PostGE2025 Tume ya Samia: Yumo Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya, mdogo wake Asha-Rose Mtengeti Migiro (Katibu Mkuu wa CCM)

PostGE2025 Tume ya Samia: Yumo Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya, mdogo wake Asha-Rose Mtengeti Migiro (Katibu Mkuu wa CCM)

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Ex Spy

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2007
Posts
313
Reaction score
2,649
Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni mdogo wa tumbo moja (ndugu wa damu) wa Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa CCM – Mtendaji Mkuu wa shughuli za chama.

Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni sehemu ya wajumbe saba wa kinachoitwa “Tume Huru ya kufanya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani”. Tume iliyoundwa na kutangazwa jana.

Pia Soma: Rais Samia aunda Tume ya Uchunguzi wa matukio ya Uvunjifu wa Amani wakati na baada ya Uchaguzi 2025

IMG_9527.jpeg


Kwa kuzingatia muundo huo wa tume hiyo, ni wazi tume yenyewe kwa ujumla, imepoteza uhalali achilia mbali weledi katika kuitwa chombo cha uchunguzi – kabla ya kuanza kazi.

Kwanini? CCM ndiyo chama ambacho mdogo wake wa tumbo moja, Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ni Katibu Mkuu (Secretary General). Je, anaweza kuwa kuwa huru kutimiza wajibu wake?

Wananchi wanataka uchunguzi wa mauaji ya kutisha ya raia. Wananchi wanataka kufahamu watu wangapi wameuwawa, wangapi wamezikwa, wangapi maiti zao hazionekani na wangapi wamejeruhiwa.

Kwa kuwa waliounda hiyo tume wametueleza kwamba wameunda tume kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa matukio ya ‘uvunjifu wa amani’, ni wazi tume hiyo haituhusu wananchi.
 
Tume ya Kikwete, muda umesonga sana lakini akina Kikwete wanaendelea na mbinu zilezile za miaka 20 iliyopita.
 
Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni mdogo wa tumbo moja (ndugu wa damu) wa Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa CCM – Mtendaji Mkuu wa shughuli za chama.

Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni sehemu ya wajumbe saba wa kinachoitwa “Tume Huru ya kufanya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani”. Tume iliyoundwa na kutangazwa jana.

View attachment 3504535

Kwa kuzingatia muundo huo wa tume hiyo, ni wazi tume yenyewe kwa ujumla, imepoteza uhalali achilia mbali weledi katika kuitwa chombo cha uchunguzi – kabla ya kuanza kazi.

Kwanini? CCM ndiyo chama ambacho mdogo wake wa tumbo moja, Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ni Katibu Mkuu (Secretary General). Je, anaweza kuwa kuwa huru kutimiza wajibu wake?

Wananchi wanataka uchunguzi wa mauaji ya kutisha ya raia. Wananchi wanataka kufahamu watu wangapi wameuwawa, wangapi wamezikwa, wangapi maiti zao hazionekani na wangapi wamejeruhiwa.

Kwa kuwa waliounda hiyo tume wametueleza kwamba wameunda tume kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa matukio ya ‘uvunjifu wa amani’, ni wazi tume hiyo haituhusu wananchi.
Sefue Ombeni buddy wa kikwe
 
Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni mdogo wa tumbo moja (ndugu wa damu) wa Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa CCM – Mtendaji Mkuu wa shughuli za chama.

Balozi Radhia Naima Mtengeti Msuya ni sehemu ya wajumbe saba wa kinachoitwa “Tume Huru ya kufanya uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani”. Tume iliyoundwa na kutangazwa jana.

View attachment 3504535

Kwa kuzingatia muundo huo wa tume hiyo, ni wazi tume yenyewe kwa ujumla, imepoteza uhalali achilia mbali weledi katika kuitwa chombo cha uchunguzi – kabla ya kuanza kazi.

Kwanini? CCM ndiyo chama ambacho mdogo wake wa tumbo moja, Dkt. Asha-Rose Mtengeti Migiro ni Katibu Mkuu (Secretary General). Je, anaweza kuwa kuwa huru kutimiza wajibu wake?

Wananchi wanataka uchunguzi wa mauaji ya kutisha ya raia. Wananchi wanataka kufahamu watu wangapi wameuwawa, wangapi wamezikwa, wangapi maiti zao hazionekani na wangapi wamejeruhiwa.

Kwa kuwa waliounda hiyo tume wametueleza kwamba wameunda tume kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa matukio ya ‘uvunjifu wa amani’, ni wazi tume hiyo haituhusu wananchi.
Hii inaitwa ufalmia aka ufalme.
 
Hivi, huyu madam president anashauriwa au anajishauri mwenyewe? Kama anashauriwa hapimi faida na hasara za ushauri? Kama anajishauri, basi anajiongoza sivyo!
Namsaidia kuunda tume huru na ya haki kwa kuwachagua baadhi ya viongozi wa dini watatu, jaji wa mahakama ya rufaa mstaafu, viongozi wawili kutoka vyama vikubwa vya siasa na mjumbe mmoja kutoka tls.
Wajumbe Hawa wasiwajibike kwake na taarifa ya uchunguzi itolewe kwa wananchi Moja kwa Moja ili kuepuka uchakachuaji.
 
Ameenda mbali zaidi akamteua aliyekuwa waziri wa ulinzi Tax wakati wa "vurugu".
Mpaka leo hatujui Risasi zilizotuliza "vurugu" zilipigwa na nani na kwa amri ya nani. Huyu Tax alitakiwa kuhojiwa, leo yeye ndio anaenda kuchunguza.

Hii ni tume ya utani
 
Back
Top Bottom