Tume Huru ya Uchaguzi: Kambi Rasmi ya Upinzani ilikuwa wapi muda wote kupeleka Muswada Binafsi bungeni kuhusu jambo hilo?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Kikatiba, kisheria na kikanuni Muswada binafsi unaruhusiwa kuwasilishwa Bungeni. Huu ni Muswada ambao huwasilishwa na Mbunge tofauti na ile miswada inayowasilishwa na Serikali ili kuwa sheria.

Muswada huweza kuwa katika kutunga sheria mpya au kurekebisha zilizopo. Hata Katiba hurekebishwa na sheria inayoanzia kwenye Mswada. Mswada pia huweza kurekebisha sheria mbalimbali kwa wakati mmoja.

Bungeni kuna Kambi Rasmi ya Upinzani inayoundwa na kuongozwa na CHADEMA. Ina Wabunge wa kutosha na wenye haki za kuwakilisha Miswada binafsi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa. Na wamechaguliwa tangu mwaka 2015.

Ni CHADEMA hao hao ndiyo wanaoshikilia hoja ya uwepo wa Tume Huru ya Uchaguzi hapa Tanzania. Hoja hii imeanikwa kama vipaumbele vya sasa vya Katibu Mkuu mpya wa chama hicho John J. Mnyika (Mb). Hoja hii inashikiwa bango mwaka huu; mwaka wa Uchaguzi Mkuu. Kwanini?

Walikuwa wapi tangu mwaka 2015 kujenga hoja hii na hata kuwasilisha Muswada binafsi Bungeni kuhusu suala hilo? Kwanini nafasi hiyo ya Muswada binafsi haikutumika hadi sasa kuitaka Serikali kuwasilisha Muswada huu ya suala hilo kwa Hati ya Dharura?
 
Mwanasheria gani wewe usieona juhudi wanazofanya wapinzani wa ccm ?! Juhudi hizi zinazimwa makusidi na kitu cha bunge kwa maelekezo ya serikali na chama chao.

Kama tu katiba mpya ya wananchi ilizimwa na haukushangaa, sembuse na hoja binafsi ya CDM !!. Serikali kupitia CCM hawajawa tayari kwa democracy, labda through vita wanaweza wakaelewa na kuheshimu wanachokitaka wananchi . Na hii ni nchi nyingi za Africa
 
Heloo VAR, am coming for youuu.

tapatalk_1577617034018.jpeg
tapatalk_1577617098170.jpeg



Chai tena ya baridi.

tapatalk_1581164603907.jpeg


Unforgetable
 
Wqpinzani hamna kitu mkuu!

Wao kikubwa ni bora kuwekeza nguvu kumpambania Kinana, Membe nq Makamba ili pengine linaweza kutokea zali la kupiga hela kama lile la 2015

Sent using Jamii Forums mobile app
Dili za hivo ni za mwenyekiti na makamu wake.
Hawa akina Blindspot wanasubili kukunja na kuzungusha ngumi tu, dili litakapokamilika.
 
Kikatiba, kisheria na kikanuni Muswada binafsi unaruhusiwa kuwasilishwa Bungeni. Huu ni Muswada ambao huwasilishwa na Mbunge tofauti na ile miswada inayowasilishwa na Serikali ili kuwa sheria.

Muswada huweza kuwa katika kutunga sheria mpya au kurekebisha zilizopo. Hata Katiba hurekebishwa na sheria inayoanzia kwenye Mswada. Mswada pia huweza kurekebisha sheria mbalimbali kwa wakati mmoja.

Bungeni kuna Kambi Rasmi ya Upinzani inayoundwa na kuongozwa na CHADEMA. Ina Wabunge wa kutosha na wenye hali za kuwakilisha Miswada binafsi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa. Na wamechaguliwa tangu mwaka 2015.

