sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
I am not bound to win, but I am bound to be true. I am not bound to succeed, but I am bound to live by the light that I have. I must stand with anybody that stands right, and stand with him while he is right, and part with him when he goes wrong.
By: Abraham Lincoln
Falsafa inayoishi ya aliyekuwa Rais wa Marekani Abraham Lincoln " sina mipaka ya kushinda, lakini nina mipaka ya kuwa mkweli, Sina mipaka ya kufanikiwa, lakini nina mipaka ya maisha ya nuru niliyo nayo, ni lazima nisimame na yeyote atakaye simamia haki na nitasimama naye akiwa sawa, isipokuwa atakapokuwa kinyume.
Yanayotokea awamu hii ni kinyume na matarajio ya Watanzania wanaoitwa wanyonge. Kwa kuwa unyonge wao ni faida kwa wajanja wachache.
Ndiyo maana uhalisia wa unyonge wao, wana nyongwa kwa kukamuliwa kodi zinazofanywa neema kwa wateule wachache, wapiga deal.
Niliwahi kusema kuwa wasomi wanamuangusha Rais, kwa kuwa wamesoma madhaifu ya Rais, imekuwa rahisi kuwa kwao kucheza na saikolojia yake.
Utashi wa Rais wetu ni sifa na mapambio, huo kwake ni ulemavu. Kwa kulijua hilo watendaji wake wameamua kucheza na akili yake kwa kumsifia kwa nyimbo na ngonjera, wakati huo huo wakitafuna keki ya taifa watakavyo.
Mbali na hayo, niliwahi kutahadhalisha kuwa huenda ufisadi katika fedha za umma ni mkubwa kuliko awamu zote za serikali zinazo ongozwa na CCM, watu walibisha na wengine kutukana.
Sasa yaliyojiri leo yanathibitisha uhalisia wa maandiko yangu mengi.
Toka kuingia kwa serikali hii madarakani, serikali imeikuwa mkanyagaji mkubwa wa katiba na mvunjaji mkubwa wa sheria za nchi.
Pamoja na kuapa kuilinda katiba, watendaji wote wa serikali wakiongozwa na Rais wamekuwa ndiyo wavunjaji wakubwa wa sheria, lakini pia wapotoshaji wakubwa wakidhani Watanzania wa leo ni wajinga!
Ikitokea mkadhani sisi wajinga mtakuwa mnakosea, japo Rais alikwisha watahadharisha kuwa sisi si wajinga, na kama wajinga basi ni wale wafukuza upepo wa CCM wanaofikiri kuwa kukosoa ni kukosa uzalendo.
Huwezi kuwalaumu moja kwa moja wasomi hawa waliogeuka kuwa majizi bila kuangalia udhaifu umeanzia wapi!
Maamuzi ya hovyo ambayo yamekuwa utamaduni kwa serikali hii ni maamuzi binafsi yanayokiuka sheria na mwongozo wa nchi, kwa maana ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Rais amekuwa akiibua miradi mikubwa inayogharimu fedha nyingi za umma bila idhini ya wananchi kwa maana ya bunge la Jamhuri ya Muungano.
Hali inayoondoa usafi wa matumizi ya umma, inayochukuliwa kama easy going.
Mathalani unakuwa na company, lakini kwa kuwa wewe ni mkurugenzi unaamua kuchota fedha za company bila kufuata utaratibu wa uendeshaji company hiyo, huo ni ubadhirifu unaotoa mianya kwa watendaji wako kuchota kwa staili yako uliyoianzisha, na mwisho wa siku company inaingia madeni makubwa yasiyo na tija then unamtafuta mwizi wakati wewe mwenyewe si msafi katika matumizi ya fedha za company.
Kwa mujibu wa sheria ya bajeti, manunuzi ya umma yatapitia na kuidhinishwa na bunge, ndipo serikali itafanya utekelezaji wa bajeti waliyo ileta yenye baraka za bunge letu, nao watafuata sheria ya manunuzi kwa kutangaza tender bid au kwa mfumo wa cortation, kwa kuzingatia sheria na viwango vya manunuzi.
Tumeona serikali ikiidhinisha billions of shilling kwa ujenzi wa uwanja wa Chato bila idhini ya bunge, tumeona manunuzi ya ndege zaidi ya 10 ambayo bunge pia haikuidhinisha.
Tumeona mikataba ya madini ya kimya kimya, wakati kuna kamati ya bunge ya nishati na madini na bunge likipata taarifa kupitia vyombo vya habari.
