Tukumbushane haya mambo matatu!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,065
22,758
Ninayo sababu ya kuanzisha uzi huu. Kuna mambo matano nitayaongelea katika kukumbushana tu na leo naanza na namba moja nayo ni kivuko, MV Dar es Salaam...naomba uvumilivu wenu.

Flashback...January, 2012

magufuli.JPG
Sakata la nauli za vivuko: Magufuli achafua hali ya hewa Dar, awaambia wakazi wa Kigamboni,"asiye na nauli ya Sh. 200 apige mbizi".

Fastforward to September, 2014...

1. MV DAR ES SALAAM


Jumatatu, tarehe 6/9/2014 - Breaking Nyuzz...!!!

KIVUKO KIPYA (MV DAR ES SALAAM) CHAWASILI.

Ile ahadi ya Waziri wa Ujenzi Dkt.John Magufuli ya kununua kivuko kipya kitakachotoa huduma ya usafiri kati ya Jiji la Dar es Salaam na mwambao wa Bahari ya Hindi hadi Bagamoyo imetimia.

Taarifa za uhakikia tulizozipata hivi punde ni kuwa kivuko hicho (Mv Dar es Salaam) kilichokuwa kinajengwa huko Denmark leo kimeshuka majini na tayari kuanza safari ya kuja Dar es Salaam ambapo kinatarajiwa kufika/kutua Dar es Salaam kati ya wiki tatu mpaka nne zijazo.

Kivuko cha MV Dar es Salaam kitakuwa na kasi kuliko kivuko chochote Afrika ya Mashariki na hasa mwambao wa bahari ya Hindi ukiacha Afrika ya Kusini.

Kivuko hiki ni muendelezo wa juhudi za Wizara ya Ujenzi za kupunguza msongamano katika Jiji la Dar es Salaam...

2.JPG


Kivuko cha MV Dar es Salaam kama kilivyoonekana juu ya Meli kabla ya kushushwa majini katika bandari ya Dar es Salaam.

1.JPG


Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiki Meli kubwa ya mizigo iliyobeba Kivuko kipya cha MV Dar es Salaam ilipokuwa inakaribia kutia nanga katika bandari ya Dar es Salaam.


MV%2BDARESSALAAM%2BPANTONI%2BKIVUKO6.JPG

Waziri wa Ujenzi Dkt. John Magufuli akionesha furaha yake ndani ya Kivuko hicho cha MV Dar es Salaam.

Mpaka hapo maswali yenye utata kuhusu hiki kivuko ni haya;

  1. Kilikuwa kipya?
  2. Kilijengwa Denmark?
  3. Kiligharimu kiasi gani?
Ijumaa 27/2/2015 - Breaking Nyuzz...!!!

KIVUKO KIPYA (MV DAR ES SALAAM) CHAFANYIWA UKAGUZI.

Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli amekagua safari ya kivuko cha Mv Dar es Salaam kwa mara ya kwanza hadi Bagomoyo, huku kukiwa na changamoto kadhaa miezi michache kabla ya uzinduzi rasmi wa huduma hiyo.

"Mbali na kuongeza pato la taifa, pia kivuko hiki kitapunguza kwa namna moja ama nyingine foleni za jiji la Dar es Salaam na kukuza utalii," alisema Magufuli

“Kulikuwa na maneno mengi kuwa kivuko hakipo… na wale waliokuwa hawaamini kimekuja, wakitaka wakiguse,” alisema Dk Magufuli na kushangiliwa na umati uliokuwa feri kabla ya kuanza ukaguzi.

“Hiki kivuko ni cha aina yake hata maegesho yake ni tofauti. Niwapongeze wenzetu wa jeshi na nina uhakika wataifanya kazi ya kujenga kwa haraka,” alisema Dk Magufuli.

Kivuko cha Mv Dar es Salaam kimejengwa kwa ustadi wa hali ya juu na huduma nzuri za kukaa kama meli ya kitalii.

unnamed%2B(38).jpg


Kivuko cha MV Dar es Salaam kikiwa njiani kuwasili eneo la Magogoni kwa ajili ya kuanza safari ya kwanza ya majaribio ya kwenda Bagamoyo mkoani Pwani.

magufuli.jpg


Waziri wa Ujenzi Dk John Magufuli akiongoza wakaazi wa jiji kwenye majaribio ya uzinduzi wa kivuko cka MV Dar es Salaam kitakachofanya kazi kati ya DSM na Bagamoyo.

unnamed%2B(36).jpg


Waziri wa Ujenzi John Magufuli akifanya ukaguzi wa MV Dar es Salaam alitoa ahadi kuwa atahakikisha nauli itakuwa nafuu kwa wananchi wote.
Mpaka hapo kuna maswali kadhaa yanayozua utata;
  1. Ufanisi na uimara wake
  2. Gharama za uendeshaji
  3. Lengo kufikiwa.
Kabla sijaendelea nakaribisha maoni, yanaweza kuwa chanya au hasi ila naomba tu lugha ya kiungwana.


