Tulio na bibi/babu wenye vituko na vibwanga tukutane hapa

Hahahaha ikawaje sasa
 
Na bibi yangu akija mgeni anaanza kumsimulia,,
Bibi mzaa mama ukimtambulisha mtu kosa,,kuna ndugu yangu alichumbiwa akaleta mchumba kwa bibi,walivyoondoka sasa,,bibi akaanza kusimulia lea anaolewa kamwanaume kabaya ,kana kipara,kafupii ahahhaha
 
Hahahahahah hiyo kali
Mim bibi hana simu,akiomba apigiwe mtu flan halaf mkawa busy,anaanza nije tu ninunue simu yangu tu akitaka kununuliwa hataki tena
 
Mgemuuliza anaenda kuvifanyia nini
 
Hahahahahah hiyo kali
Mim bibi hana simu,akiomba apigiwe mtu flan halaf mkawa busy,anaanza nije tu ninunue simu yangu tu akitaka kununuliwa hataki tena
wanavituko sio vya nchi hii,mpaka nikawa najiuliza niwazee wangu tuu auu??!ila Uzi huu umenifanya nipate faraja mweh!!!
 
Mashikolo mageni mayooo
 
Rip dearest bibi yangu. Alikuwa na vituko sana alinipenda kuliko wajikuu wote wa ukoo mzima, walikuwa na uchoyo Fulani ila kwangu hakuna kitu ambacho sikula kwake.

Historia inaonesha hakuwai kulala na babu (rip) yaan wakati wa kupata mimba wazee walikuwa wanakuja wanamkamata, babu anafanya yake, mimba tiyari ndo mwisho, hadi mtoto mwingine.

Wakati nakua nilikuta kila MTU analala kivyake. Babu ndo alitangulia mbele za haki.

Vituko vyake sasa uzee kweli fainali,walikuwa ana uwezo wa kukimbizana na wajukuu baadae ya kuiba maembe anakukimbiza umbali wa km hata 300

Alinipenda balaa, alikuwa akipika kabla hajala atatoa ndizi moja tu, aweke kwenye sahani aje kwetu, atauliza luckyline yupo WAP mama alisema hayupo atanisubiri hapo chakula amekifunika kitambaa nikija ananipa nakupa peke yangu ndo ataondoka.

Alikuwa awezagi kula chakula kilicjopikwa na MTU yeyote labda mm. Alikuja kula chakula kilichopikwa na MTU mwingine baadae ya kuzeeka sana.

Alinipenda kupitiliza mpaka kijiji kizima kilijua.
Alipoona nguvu zinapungua akamjulisha kila MTU kuwa siku akifa mm sio wasimzike, wanisubiri nifike,

Kweli mwaka 2015 bibi aliumwa uzeee, kila siku alimwambia mama niende nyumbani bibi nguvu kwisha, Bahati mbaya ndo nilikuwa nimepata kazi sehemu nyingine hata mwezi, nilikosa ruhusa.

Siku moja nilikosa usingizi usiku asubuhi nikamwambia mkurugenzi naomba niende kumuona bibi kabla hajafa ilikuwa j4 mkurugenzi akasema jitahidi uende jmosi kabla ya jos j5 bibi kafariki, nililia sana

Mama alinambia, mpaka anakufa alikuwa anauliza Niko wapi, sijui alitaka kunambia nini?

Basi upendo wa bibi kwangu ulisababisha wajukuu wengine wasinipende, baada ya bibi kufa wakataka wazike kisa mm Niko mbali, kijijin hakuna mochwari, wajukuu wanakomalia wazike, wazee nao wakakomaa, wanisubiri bibi alisema.

Tangu naanza safari nililia kwenye basi nilishindwa kujizuia, nakumbuka upendo wa bibi, yaani zamani bibi akijua nakuja likizo alikaa barabarani na kusubiri Gari nikishuka alitamani anibebe, jamani bibi alinipenda.

