Tumbo kuunguruma, nini tatizo

Tumbo kuunguruma, nini tatizo

GESI TUMBONI (COLIC):

Ikiwa mtu atakula kwa wingi vyakula vinavyoleta
gesi halafu vyakula hivyo visisagike vizuri

tumboni, hukusanya gesi tumboni na kufanya
mingurumo humo na kumsababishia maumivu,
humkosesha mtu utulivu na kumfanya kutoka

jasho na machovu bila ya kufanya kazi.
Mtu hujisikia mara kwa mara aende haja kubwa na
akienda hapati choo. Pia humsababishia mtu

kuumwa kwa mgongo au kiuno.
Ikiwa gesi hii itakosa kutoka kwa njia ya haja
kubwa, basi yaweza kupanda juu na kufanya
presha sehemu au karibu ya moyo na kusababisha
maumivu ya moyo.

TIBA:

Chukua Asali safi mbichi iwe ya Asali ya nyuki robo lita , unga wa arki susi vijiko
vitatu vikubwa na unga wa habat soda vijiko viwili

vikubwa. Koroga zote pamoja kwa kijiko. Chukua
vijiko viwili vya mchanganyiko huu ukoroge ndani

ya kikombe cha maji ya moto halafu yakishapoa
unywe kikombe kimoja kutwa mara mbili asubuhi

na jioni.
 
umekunywa maji ya moshi ambayo tumezoea kukinga tu kwenye bomba na kuendelea,pia pale moshi zile mboga mboga zinazouzwa mjini pale wanatumia ngao (dawa ya kupuliza mbu) ktk kukuzia mboga2 mashambani.acha kabisa kula ovyo

kwa sasa wewe unasumbuliwa na gesi nyingi sana tumboni.

CHA KUFANYA............nenda kapime choo ktk hospitali zinazoeleweka, usitumie dawa za gesi,kwani gesi ni matokeo ya constipation

..................................nenda pale mombasa stoo mjini moshi karibu na NMB mandela.au watafute wamasai

huna tatizo la nguvu za kiume kama huyo kiungo cha kujisaidia alivo comment hapo juu...nin hiyo gesi tu labda yeye ndio chakula/shoga.

Sawa professa,jifunze kuheshimu koment za watu.
 
Mkuu kunywa viroba, kimoja kutwa mara tatu kwa siku tatu. Dalili zikiendelea mone daktari
 
Mzizimkavu hizo dawa zinapatikana ktk maduka ya kawaida ya madawa na je hiyo asali ni nyuki wadogo au wakubwa? Na asiyetumia asali afenyeje?
ndio hizo dawa zinapatikana kwenye maduka ya Dawa hapo Kariakoo Asali upate yenye nyuki Wakubwa sio wadogo tena hiyo asali upate mbichi safi isiyochanganywa na sukari mkuu. Kwani wewe asali ukila inakudhuru?
 
GESI TUMBONI (COLIC):

Ikiwa mtu atakula kwa wingi vyakula vinavyoleta
gesi halafu vyakula hivyo visisagike vizuri

tumboni, hukusanya gesi tumboni na kufanya
mingurumo humo na kumsababishia maumivu,
humkosesha mtu utulivu na kumfanya kutoka

jasho na machovu bila ya kufanya kazi.
Mtu hujisikia mara kwa mara aende haja kubwa na
akienda hapati choo. Pia humsababishia mtu

kuumwa kwa mgongo au kiuno.
Ikiwa gesi hii itakosa kutoka kwa njia ya haja
kubwa, basi yaweza kupanda juu na kufanya
presha sehemu au karibu ya moyo na kusababisha
maumivu ya moyo.

TIBA:

Chukua Asali safi mbichi iwe ya Asali ya nyuki robo lita , unga wa arki susi vijiko
vitatu vikubwa na unga wa habat soda vijiko viwili

vikubwa. Koroga zote pamoja kwa kijiko. Chukua
vijiko viwili vya mchanganyiko huu ukoroge ndani

ya kikombe cha maji ya moto halafu yakishapoa
unywe kikombe kimoja kutwa mara mbili asubuhi

na jioni.