Kwa mantiki hii, kwa saga la Kangi ni muendelezo wa matendo ya kiongozi mkuu kwa anayoyafanya, ndio maana hoja ya Mh. Zitto Zuberi Kabwe inapata mashiko, kuwa kwa kuwa mchongo hakuanzia kwa Rais asiyefuata sheria ya bajeti kwa maslahi binafsi ndiyo maana deal la Lugola na wenzake limemkera Mkuu.
Kama alivyosema Rais Watanzania si wajinga nami nasema mtoto umleleavyo ndivyo akuavyo.
Tumeacha misingi ya sheria, tunaendesha nchi kwa mazoea, na kwa kuwa tuna dola iliyo kosa weredi, tumeruhusu kushughulikiwa ili kulinda maslahi binafsi ya wachache.
Yote haya yanasababishwa na mfumo mbovu unaolindwa na katiba isiyo na meno, inayotoa mwanya kwa wakosoaji kushughulikiwa na vyombo vya dola.
Kwa kulitambua hilo na kwa udhaifu wa katiba yetu hakuna aliye salama ndani ya CCM, kwa kuwa mfumo uliopo unamtengenezea hata malaika mianya ya kuwa fisadi.
Kwa kudhihirisha hilo tumbua tumbua ya Rais Magufuli haiwezi kuiacha CCM salama ikiwa tutafuata misingi ya utawala bora.
Ndiyo maana falsafa ya Abraham Lincoln inapokuwa na nguvu. Inatoa mwelekeo wa nchi yetu wapi yatupasa kwenda na kwa mfumo upi.
Ndani ya CCM hakuna msafi, wote wamechafuka, takribani kila wizara ina uchafu kwa staili hii ya chukua chako mapema CCM inapoteza legitimacy ya kuwaongoza Watanzania, kwa kuwa mfumo wa chama chao umeruhusu kuwanyonya Watanzania.
Ni wakati sasa wa kuamua wapi tunaipeleka nchi na nini mustakabali wa rasilimali zetu.
Hatuwezi kuendesha nchi kama gari lisilo na brake, ni lazima tujiulize nini hatima ya ufisadi unao fanyika kwa kukata mzizi na asili ya ufisadi wenyewe, vinginevyo tumbua tumbua ya Rais Magufuli haitakuwa na faida kwa nchi zaidi ya tafsiri ya kuzungukana kwenye deals.
By: Abraham Lincoln
Falsafa inayoishi ya aliyekuwa Rais wa Marekani Abraham Lincoln " sina mipaka ya kushinda, lakini nina mipaka ya kuwa mkweli, Sina mipaka ya kufanikiwa, lakini nina mipaka ya maisha ya nuru niliyo nayo, ni lazima nisimame na yeyote atakaye simamia haki na nitasimama naye akiwa sawa, isipokuwa atakapokuwa kinyume.
Yanayotokea awamu hii ni kinyume na matarajio ya Watanzania wanaoitwa wanyonge. Kwa kuwa unyonge wao ni faida kwa wajanja wachache.
Ndiyo maana uhalisia wa unyonge wao, wana nyongwa kwa kukamuliwa kodi zinazofanywa neema kwa wateule wachache, wapiga deal.
Niliwahi kusema kuwa wasomi wanamuangusha Rais, kwa kuwa wamesoma madhaifu ya Rais, imekuwa rahisi kuwa kwao kucheza na saikolojia yake.
Utashi wa Rais wetu ni sifa na mapambio, huo kwake ni ulemavu. Kwa kulijua hilo watendaji wake wameamua kucheza na akili yake kwa kumsifia kwa nyimbo na ngonjera, wakati huo huo wakitafuna keki ya taifa watakavyo.
Mbali na hayo, niliwahi kutahadhalisha kuwa huenda ufisadi katika fedha za umma ni mkubwa kuliko awamu zote za serikali zinazo ongozwa na CCM, watu walibisha na wengine kutukana.
Sasa yaliyojiri leo yanathibitisha uhalisia wa maandiko yangu mengi.
Toka kuingia kwa serikali hii madarakani, serikali imeikuwa mkanyagaji mkubwa wa katiba na mvunjaji mkubwa wa sheria za nchi.
Pamoja na kuapa kuilinda katiba, watendaji wote wa serikali wakiongozwa na Rais wamekuwa ndiyo wavunjaji wakubwa wa sheria, lakini pia wapotoshaji wakubwa wakidhani Watanzania wa leo ni wajinga!
