Tulivyojengwa JKT 1970

Tulivyojengwa JKT 1970

RUVU JKT
HIFADHI YA MAISHA YANGU: (NAKUMBUKA NATAFAKARI SANA, NASONONEKA)

1.1 Ni kwanza kondoka kwetu, napenda hilo mjuwe;
1.2 Niko Ruvu nathubutu, kujenga Taifa liwe,
1.3 Kishapo nirudi kwetu, mengineyo nipangiwe,
1.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

2.1 Ninang'arisha viatu, na magwanda niyafuwe,
2.2 Kisha nibebe mtutu, shabaha nijaribiwe,
2.3 Kamwe sitouwa mtu, ila nchi ivamiwe,
2.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

3.1 Ubongo siote kutu, twenda elimu tugawe,
3.2 Twafundisha watukutu, pia wazazi wenyewe,
3.3 Ghafla twaona chatu, wacha mbio tuzitowe,
3.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

4.1 Ruvu Chini shamba letu, ardhi tuitibuwe,
4.2 Tunapanda kila kitu, mpunga na njugumawe,
4.3 Shamba kamwe si msitu, bora mazao yakuwe,
4.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

5.1 Twabeba mapanga yetu, wasitutishe nguruwe,
5.2 Mashoka yaliyo butu, inabidi tuyanowe,
5.3 Tuwezefyeka misitu, mpingo tuuondowe,
5.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

6.1 Ufugaji kazi yetu, wavivu msitujuwe,
6.2 Tule nyama kefu yetu, na maziwa tukamuwe,
6.3 Ngozi nazo ni sapatu, pia jamvi zikaliwe,
6.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

7.1 Afande yu mwanagutu, anenayo muambiwe?
7.2 Adhani atenda utu, siutaki udadawe,
7.3 Tanga nina wangu Fatu, mwambeni asinijuwe,
7.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

8.1 Walojawa ukurutu, wataka waabudiwe?
8.2 Eti sisi 'recruit', adabu sawa tutiwe,
8.3 Liko wapi kosa letu, hadi haya tutendewe?
8.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

9.1 Imara fuadi zetu, nchi hii tu wenyewe,
9.2 Uzalendo sifa yetu, si sawa tuonelewe,
9.3 Wengi wetu Wabantu, haiswihi tuchezewe!
9.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

10.1 Twangoja majibu yetu, ili vyuo tupangiwe,
10.2 Tukanowe vichwa vyetu, mambo mengi tuyajuwe,
10.3 Tuijenge nchi yetu, uchumi wake ukuwe,
10.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

11.1 Sitobadilika katu, pendo langu kwako wewe,
11.2 Tanga wewe u mwenetu, sina wako mfanowe,
11.3 Sitokucheza upatu, daima mimi ni wewe,
11.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

Omari R. Nundu
D Coy, RUVU JKT
27 Disemba 1970
Hii imekaa vizuri mkuu.
hapan shaka baada ya hapo uliuona ''Mlima'' na akina Jenerali.
 
Hiyo JKT haikukusaidia muliharibu mazingira kwa kufyeka misitu na kuondoa mpingo ambayo ni miti adimu duniani inatakiwa mshitakiwe kwa uharibifu wa mazingira pia muliopita jkt enzi hizo ndiyo mumefilisi nchi kwa ufisadi endelevu Mara Richmond hatujapumua meremeta hatujakaa tegeta escrow.
 
Kila mmoja wetu ana uhuru wa kusema na jambo usilolijuwa ni usiku wa kiza hivyo tahadhari ni muhimu kwani ulimi hauna mfupa. Ni tabia murua ya binadamu kuchunguza kujuwa ukweli, kujiridhisha, kuamini halafu ndio kueneza. Ukifanya vinginevyo unapungukiwa na sifa za ukhalifa duniani. Matokeo unaendeleza chuki kuhusu Fulani kitu ambacho ni sifa ya viumbe wengine sio binadamu!

Maneno mazito sana hayo kwa wenye kufikiri.
 
Mzee Nundu,
Mi nashauri tu kua ni vizuri ukaandika kitabu au vitabu kufumbua hayo yaliyoko moyoni mwako, ukaainisha hoja na matukio kinagaubaga ili sisi wananchi tukupate kwa ufasaha. Haya mashairi ni mazuri lakini hayatupi picha ya nini unataka kusema!
Kiapo mzeee! Yale maneno wanayoapa huku wameshika vitabu vitakatifu yanawazuia kunena. Karibu na mwisho huwa nasikia wanasema ........NA KWA VYOVYOTE VILE SITATOA SIRI ZA BARAZA LA MAWAZIRI.....

