaa kimya,mtu anatumia lugha chafu jamaa wanaacha tu.Inatakiwa hata mtu anapopinga anapaswa kupinga kwa hoja,lakini hapa jf ni ziro kabisa.Mpaka sas nafikiri waanzilishi hili jukwaa ndivyo walivyoamua liwe jukwaa la wahuni na si Great thinker kama wanavyojiita.Wenye akili zao muwasikilize WAPO RADIO kwenye meza ya BUSARA kuanzia saa nne,watu wanapingana kwa hoja ama wanachangia mada kwa ueledi wa hali ya juu kabisa kushinda hapa jf.Kilichobakia hapa jf ni upuuzi mtupu hata kama kuna mada ya maana kiasi gani!!
 
Tusilaumu sana kwani haya ndio matokeo ya BRN. Elimu ya vijana wengi ndio hiyo ya kudandia mada bila kuisoma na kuitafakari vizuri. Tutake tusitake lazima kutokee mageuzi katika elimu ya nchi hii kama tunataka tuwe na jamii iliyoenda shule. Hata kwenye usaili msailiwa anaomba kiswahili kitumike wakati kazi anayoomba inamhitaji ajue kiingereza kwa ufasaha! Nathubutu kusema miaka hamsini baada ya uhuru elimu yetu imeshuka sana.

Una maanisha nini?
Elimu ipi ni bora kwako? "colonial education?" Muda mfupi baada ya Tanganyika kupata uhuru wake Elimu yetu (watanganyika)ilikuwaje?
Una maanisha hawa wasomi waliopo leo ni mburula tu?
Tumekuwa mashabiki hatufikirii tena.
 
Mkuu,

Tunahitaji kufanya utafiti rasmi, nimekuwa na wasiwasi sana nikisoma michango ya walio wengi kwenye mitandao.
Yawezekana wajinga pamoja na wapumbavu wanazidi 90%. Hii ni hatari kwa jamii.
Watu wanaweza hata kushabikia jambo linalowaletea mauti katika siku chache zinazofuata!

sina uhakika wa asilimia!!ila ukweli inakera kusapoti upumbavu hata kwa jambo la wazi,inashangaza watu wameamua kujitoa akili kwa ushabiki wa vyama,vichwa vimebaki Kama makopo wa Chooni!
 
Nashukuru hata kwenye thread hii akili za makopo hazijatokea kwa wingi vinginevyo wangekuja na kuvurumusha matusi kwa mleta hoja, mimi siku moja niliwahi kusema hili jukwa liitwe "jukwaa la ushabiki na viloja" ili liendane na vitu wanavyopost watu nikaonekana mimi ndo kioja!
 
Nashukuru hata kwenye thread hii akili za makopo hazijatokea kwa wingi vinginevyo wangekuja na kuvurumusha matusi kwa mleta hoja, mimi siku moja niliwahi kusema hili jukwa liitwe "jukwaa la ushabiki na viloja" ili liendane na vitu wanavyopost watu nikaonekana mimi ndo kioja!



Ni kweli kabisa mkuu leo umenena ukweli mtupu.Tunabahati mbaya saana hili taifa kuwa na vijana wengi kuwa na elimu feki lakini pia maskini, ona aibu hii kubwa kwa vijana madawa kulevya , hii ni ishara mbaya kwa taifa linalotegemewa kuja kukuza uchumi wake kupitia viwanda kama vijana wenyewe ndo hao hawajui hata kujenga hoja, kudadisi ns kuhoji. Mbele naiona hatari kubwa rafiki.Mi nishauri jukwaa hili watu wawekewe masharti magumu zaidi mtu akipost kitu kishabiki afutiliwe mbali na mada yake huko.
 
Mkuu,

Tunahitaji kufanya utafiti rasmi, nimekuwa na wasiwasi sana nikisoma michango ya walio wengi kwenye mitandao.
Yawezekana wajinga pamoja na wapumbavu wanazidi 90%. Hii ni hatari kwa jamii.
Watu wanaweza hata kushabikia jambo linalowaletea mauti katika siku chache zinazofuata!
na hao wapumbavu ndio mtaji wa wanasiasa wetu
 
Hii yote inaletwa na wachangiaji walioajiriwa na wanasiasa kutukana na wengine kununuliwa simu au kwa lugha ya wenyewe kujibu mapigo. Hawa kwa kuwa ajira zao zinatokana na ukali wa matusi basi wanalazimika kutumia kiungo tofauti na kichwa ili ajira iendelee na wapate na bonas. Tunakoelekea vichaa watakuwa wengi.
 
Back
Top Bottom