Anyway nilipofika msibani nilikuta wapumbavu wajukuu kaka zangu Dada zangu midomo wameivuta hawaniongereshi, sikukuta maandalizi yoyote, namaanisha zile mbwembwe za wajukuu, maua/shada na nilijua hawatafanya, nilivyofika Mjini nikatengeneza yakutosha na nikatafuta waandaaji wa sehemu ya ibada.

Nilipofika nilipokelewa wazee waliopigania wasizike waliponiona walifurahi sana huku wengine wamenuna kuwa wananisubiri mm nani,simnajua mambo ya kijijini, nilipofika nilipata nguvu process zote zikaanza upya. Na bibi yangu akazikwa kama nilivyotaka mm.

Kweli mpaka sasa siamini kama bibi yangu siko nae tena ,nilimkuta kashakuwa wa baridi ndani ya jeneza macho hanioni tena nililia sana nikamuomba msamaha kwa kutofika mapema nilitamani nimbebe mgongoni ila haikuwezekana. Ila naamini alinisikia kuwa nimefika maana niliambiwa kuwa kabla sijafika mambo yalikuwa hayaendi walikuwa wakilazimisha wazike kabla sijafika hata jeneza liliwashinda. Nilipofika tu kila kitu kilikuwa chepesi

Apumzike kwa amani, alifariki akiwa 96-age.nampenda hata Leo.
 
Bibi yangu kila nikienda kumsalimia ilikuwa lzm nilale nae kitanda kimoja, naweza nikampa sababu kibao bhana bibie mm nimeshakuwa mtu mzima bhana acha nikale mwenyewe kwani ananielewa,ila yote hiyo ni kwasababu ndio alinilea toka nikiwa na nilikuwa nalala nae,kitu alichokuwa ananifurahisha zaidi ni imani yake kwa kanisa katoliki,kila siku yy ilikuwa ni kanisani hamna anaacha kwenda labda anaumwa sana,Ila ndio hivyo Mungu alimpenda zaid
RIP bibi
 
Alikua na maana gani kuchemsha jiwe kwenye chungu?
Hiko ni kipindi cha njaa ndio wazazi walikuwa wanafanya hivyo,wamama wanaweka mawe kwenye chungu mnayachochea moto kuanzia asubuh hadi jion wakati huo mzee anapambana huko mpate chakula
 
Rip dearest bibi yangu. Alikuwa na vituko sana alinipenda kuliko wajikuu wote wa ukoo mzima, walikuwa na uchoyo Fulani ila kwangu hakuna kitu ambacho sikula kwake.



Apumzike kwa amani, alifariki akiwa 96-age.nampenda hata Leo.


Pole sana. RIP bibi
 
Bibi yangu alikuwa akitupikia chakula inabidi tule tubakize kidogo, ukimaliza chote haamini kama umeshiba, akija kututembelea nyumbani akiona tunakula bila kusaza anaanza kumgombeza mama kuwa utaua watoto kwa njaa, mama kwa hasira anaamua kupika tena, halafu anashangaa hakuna mtoto anayekula maana mama alikuwa anajua kukadiria. Neno pekee la Kiswahili alilokuwa analijua ni UTASIBA? akimaanisha UMESHIBA? Alikuwa mkarimu mno, nimemmiss mno bibi yangu, R. I. P Bibi
 
Bibi yangu alikuwa akitupikia chakula inabidi tule tubakize kidogo, ukimaliza chote haamini kama umeshiba, akija kututembelea nyumbani akiona tunakula bila kusaza anaanza kumgombeza mama kuwa utaua watoto kwa njaa, mama kwa hasira anaamua kupika tena, halafu anashangaa hakuna mtoto anayekula maana mama alikuwa anajua kukadiria. Neno pekee la Kiswahili alilokuwa analijua ni UTASIBA? akimaanisha UMESHIBA? Alikuwa mkarimu mno, nimemmiss mno bibi yangu, R. I. P Bibi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…