Ni vyakula gani ambavyo vinasababisha sana gesi kujaa tumboni?.
 
ndio hizo dawa zinapatikana kwenye maduka ya Dawa hapo Kariakoo Asali upate yenye nyuki Wakubwa sio wadogo tena hiyo asali upate mbichi safi isiyochanganywa na sukari mkuu. Kwani wewe asali ukila inakudhuru?[/QU Ahsante mkuu ila mie asali inanidhuru maana hata nikiona tu natapika bila hata kuila . Labda kama kuna tiba mbadala
 
ndio hizo dawa zinapatikana kwenye maduka ya Dawa hapo Kariakoo Asali upate yenye nyuki Wakubwa sio wadogo tena hiyo asali upate mbichi safi isiyochanganywa na sukari mkuu. Kwani wewe asali ukila inakudhuru?[/QU Ahsante mkuu ila mie asali inanidhuru maana hata nikiona tu natapika bila hata kuila . Labda kama kuna tiba mbadala
Tumia Dawa hii kama una ugonjwa wa Gesi Gesi Na Maumivu:
bugia unga laini wa Habbat-Sawdaa kiasi cha kijiko kimoja kabla ya kula chakula ukichanganya na gilasi ya maji yenye vuguvugu iliyotiwa asali ya muwa kiasi cha vijiko vitatu; fanya hivyo kila siku kwa muda wa wiki moja.
 
naomben msaada wenu jaman kwasababu nasumbuliwa na tatizo la tumbo kuungurum kwa muda mrefu sasa
 
Nendo hisp ukapime pengine ni dall za vidonda vya tumbo!Minyoo na Nk

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Kiasili tumbo kuunguruma ni dalili kuwa linafanya kazi.Likiacha kuunguruma hiyo si dalili nzuri,ndio maana ukienda hospitali daktari anaweka kifaa fulani hivi kusikiliza tumboni kwako;pale anakuwa anataka kujua kama tumbo linaungruma au la na pia anakuwa anasikiliza kama sauti inatoka inavyotakiwa(madr.wenyewe wanajua).

Kuunguruma kwa tumbo sio dalili ya minyoo.Kiasili,minyoo haina mdomo wa kuweza kutoa sauti.Na kuna minyoo mingine ni midogo sana hata haionekani kwa macho,kwa hiyo hatutegemei itoe sauti hadi tuisikie tulioko nje!Kwa hiyo ni vema tukaondoa hisia ya kwamba tumbo likunguruma kuna minyoo.Kiukweli tumbo linaweza likaunguruma lakini hakuna minyoo hali kadhalika unaweza kuwa na minyoo lkn tumbo lisiungurume.Kwa hiyo tumbo kuunguruma sio dalili ya minyoo!

Dalili ya kidonda ni maumivu,kuvuja damu nk.Hali kadhalika vidonda vya tumbo kama vilivyo vidonda vingine dalili zake hazitofautiani sana na vidonda vingine.Kwa hiyo kuunguruma kwa tumbo,hakutoshi kuwa dalili ya vidonda vya tumbo!Unaweza kuwa na vidonda vya tumbo lkn tumbo lisiungurume hali kadhalika tumbo linaweza kuunguruma lakini usiwe na vidonda vya tumbo.Ingawa hata hiyo,ikiwa kuna damu nyingi inavuja kwenye utumbo tumbo linaweza kuunguruma lakini hiyo isingekuwa ndiyo dalili ya mwanzo.

Kuunguruma kwa tumbo(bowel sounds) kama nilivyosema ni asili ya tumbo lolote linalofanya kazi.Inapotokea sauti ya muungurumo inakuwa kubwa(hyperactive bowel sounds) kiasi cha kusikika huku nje ni dalili kuwa utumbo unafanya kazi isivyo kawaida;mara nyingi kunakuwa na dalili zingine zilizotangulia au zinazofuata kwa mfano kuharisha au tumbo kuuwasha/kuuma.

Sababu kubwa ya tatizo hili ni chakula tunachokula.Ikiwa una allergy/hypersensitivity na chakula fulani,tumbo linaweza kuunguruma tu bila kuuma au kuwasha.Isipokuwa utagundua tu kwamba kuna chakula fulani ukila ndio unaliona tatizo hilo.Bahati mbaya sana chakula tunachokiita kizuri au kitamu ni kile kilichoungwa vikorokoro viiingi.. Mara nyingi kati ya hivyo,kimojawapo au baadhi vinawezakuwa tumbo lako halikubaliani navyo,kwa hiyo unajikuta katika maisha yako tumbo linakusumbua tuu..bila kujua sababu hasa ni nini.

Sababu nyingine ni:
1.Ugonjwa wa kuharisha na maambukizi(infection) tumboni.
2.Kujisokota kwa utumbo(mechanical intestinal obstustion)
3.Njaa.

