1. Kupakwa GV kwenye kidonda
2. Kung'olewa jino kwa uzi
3. Ubwabwa kupikwa jumapili tu
4. Kidonda kuwekwa unga wa 'rangi mbili' a.k.a tetesakrin
5. Kupamba kadi na pamba sebuleni
6. Ukumbi wa sherehe kupambwa kwa toilet paper
7. Kunyolewa kwa mkasi
8. Kufunga pesa kwenye leso au pindo la kanga
9. Wavulana kuvaa nguo ya ndani aina moja nchi nzima (VIP), usiombe ikakatika ukakuta imebana kifua.
10. Ku rewind kanda kwa peni
11. Nchi nzima Kuangalia Movie ya Commando John, Double Impact, Rambo na Bruce Lee..
12. Watoto Wa Mtaa Mzima Kufahamiana sababu ya kucheza Wote Jioni Kombolela na Kibaba..
13. Kuunguzana na tunda ya Ubuyu baada ya kulisugua chini
14. Kukata ndala, ati ni kifutio
15. Kunyolewa msalaba shuleni kisa nywele ndefu
16. Kuweka Vibox box kwenye Shati la shule Mgongoni..
17. Kuweka Shati la Shule "Blue" eti liwe maridadi.
18. Ubitozi Ulikuwa ni Kusimamisha Kora Ya Shati.
19. Ukiandika Barua kwa Umpendae lazima uchore moyo na Mkuki na lazima upulizie Pafyumu ya "YU".
20. Hata kama Mlikuwa mmegombana January lakini Mtu anakuambia "Utaipata Siku Ya Kufunga Shule".
Je wewe unakumbuka nini??
Nimeipenda hii...kumbuka bitoz lilitokana na wale wanamuziki maarufu wa Uingereza 'the Beatles.."
Nyingeza:
21. Kwenda shuleni boarding na sanduku la mbao
22. kuvaa mashati ya nylon na kuweka noti nyekundu ya sh. 100 maarufu kama 'masai' kwenye mfuko wa shati kuwakoga wenzako
23. kwa wale wa vijijini kuvaa viatu siku ya Jumapili tu...
24. Magari ya Omo kufika maeneo mbalimbali mjini kuonyesha sinema nyingi zikiwa za 'cow boys' za akina Bud Spencer, Lee Van Cleef, Clint Eastwood, John Wayne na wengineo
25. Kutembea na notebook kwenye mfuko wa nyuma wa kaptura ikiwa na maneno magumu ya kiingereza
26. vijana wa jinsia ya Ke kuwaandikia barua vijana wa Me zikiwa zimezungushwa na michoro ya maua na kuweka 'poda' (powder)