Kwangu mimi naona mzee Nundu alishughulikiwa tu, huyu mzee ni mzalendo.
 
Kiapo mzeee! Yale maneno wanayoapa huku wameshika vitabu vitakatifu yanawazuia kunena. Karibu na mwisho huwa nasikia wanasema ........NA KWA VYOVYOTE VILE SITATOA SIRI ZA BARAZA LA MAWAZIRI.....

Kwangu mimi naona mzee Nundu alishughulikiwa tu, huyu mzee ni mzalendo.
Hivi sera sijui sheria ya whistleblowing iliishiaga wapi? Hivi viapo vina sambaratisha taifa.
 
RUVU JKT
HIFADHI YA MAISHA YANGU: (NAKUMBUKA NATAFAKARI SANA, NASONONEKA)

1.1 Ni kwanza kondoka kwetu, napenda hilo mjuwe;
1.2 Niko Ruvu nathubutu, kujenga Taifa liwe,
1.3 Kishapo nirudi kwetu, mengineyo nipangiwe,
1.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

2.1 Ninang'arisha viatu, na magwanda niyafuwe,
2.2 Kisha nibebe mtutu, shabaha nijaribiwe,
2.3 Kamwe sitouwa mtu, ila nchi ivamiwe,
2.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

3.1 Ubongo siote kutu, twenda elimu tugawe,
3.2 Twafundisha watukutu, pia wazazi wenyewe,
3.3 Ghafla twaona chatu, wacha mbio tuzitowe,
3.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

4.1 Ruvu Chini shamba letu, ardhi tuitibuwe,
4.2 Tunapanda kila kitu, mpunga na njugumawe,
4.3 Shamba kamwe si msitu, bora mazao yakuwe,
4.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

5.1 Twabeba mapanga yetu, wasitutishe nguruwe,
5.2 Mashoka yaliyo butu, inabidi tuyanowe,
5.3 Tuwezefyeka misitu, mpingo tuuondowe,
5.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

6.1 Ufugaji kazi yetu, wavivu msitujuwe,
6.2 Tule nyama kefu yetu, na maziwa tukamuwe,
6.3 Ngozi nazo ni sapatu, pia jamvi zikaliwe,
6.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

7.1 Afande yu mwanagutu, anenayo muambiwe?
7.2 Adhani atenda utu, siutaki udadawe,
7.3 Tanga nina wangu Fatu, mwambeni asinijuwe,
7.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

8.1 Walojawa ukurutu, wataka waabudiwe?
8.2 Eti sisi 'recruit', adabu sawa tutiwe,
8.3 Liko wapi kosa letu, hadi haya tutendewe?
8.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

9.1 Imara fuadi zetu, nchi hii tu wenyewe,
9.2 Uzalendo sifa yetu, si sawa tuonelewe,
9.3 Wengi wetu Wabantu, haiswihi tuchezewe!
9.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

10.1 Twangoja majibu yetu, ili vyuo tupangiwe,
10.2 Tukanowe vichwa vyetu, mambo mengi tuyajuwe,
10.3 Tuijenge nchi yetu, uchumi wake ukuwe,
10.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

11.1 Sitobadilika katu, pendo langu kwako wewe,
11.2 Tanga wewe u mwenetu, sina wako mfanowe,
11.3 Sitokucheza upatu, daima mimi ni wewe,
11.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

Omari R. Nundu
D Coy, RUVU JKT
27 Disemba 1970

dah....!! ase umenigusa ruvu ndo kambi yangu
AH 3570 SM SYLVESTER PIUS KAKANI
832 KJ RUVU JKT
OP MIAKA 50 JKT
Jun 2013-Sep 2013
KWA MUJIBU WA SHERIA
D COY
 
Mzee Nundu,
Mi nashauri tu kua ni vizuri ukaandika kitabu au vitabu kufumbua hayo yaliyoko moyoni mwako, ukaainisha hoja na matukio kinagaubaga ili sisi wananchi tukupate kwa ufasaha. Haya mashairi ni mazuri lakini hayatupi picha ya nini unataka kusema!