Ni CHADEMA hao hao ndiyo wanaoshikilia hoja ya uwepo wa Time Huru ya Uchaguzi hapa Tanzania. Hoja hii imeanikwa kama vipaumbele vya sasa vya Katibu Mkuu mpya wa chama hicho John J. Mnyika (Mb). Hoja hii inashikiwa bango mwaka huu-mwaka wa Uchaguzi Mkuu. Kwanini?

Walikuwa wapi tangu mwaka 2015 kujenga hoja hii na haya kuwasilisha Mswada binafsi Bungeni kuhusu suala hilo? Kwanini nafasi hiyo ya Mswada binafsi haikutumika hadi sasa kuitaka Serikali kuwasilisha Mswada huu ya suala hilo kwa Hati ya Dharura?
Kama ulikuwa unafuatilita kwenye majadiliano ya katibu mpya hili suala la tume huru lilikubalika lakini mwisho wa siku vyama vya upinzani kutokana na ubinafsi wao walisababisha mchakato wa katiba mpyausimame na leo wanalalamika.
Binafsi kwangu kwa kuanzia Tume huru na kukubalika kwa mgombea binafsi ilikuwa inatosha sana kwa kuanzia lakini wapi!!!
Tumerudi square back to square one.
 
Tatizo siyo wabunge wa CHADEMA. Tatizo kubwa ni Serikali yenu ambayo inaongozwa na viongozi ambao ni inept, incompetent, stupid and imperious. Viongozi wenu hawataki mambo ambayo ni chanya kwa taifa na kwa vizavi vya kesho.
Mfano mzuri ni suala la mapendekezo ya katiba mpya ambalo viongozi wenu ambao ni inept wamelikanyagia wazi wazi bila kujali faida ya katiba mpya. Hofu yao kubwa ni kwamba kwa katiba mpya wasingekuwa salama kwa matendo yao wanayoyafanya leo hii.

Keep fighting mambo yatakaa sawa. Ingawa jambo nzuri haliwezi kuja kwa maneno tu.
 
Kikatiba, kisheria na kikanuni Muswada binafsi unaruhusiwa kuwasilishwa Bungeni. Huu ni Muswada ambao huwasilishwa na Mbunge tofauti na ile miswada inayowasilishwa na Serikali ili kuwa sheria.

Muswada huweza kuwa katika kutunga sheria mpya au kurekebisha zilizopo. Hata Katiba hurekebishwa na sheria inayoanzia kwenye Mswada. Mswada pia huweza kurekebisha sheria mbalimbali kwa wakati mmoja.

Bungeni kuna Kambi Rasmi ya Upinzani inayoundwa na kuongozwa na CHADEMA. Ina Wabunge wa kutosha na wenye hali za kuwakilisha Miswada binafsi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa. Na wamechaguliwa tangu mwaka 2015.

Ni CHADEMA hao hao ndiyo wanaoshikilia hoja ya uwepo wa Time Huru ya Uchaguzi hapa Tanzania. Hoja hii imeanikwa kama vipaumbele vya sasa vya Katibu Mkuu mpya wa chama hicho John J. Mnyika (Mb). Hoja hii inashikiwa bango mwaka huu; mwaka wa Uchaguzi Mkuu. Kwanini?

Walikuwa wapi tangu mwaka 2015 kujenga hoja hii na haya kuwasilisha Muswada binafsi Bungeni kuhusu suala hilo? Kwanini nafasi hiyo ya Muswada binafsi haikutumika hadi sasa kuitaka Serikali kuwasilisha Muswada huu ya suala hilo kwa Hati ya Dharura?
Mpaka sasa sioni upinzani wa kweli. Wengi wanatetea maslahi binafsi, huo ndio ukweli. Nilitarajia awamu hii kungekuwa na mapambano ya dhati kabisa kutaka KATIBA MPYA, badala yake wapinzani wanaodhaniwa kuwa wapinzani wakaendekeza viajenda vyao vyepesi tu. Ni kama kikundi cha watu wasio na dira, ila ukiwaambia ukweli wanakuona huwapendi.

Sent from my SM-T355Y using Tapatalk
 
Back
Top Bottom