 
Duh...
Hizi Nondo hizi
Umenikumbusha Lecturer Mmoja Chuoni bingwa wa ku Complicate.
Katika kufanya Marking aka mix Marking Scheme yake Mwenyewe na Mitihani ya wanafunzi.
Akajikuta anai treat na kui mark kama Mtihani wa Mwanafunzi na kuishia kuipa Karai (C)
 
Unakaribisha maoni ya nini wakati majibu na hitimisho umefanya kabla hata ya kuleta mada yako!

Nadhani umechelewa kuamuka na hufahamu kama kampeni za Uchaguzi zilishaisha na Uchaguzi wa Tanzania umemalizika miezi zaidi ya mitatu iliyopita.

Hakuna kitu kibaya katika siasa kama unafiki.

Ni katika unafiki kama huu ndiyo maana tulisikia baadhi ya wanasiasa wakijitahidi kumsafisha kisiasa mwanasiasa ambaye wao wenyewe walianza kutueleza kuwa ni fisadi papa na wakaendeleza kusisitiza kwa miaka zaidi ya minane lakini siku ambayo lupia ilipenyezwa, wakawa wa kwanza kuyakana maneno yao kinafiki.

Haishangazi UKAWA ni kati ya wale walikuwa wanasema huyu mwanasiasa ni fisadi papa lakini nitampa kura yangu!

Kupambana kihoja na Serikali ya Rais Magufuli lazima kwanza ujivike ujinga au upumbavu kama wewe siyo mpumbavu au mjinga!

Kwa sasa hata wajinga pia wamekuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuhusu utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Wapumbavu wameamua kujilipua ili upumbavu wao ufahamike kwa wengi hapa Jamiiforums!

Wengine kwa sasa wanatafuta shule zinazofundisha ujinga ili wakasome na wapate hoja za kuweza kupambana na utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Awamu hii ya tano tutaona na kusikia mengi!
 
Unakaribisha maoni ya nini wakati majibu na hitimisho umefanya kabla hata ya kuleta mada yako!

Hakuna kitu kibaya katika siasa kama unafiki na ndumila kuwili.

Ni katika unafiki kama huu ndiyo maana tulisikia baadhi ya wanasiasa wakijitahidi kumsafisha kisiasa mwanasiasa ambaye wao wenyewe walianza kutueleza kuwa ni fisadi papa na wakaendeleza kusisitiza kwa miaka zaidi ya minane lakini siku ambayo lupia ilipenyezwa, wakawa wa kwanza kuyakana maneno yao kinafiki.

Haishangazi UKAWA ni kati ya wale walikuwa wanasema huyu mwanasiasa ni fisadi papa lakini nitampa kura yangu!

Kupambana kihoja na Serikali ya Rais Magufuli lazima kwanza ujivike ujinga au upumbavu kama wewe siyo mpumbavu au mjinga!

Kwa sasa hata wajinga pia wamekuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuhusu utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Wapumbavu wameamua kujilipua ili upumbavu wao ufahamike kwa wengi hapa Jamiiforums!

Wengine kwa sasa wanatafuta shule zinazofundisha ujinga ili wakasome na wapate hoja za kuweza kupambana na utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Awamu hii ya tano tutaona na kusikia mengi!
ukweli unauma..vumilia kiaina dawa ingiir vizuri mkuu
 
Unakaribisha maoni ya nini wakati majibu na hitimisho umefanya kabla hata ya kuleta mada yako!

Hakuna kitu kibaya katika siasa kama unafiki na ndumila kuwili.

Ni katika unafiki kama huu ndiyo maana tulisikia baadhi ya wanasiasa wakijitahidi kumsafisha kisiasa mwanasiasa ambaye wao wenyewe walianza kutueleza kuwa ni fisadi papa na wakaendeleza kusisitiza kwa miaka zaidi ya minane lakini siku ambayo lupia ilipenyezwa, wakawa wa kwanza kuyakana maneno yao kinafiki.

Haishangazi UKAWA ni kati ya wale walikuwa wanasema huyu mwanasiasa ni fisadi papa lakini nitampa kura yangu!

Kupambana kihoja na Serikali ya Rais Magufuli lazima kwanza ujivike ujinga au upumbavu kama wewe siyo mpumbavu au mjinga!

Kwa sasa hata wajinga pia wamekuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuhusu utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Wapumbavu wameamua kujilipua ili upumbavu wao ufahamike kwa wengi hapa Jamiiforums!

Wengine kwa sasa wanatafuta shule zinazofundisha ujinga ili wakasome na wapate hoja za kuweza kupambana na utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Awamu hii ya tano tutaona na kusikia mengi!
Mkuu
Unaonaje ukaanzisha a Separate thread for this.
Tutakuja huko kuchangia pia.
Hapa tunajikita kwenye MV Dar es Salaam.
Unatuharibia Floo na mtitiriko wa uchangiaji Ndugu.
 
