Tumekuwa washabiki,hatufikiri tena

Tumekuwa washabiki,hatufikiri tena

Una maanisha nini?
Elimu ipi ni bora kwako? "colonial education?" Muda mfupi baada ya Tanganyika kupata uhuru wake Elimu yetu (watanganyika)ilikuwaje?
Una maanisha hawa wasomi waliopo leo ni mburula tu?
Tumekuwa mashabiki hatufikirii tena.

Ni bora Elimu ya Kikoloni watanganyika walifikiri kwa kutumia akili zao kuliko elimu ya sasa tunafikiria kwa kutumia makalio yetu.Hatuna uzalendo tena.Utaifa ulishafariki na tuliuzika makaburi ya Kinondoni siku nyingi.Watanzania tunafurahia kundi fulani likinyanyaswa na watawala sababu tu watawala wale ni jama,marafiki,baba,mama au ndugu wakaribu.

Tumekuwa na akili ambazo watoto au wajukuu zetu watafukua makaburi yetu kuona kama vichwa vyetu vilikuwa na ubongo au maji.

JF enzi hizo lilikuwa jukwaa ambalo unatamani kila siku usome ajenda zake na hoja zitolewazo na members wake,lakini leo ni matusi ya ajabu,mipasho isiyo na maana,udini,uvyama,ukabila ndivyo vilivyojazana.Kwa ukweli JF imeshuka thamani inabidi MODS wajiangalie upya wapi wameanguka na sababu gani ili walirudishe jukwaa lile la enzi zile.
 
Mi nafikiri la mwisho ndo ulitaka kuandika ile usionekane buku 7, nyingine mbwembwe tu, ipo juu kwa lipi?
 
Ni kweli kabisa mkuu.Siku zote ushabiki na ukereketwa ukizidi,uwezo wa kufikiri unakimbia mara moja kwani hivi viwili haviwezi kukaa zizi moja.Chukulia kwa mfano suala la ufisadi na makada wa sisiemu, hili litolewa kama mada,matusi yanakuwa mengi hasa kutoka kwa mashabiki wa chama tawala wanasahau kabisa namna ufisadi unavyowatesa watanzania wengi.halafu tatizo lingine kubwa kwa watanzania ni uvivu wa kujisomea ili kufahamu issue mbalimbali na hivyo kuwa na weledi wa kuchangia mambo mbalimbali kwa hoja ambazo ni kuntu.
 
Ni kweli kabisa mkuu ushabiki unatumaliza.Chukulia mfano wa Zitto na posho za kbunge la katiba.Kijana amesema kwamba posho hizi hatazichukua.Msimamo wake huu unakosolewa na baadhi ya wafuasi wa Chadema na kumuita mnafiki!Pamoja na tofauti zao na Zitto walitakiwa kumuunga mkono juu ya suala hili kwani athari ya hili ni kwa watanzania wote bila kuangalia chama.Ufisadi unaliangamiza taifa letu, wake up comrades!
 
Maneno yako yanadhihirisha mapenzi mema kwa wana jf.

Nakubaliana nawe ili tuwe great thinkers ni lazima kuuepuka ushabiki.
 
Nimekuwa fb na jf sasa naona uwezo wa watanzania umefika ukomo japo si wote.ukiangalia mijadala mingi haijibiwi kwa hoja ila kwa ushabiki na uchama.hatufikiri tena,hatina mda wa kuhoji wala hatutaki kujua tena ukweli ila kama uongo unahusu upande usiokugusa unashabikia,ukweli unaokugusa unageuka kuwa muongo.tumefika pabaya.Huu si ushabiki ni ujinga.

Mfano:mada ikihusu ufisadi wa viongozi ukisapoti wewe ni chadem!
Mada ikikosoa viongozi wa chadema ukisapoti hata kama ni kweli unaitwa ccm tena lumumba au buk7 !!
Mada ikimsifia dr slaa hata kama anastahili kwa hilo jambo wanataka utukane ili usiitwe Lumumba au ccm.

mada ikiwa inamsifia jk unatakiwa uponde sana kuepuka kuitwa chadem!

Ndugu zangu watanzania huu ni ushabiki au ni UJINGA!

Tuzinduke.penye ukweli tuseme.ccm juuuuuu!

Hapo mwisho kwenye bold,umeonyesha ushabiki wa kijinga pia
 
Back
Top Bottom