Lakini pia kuna wakati tumbo linaweza kuunguruma bila sababu yoyote ya msingi!
 
WanaJF,

Tafadhalini niambieni nini husababisha tumbo kuunguruma mara kwa mara hata kama mtu amepimwa vipimo vyote hospitalini na kuonekana kuwa hana minyoo au vidonda tumbo ambavyo mara nyingi husemekana kusababisha tumbo kujaa gesi na kuunguruma!

Je,ni kweli kuwa kama mtu ana matatizo ya tumbo kuunguruma mara kwa mara awapo faragha na mwenzi wake inaweza kuwa ni chango? Chango la tumbo ni ugonjwa gani na tiba yake ni nini? Je,chango la tumbo linaweza kusababisha madhara ya upungufu wa nguvu za kiume au kike na wakati mwingine kukosa kabisa uwezo wa kuzalisha?

Nawasilisha kwenu wataalamu,MziziMkavu na wadau wote.
 
KULA HIVI KUONDOA MATATIZO YA TUMBO KUJAA GESI NA KUUNGURUMA.




attachment.php


water-bottle-glass-by-nkzs.jpg





KWA njia moja au nyingine, unajikuta tumbo limechafuka kwa kujaa gesi, kuuma na hata kuunguruma, unahisi unahitaji kunywa dawa ili litulie. Katika makala ya leo utajifunza njia bora ya kutuliza mchafuko wa tumbo kwa kutumia vyakula badala ya dawa za kisasa ambazo hutuliza dalili na haziondoi tatizo.



CHANZO


Kabla ya kukimbilia kwenye tiba, ni vizuri kwanza kujua chanzo cha tatizo na katika hili unahitaji kujua ni vyakula gani ukila vinasababisha matatizo ya tumbo. Aina ya vyakula inaweza kutofautiana kati ya mtu na mtu lakini kuna aina ya vyakula vinajulikana zaidi kusababisha matatizo ya tumbo.


Kwa mujibu wa Mkurugezni wa Tiba wa Chuo Kikuu cha Tolune. DK. Timothy S. Harlan (M.D) ambaye pia anajulikana kwa jina la utani kama Dk. Gourment, vyakula na vinywaji vinavyochangia tumbo kujaa na ukosefu wa choo kwa muda mrefu huwa ni soda, ulevi (hasa bia), vyakula vyenye mafuta mengi na vyenye chumvi nyingi.


Kwa mujibu wa Dk. Harlan, vyakula hivyo vinapoingia tumboni, huwa na tabia ya kuchelewesha usagaji wa chakula na uondoaji wa uchafu kwenye utumbo, hivyo huwa kikwazo katika mfumo mzima wa usagaji chakula kwa urahisi.

Ili kujiepusha na matizo ya tumbo ya muda mrefu na hata kuzuia uwezekano wa kuumwa na tumbo mara kwa mara, unashauriwa kula vifuatavyo, karibu kila siku ili kulifanya tumbo lako kuwa safi wakati wote:

PAPAI (PAPAYA)


Baadhi ya utafiti uliyopo, unaonesha kwamba ‘enzyme' waliyomo kwenye papai husaidia usagaji wa chakula tumboni na hivyo kulifanya tunda hili kuitwa na mtafiti wa zama za kale Christopher Columbus kama ‘tunda la malaika'.


Watafiti wamebaini kuwa tunda hili, lenye ladha tamu na harufu nzuri, huboresha mfumo wa usagaji chakula, husafisha utumbo, huzuia magonjwa ya uvimbe tumboni na huimarisha mfumo wa kinga ya mwili.


"Vitamini na virutubisho vya papai vina faida nyingi, lakini faida kubwa ya papai ipo kwenye kirutubisho (Enzyme) aina ya ‘Papain' ambacho hujulikana kwa uwezo mkubwa ilionao wa usagaji mzuri wa chakula tumboni," anasema Dk. Cari Case mwandishi wa blog ya masuala ya afya.


Mwandishi huyo anaongeza kwa kusema kuwa papai limekuwa likitumika kama tiba tangu karne ya 18, lakini utafiti wa kisayansi haukugundua faida za papai hadi mwaka 1870 wanasayansi walipogundua kirutubisho cha ‘papain kilichomo kwenye papai na tangu wakati huo tafiti nyingi zimekuwa zikifanywa kuhusu faida za tunda hili na uwezo wa tiba iliyonalo.


