Tulia Ackson ni nani, CV yake ipoje?

Tulia Ackson ni nani, CV yake ipoje?

John Kachembeho

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
560
Reaction score
389
Leo hii katika bunge la katiba, mjumbe mmoja kwa jina la Dk. Tulia Apson alitoa mchango wake makini na wa kisomi sana ikiwa ni pamoja na kuwataka wajumbe sasa waache kujadili watu na kujikita katika mjadala wa rasimu ya katiba.

Kwa manufaa ya wanajukwaa na watanzania kwa ujumla, huyu dada makini Dk Tulia Apson ni nani hasa, anawakilisha kundi gani huko bungeni? Ana nafasi gani katika Tanzania?

========

PERSONAL DETAILS
Surnname: Mwansasu
Middle Name: Ackson
First Name: Tulia
Salutation: Hon. Dr
Marital Status: Married
Date of Birth: 23 Dec. 1976
Place of Birth: Tukuyu Mbeya.
Sex: F
Email: tuliaj@gmail.com
Postal Address: 35093 Dar es Salaam


EDUCATION BACKGROUND

1984 - 1990 Mabonde Primary School Primary Education
1991 - 1994 Lolera Secondary School CSE
1995 - 1997 Zanaki Secondary School ACSE
1998 - 2001 University of Dar es Salaam LLB
2001 - 2003 University of Dar es Salaam LLM
2005 - 2007 University of Cape Town Ph. D


EMPLOYMENT EXPERIENCE
2011 - 2015
University of Dar es Salaam Senior Lecturer
2009 - 2015 University of Dar es Salaam Associate Dean
2001 - 2001 Attorney General's Office Trainee
pic1.jpg

Dk Tulia amezaliwa Novemba 23, 1976 eneo la Bulyaga, wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Alipata elimu ya awali katika Shule ya Mabonde wilayani Tukuyu kati ya mwaka 1984 na 1990 kabla ya kujiunga na shule za Lolera na Zanaki kwa elimu ya sekondari kati ya mwaka 1991 na 1997.

Alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1998 kwa Shahada ya kwanza ya Sheria kabla ya kurejea tena Chuoni hapo mwaka 2001 na kufanikiwa kutunukiwa Shahada ya pili, mwaka 2003.

Mwaka 2005-2007 alijiunga na Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini kwa digrii ya udaktari wa filosofia katika sheria kabla ya kurejea nyumbani na kuhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Februari 2014 Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete alimteua kuwa mbunge wa Bunge Maalum la Katiba (BMK) kabla ya kuteuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Septemba 9, mwaka huu.

Alichukua fomu kuwania Uspika kupitia CCM kabla ya kujitoa dakika za lala salama kisha akateuliwa na Rais Magufuli kuwa mbunge wa viti maalumu kwa mujibu wa madaraka yake ya urais.
 
Hahahaaaa teh haya tena van Damme na Rambo...Govinda na Mithun...nani kubwa la maaduiii???
 
Yaani Mbowe ujanja wake wote amenyooshwa na kuamua kususa
Lakini inasemekana ni janja ya kukwepa kuchangia sheria ya kuanzisha mahakama ya mafisadi,watachangia nini? Wakati wameamua kuukumbatia ufisadi
 
Who is Tulia Ackson? Jipu lililoingizwa Bungeni na Magufuli kwa maelekezo ya kuwaadhibu Wabunge wote wa upinzani ambao huichachafya Serikali Bungeni.
kawaadhibu wapi mkuu,leta hapa ushahidi alipo waadhibu wapinzani.....na ulete na vifungu vinavyoonyesha amekiuka sheria zilizopitishwa na wabunge wenyewe wakiwemo wa upinzani.............................

"asiyeridhika na maamuzi akakte rufaa" - dr.tulia
 
Huyo dada amewashika kijiji ndugu zetu wa Ukawa
 
Back
Top Bottom