Ikitokea mkadhani sisi wajinga mtakuwa mnakosea, japo Rais alikwisha watahadharisha kuwa sisi si wajinga, na kama wajinga basi ni wale wafukuza upepo wa CCM wanaofikiri kuwa kukosoa ni kukosa uzalendo.
Huwezi kuwalaumu moja kwa moja wasomi hawa waliogeuka kuwa majizi bila kuangalia udhaifu umeanzia wapi!
Maamuzi ya hovyo ambayo yamekuwa utamaduni kwa serikali hii ni maamuzi binafsi yanayokiuka sheria na mwongozo wa nchi, kwa maana ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Rais amekuwa akiibua miradi mikubwa inayogharimu fedha nyingi za umma bila idhini ya wananchi kwa maana ya bunge la Jamhuri ya Muungano.
Hali inayoondoa usafi wa matumizi ya umma, inayochukuliwa kama easy going.
Mathalani unakuwa na company, lakini kwa kuwa wewe ni mkurugenzi unaamua kuchota fedha za company bila kufuata utaratibu wa uendeshaji company hiyo, huo ni ubadhirifu unaotoa mianya kwa watendaji wako kuchota kwa staili yako uliyoianzisha, na mwisho wa siku company inaingia madeni makubwa yasiyo na tija then unamtafuta mwizi wakati wewe mwenyewe si msafi katika matumizi ya fedha za company.
Kwa mujibu wa sheria ya bajeti, manunuzi ya umma yatapitia na kuidhinishwa na bunge, ndipo serikali itafanya utekelezaji wa bajeti waliyo ileta yenye baraka za bunge letu, nao watafuata sheria ya manunuzi kwa kutangaza tender bid au kwa mfumo wa cortation, kwa kuzingatia sheria na viwango vya manunuzi.
Tumeona serikali ikiidhinisha billions of shilling kwa ujenzi wa uwanja wa Chato bila idhini ya bunge, tumeona manunuzi ya ndege zaidi ya 10 ambayo bunge pia haikuidhinisha.
Tumeona mikataba ya madini ya kimya kimya, wakati kuna kamati ya bunge ya nishati na madini na bunge likipata taarifa kupitia vyombo vya habari.
Kwa mantiki hii, kwa saga la Kangi ni muendelezo wa matendo ya kiongozi mkuu kwa anayoyafanya, ndio maana hoja ya Mh. Zitto Zuberi Kabwe inapata mashiko, kuwa kwa kuwa mchongo hakuanzia kwa Rais asiyefuata sheria ya bajeti kwa maslahi binafsi ndiyo maana deal la Lugola na wenzake limemkera Mkuu.
Kama alivyosema Rais Watanzania si wajinga nami nasema mtoto umleleavyo ndivyo akuavyo.
Tumeacha misingi ya sheria, tunaendesha nchi kwa mazoea, na kwa kuwa tuna dola iliyo kosa weredi, tumeruhusu kushughulikiwa ili kulinda maslahi binafsi ya wachache.
Yote haya yanasababishwa na mfumo mbovu unaolindwa na katiba isiyo na meno, inayotoa mwanya kwa wakosoaji kushughulikiwa na vyombo vya dola.
Kwa kulitambua hilo na kwa udhaifu wa katiba yetu hakuna aliye salama ndani ya CCM, kwa kuwa mfumo uliopo unamtengenezea hata malaika mianya ya kuwa fisadi.
Kwa kudhihirisha hilo tumbua tumbua ya Rais Magufuli haiwezi kuiacha CCM salama ikiwa tutafuata misingi ya utawala bora.
Ndiyo maana falsafa ya Abraham Lincoln inapokuwa na nguvu. Inatoa mwelekeo wa nchi yetu wapi yatupasa kwenda na kwa mfumo upi.
Ndani ya CCM hakuna msafi, wote wamechafuka, takribani kila wizara ina uchafu kwa staili hii ya chukua chako mapema CCM inapoteza legitimacy ya kuwaongoza Watanzania, kwa kuwa mfumo wa chama chao umeruhusu kuwanyonya Watanzania.
Ni wakati sasa wa kuamua wapi tunaipeleka nchi na nini mustakabali wa rasilimali zetu.
Hatuwezi kuendesha nchi kama gari lisilo na brake, ni lazima tujiulize nini hatima ya ufisadi unao fanyika kwa kukata mzizi na asili ya ufisadi wenyewe, vinginevyo tumbua tumbua ya Rais Magufuli haitakuwa na faida kwa nchi zaidi ya tafsiri ya kuzungukana kwenye deals.