MTINDI (YOGURT)


Hata kama wewe si mpenzi wa mtindi, jaribu kunywa na utaupenda, hasa uwezo wake wa kuondoa matatizo ya kujaa gesi tumboni pamoja na matatizo mengine. Mtindi mzuri ni ule ‘plain' ambao haujachanganywa na ladha au vitu vingine kwa lengo la kuongeza
ladha. Bakteria asilia waliyomo kwenye maziwa mtindi ndiyo hufanya usagaji wa chakula kuwa mwepesi.

Mwisho, ili kupata faida ya papai na mtindi kama ilivyoelezwa hapo juu, ni vizuri ukala mara kwa mara kama siyo kila siku, kabla au mara baada ya kula vyakula ambavyo vinaweza kukuletea shida tumboni, au ukaweka mazoea ya kula kila siku ili kuliweka tumbo lako katika hali salama.


Kunywa Maji Mengi Ya Uvuguvugu.

Kwa Mtu Mgonjwa wa Maradhi yoyote inatakikana awe anakunywa maji Uvuguvugu unapo amka

Asubuhi kabla ya kupiga mswaki unywe Glasi 2 za Maji ya Uvugvugu na baada ya kupiga Mswaki

anywe glasi 1 na kabla ya kunywa chai unywe Glasi moja ya maji moto kila siku afanye hivyo

kwa wakati wa asubuhi.


Na Wakati wa mchana Dakika 15 au dakika 30 kabla ya kula chakula cha mchana unywe maji ya moto au Maji ya Uvuguvugu Glasi 1.

Na Wakati wa chakula cha Usiku unatakiwa unywe Maji ya Uvuguvugu Glasi 2 kabla ya kula chakula cha usiku.

na unywe Maji Ya Uvuguvugu Glasi 1 kabla ya kwenda kulala usiku.Mkuu.@
kisugujira
 

Attachments

  • Papai.jpg
    Papai.jpg
    16.8 KB · Views: 12,391
Tumbo kuunguruma laweza sababishwa na mambo kadhaa, hii ni dalili mojawapo mgandamano au mlundikano wa taka tumboni ujulikanao kwa kitaalam kama "COPROSTASIS", tatizo hili lisipotatuliwa mapema upelekea mtu kuwa katika hatari ya kupata saratani ya utmbo mpana, ama COLON CANCER, FUATILIA UZI HUU KUHUSU COLON CANCER ni vyema kuchukua taadhari kwa kuwa na desturi ya kusafisha matumbo yetu mara kwa mara kujiepusha na magonjwa mengi mbalimbali.

Wataalamu wanasema - "90% of all chronic diseases comes from unhealthy colon", what are those chronic Diseases? SOMA UZI HUO HAPO JUU

ni PM au nitwangie kwa maelekezo zaidi +255784475576.

<strong><font size="3">

 
Last edited by a moderator:
WanaJF,

Tafadhalini niambieni nini husababisha tumbo kuunguruma mara kwa mara hata kama mtu amepimwa vipimo vyote hospitalini na kuonekana kuwa hana minyoo au vidonda tumbo ambavyo mara nyingi husemekana kusababisha tumbo kujaa gesi na kuunguruma!

Je,ni kweli kuwa kama mtu ana matatizo ya tumbo kuunguruma mara kwa mara awapo faragha na mwenzi wake inaweza kuwa ni chango? (Chango la tumbo ni ugonjwa gani na tiba yake ni nini?) Je,chango la tumbo linaweza kusababisha madhara ya upungufu wa nguvu za kiume au kike na wakati mwingine kukosa kabisa uwezo wa kuzalisha?

Nawasilisha kwenu wataalamu,MziziMkavu na wadau wote.
Hujatuambia wewe kwanza ni Mwanamme au Mwanamke? mbona unatuchanganya? Nijuavyo mimi kuhusu ( Chango la tumbo ni ugonjwa wa wanawake) sasa wewe ni

Mwanamke? Kwa wanaume wanapata ugonjwa wa ngiri sio chango la tumbo. Hebu fuata ushauri wa mkuu

MziziMkavu hapo chini utafanikiwa.Ukiwa na ngiri inaweza kukupunguzia nguvu za kiume na kama unataka

Dawa za kuongeza Nguvu za kiume tembelea hapa
https://www.jamiiforums.com/jf-doctor/196934-dawa-za-nguvu-za-kiume-kwa-anayetaka.html
 
Back
Top Bottom