Ndugu wana Jamii, niliwahi kuleta thread hapa jukwaani yenye title mapenzi ni shida!!!!! Nilielezea yaliyojiri kati yangu na binti mmoja ambaye nilitokea kumpenda sana, ukiweza tafuta huo uzi upo humu kwa reference zaidi.
Niliendelea kuwa nae kwa kujivuta vuta hivyo hivyo, ingawa moyoni alishaanza kunitoka kidogo kidogo. Ukweli ni kwamba nilanza kutafuta mtu mwingine kimyakimya sababu nilijuwa wazi huyu wa sasa sina mpango nae ingawa kumuacha ilikuwa mtihani kwa kiasi kwani nilikuwa tayari kwenye mapenzi yenye kerooooo Mmnoooooo!!!!!.
Last week ilikuwa siku ya alhamisi nilitoka dinner na huyu binti (wa zamani) kwa lengo la kutaka kumuelezea maamuzi yangu ya kumaliza mahusiano nae, tukakaa sehemu kwa kinywaji na msosi lakini nilishindwa kumuulezea kwa sababu alikuwa yuko very romantic kuliko maelezo, wakati huo kesho yake nilikuwa tayari na ahadi na bi dada mpya nikitegemea ningemaliza ile game alhamis na Ijumaaa ningekuwa huru na mtu mpya, kwa kweli kwa ile alhamis nilishindwa, mwisho wa yote alhmisi tukaondoka tukiwa sawa maana sikuweza timiza lengo langu,hivyo nikamuomba tukutane kesho yake Ijumaa kwa muda mfupi, lengo ikiwa ni kumpa taarifa ya kuwa mimi na yeye mwisho wetu ni pale. Basi Ijumaa kweli tukakutana kwa dk 45 akiwa katika moody nzuri kabisa lakini nikasema iwe jua iwe mvua leo ndiyo MWISHO.
Tulikuwa katika mazungumzo ya kawaida ndipo mimi nilipomtamkia kuwa baada ya kukaa nae kwa muda wote tulikuwa pamoja ningependa kumuueleza kuwa MIMI KUANZIA SIKU ILE YA IJUMAAA NDIYO MWISHO WA YEYE NA MIMI NA NISINGEPENDA MAWASILIANO WALA KUTAFUTANA MAANA TAYARI NIMESHAPATA BABY MWINGINE. Wakati natoa taarifa hiyo mdada mpya akapiga simu kunielezea kuwa ameshafika eneo husika ili tuendelee na appointment yetu. Binti alipigwa na butwaaaa na hakuamini akabaki anashangaaaaaaaa na kulalamika kuwa AMEUMIA MNOOOOOOOOOOOO na hata weza lala kwa sababu hakutegemea.
Haya wa ndugu tusipende kushindana na hawa viumbe ila dawa ya mwanamke huwa ni mwanamke mwenzake. Nakaribisha maoni yenu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!