Aandike kitabu, OK. Lakiji Je, watanzania wana utamaduni wa kusoma vitabu? Boraa aandike humu kwanza kwani wengi wasio na tamaduni ya kusoma vitabu watafikiwa upesi.
 
dah....!! ase umenigusa ruvu ndo kambi yangu
AH 3570 SM SYLVESTER PIUS KAKANI
832 KJ RUVU JKT
OP MIAKA 50 JKT
Jun 2013-Sep 2013
KWA MUJIBU WA SHERIA
D COY

clush program
 
RUVU JKT
HIFADHI YA MAISHA YANGU: (NAKUMBUKA NATAFAKARI SANA, NASONONEKA)

1.1 Ni kwanza kondoka kwetu, napenda hilo mjuwe;
1.2 Niko Ruvu nathubutu, kujenga Taifa liwe,
1.3 Kishapo nirudi kwetu, mengineyo nipangiwe,
1.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

2.1 Ninang'arisha viatu, na magwanda niyafuwe,
2.2 Kisha nibebe mtutu, shabaha nijaribiwe,
2.3 Kamwe sitouwa mtu, ila nchi ivamiwe,
2.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

3.1 Ubongo siote kutu, twenda elimu tugawe,
3.2 Twafundisha watukutu, pia wazazi wenyewe,
3.3 Ghafla twaona chatu, wacha mbio tuzitowe,
3.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

4.1 Ruvu Chini shamba letu, ardhi tuitibuwe,
4.2 Tunapanda kila kitu, mpunga na njugumawe,
4.3 Shamba kamwe si msitu, bora mazao yakuwe,
4.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

5.1 Twabeba mapanga yetu, wasitutishe nguruwe,
5.2 Mashoka yaliyo butu, inabidi tuyanowe,
5.3 Tuwezefyeka misitu, mpingo tuuondowe,
5.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

6.1 Ufugaji kazi yetu, wavivu msitujuwe,
6.2 Tule nyama kefu yetu, na maziwa tukamuwe,
6.3 Ngozi nazo ni sapatu, pia jamvi zikaliwe,
6.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

7.1 Afande yu mwanagutu, anenayo muambiwe?
7.2 Adhani atenda utu, siutaki udadawe,
7.3 Tanga nina wangu Fatu, mwambeni asinijuwe,
7.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

8.1 Walojawa ukurutu, wataka waabudiwe?
8.2 Eti sisi 'recruit', adabu sawa tutiwe,
8.3 Liko wapi kosa letu, hadi haya tutendewe?
8.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

9.1 Imara fuadi zetu, nchi hii tu wenyewe,
9.2 Uzalendo sifa yetu, si sawa tuonelewe,
9.3 Wengi wetu Wabantu, haiswihi tuchezewe!
9.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

10.1 Twangoja majibu yetu, ili vyuo tupangiwe,
10.2 Tukanowe vichwa vyetu, mambo mengi tuyajuwe,
10.3 Tuijenge nchi yetu, uchumi wake ukuwe,
10.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

11.1 Sitobadilika katu, pendo langu kwako wewe,
11.2 Tanga wewe u mwenetu, sina wako mfanowe,
11.3 Sitokucheza upatu, daima mimi ni wewe,
11.4 Nimeshakuaga kwetu, lolote Mola naliwe!

Omari R. Nundu
D Coy, RUVU JKT
27 Disemba 1970

upo vizuri sna mzee tatizo upo ccm hapo ndo pagumu.
 
Tatizo la umma dhidi ya cream ya TANU YOUTH LEAGUE 70s NI KUWA MLIMALIMALIZA ELIMU ZA JUU NA JESHINI MLIENDA ILA MLIPOPEWA PROMOSHENI CHAMANI MKAWA MIUNGU WATU....MARAFIKI ZENU KWENYE SU...NA SERIKALINI WAMEBOMOA MAADILI KIASI SASA BADO WAZEE KAMA ANDREA CHENGE NDIO WAPIGA DEAL VIONGOZI.

MH. NUNDU YUKO SAHIHI LAKINI WENZAKO HAWAYAISHI MAISHA HAYO YA HOFU YA MUNGU....
 
kwanza kabisa nakupongeza mh Nundu kwa ujasiri na uzalendo uliouonyesha wa kukubali kuacha uliyokuwa unayafanya na kuamua kutumia weledi, uzoefu na taaluma yako katika kuwatumikia watanzania katika nafasi ya uwaziri. wengi wetu tunajua sana mambo ya mtaani na hata hoja zetu zinajengwa kwa knowledge ya mtaani ndio maana unaambiwa hayo. ni wachache sana watakusemea vizuri kwan siku zote ukitanguliza chuki mtu au jambo fulani ni dhahiri hata maamuzi au maandishi yako yatabaki kuwa ya namna hiyo. Naamini kwa wanaoamini katika hazina ya busara na hekima ya nyie wazee wetu wamefurahi kwa kutasoma shairi lako na kujifunza kitu. If they can learn to hate, they can be taught to love. Mandela
 
Hivi kwa nini unanitukana? Siruhusiwi kuandika humu mawazo na hisia zangu? Hata hivyo asante sana.
mzee wangu sijakutukana ??? kwanza nakuheshimu sana
hapa ni jukwaa huru na mimi nimeandika ninavyosijikia
:focus::focus:
 
Back
Top Bottom