Duh...
Hizi Nondo hizi
Umenikumbusha Lecturer Mmoja Chuoni bingwa wa ku Complicate.
Katika kufanya Marking aka mix Marking Scheme yake Mwenyewe na Mitihani ya wanafunzi.
Akajikuta anai treat na kui mark kama Mtihani wa Mwanafunzi na kuishia kuipa Karai (C)
Umenikumbusha huyu mzee anaitwa Dr Bruda Itandala

Duc in Altum
 
Unakaribisha maoni ya nini wakati majibu na hitimisho umefanya kabla hata ya kuleta mada yako!

Hakuna kitu kibaya katika siasa kama unafiki na ndumila kuwili.

Ni katika unafiki kama huu ndiyo maana tulisikia baadhi ya wanasiasa wakijitahidi kumsafisha kisiasa mwanasiasa ambaye wao wenyewe walianza kutueleza kuwa ni fisadi papa na wakaendeleza kusisitiza kwa miaka zaidi ya minane lakini siku ambayo lupia ilipenyezwa, wakawa wa kwanza kuyakana maneno yao kinafiki.

Haishangazi UKAWA ni kati ya wale walikuwa wanasema huyu mwanasiasa ni fisadi papa lakini nitampa kura yangu!

Kupambana kihoja na Serikali ya Rais Magufuli lazima kwanza ujivike ujinga au upumbavu kama wewe siyo mpumbavu au mjinga!

Kwa sasa hata wajinga pia wamekuwa wachambuzi wa mambo ya kisiasa kuhusu utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Wapumbavu wameamua kujilipua ili upumbavu wao ufahamike kwa wengi hapa Jamiiforums!

Wengine kwa sasa wanatafuta shule zinazofundisha ujinga ili wakasome na wapate hoja za kuweza kupambana na utendaji wa serikali ya Rais Magufuli!

Awamu hii ya tano tutaona na kusikia mengi!




Naamini umejibu/kuchangia hii mada kwa kukurupuka!,laiti ungejipa muda wa kutafakari na kuvuta pumzi ya kutosha ili kuruhusu hewa safi iingie kwenye mapafu yako,wala usingeandika haya uliyooyaandika.

Tusiwe wepesi wa kusahau na kuwa walipukaji mithiri ya gesi pale tunapoona hoja kinzani.Ninayaandika haya nikiwa na kumbukumbu sahihi,laiti miaka 10 au 5 iliyopita nchi yetu ingekuwa imeongozwa na serikali ya chama tofauti na hii ya Magufuli,hakika ungekuwa na haki ya kupaza sauti na uthubutu wa kukemea ubadhirifu wa serikali iliyotangulia.

Maovu yote ambayo tunaweza kuyaorodhesha hapa yaliyolikumba Taifa letu,chanzo chake ni utendaji na utekelezaji usioridhisha wa wale tuliowapa dhamana ya kuongoza Taifa letu.Tangu Magufuli akalie kitu cha Ikulu,ni eneo moja au mawili aliyoyagusa lakini Taifa limeshuhudia ubadhirifu wa kutisha kiasi cha watu kuhoji kama Tanzania ilishawahi kuwa na serikali hapo awali.

Kama eneo moja limetupa picha halisi ya namna watu walivyokuwa wanashirikiana na maafisa wa Serikali kuliibia Taifa,vipi maeneo mengine yaliyosalia yakimulikwa si utaibuliwa ufisadi wa kutosha kiasi cha kuweza kuwafanya Watanzania "wazimie mioyoni"?

Yaliyobumbuluka Bandarini yanaweza kuwepo katika sekta zote zilizopo nchini.Ulishajiuliza kama haya ndiyo yaliyokuwa yanafanyika huko bandarini,vipi kuhusu sekta Kubwa kabisa hapa nchini ambayo ndiyo inayoongoza kwa kutengewa bajeti Kubwa na kuwa na miradi mingi ya ufadhiri?Namaanisha sekta ya ujenzi hususan ujenzi wa barabara.

Tufike mahali tukubaliane kama Taifa kuwa tumefikishwa hapa na tuliowapa dhamana ya kuliongoza Taifa letu,kama tatizo la msingi la ubadhirifu ndani ya Taifa hili alikuwa ni Mh.Lowassa,mheshimiwa huyu alikuwa nje ya serikali kwa zaidi ya miaka 8,kama yeye ndiye S.I. Unit ya ubadhirifu nchini na alikuwa nje ya mfumo wa serikali,nani aliruhusu ubadhirifu wa kutisha ulikuwa unafanywa na makampuni makubwa hapo bandarini?Nani aliyehusika na uhujumu wa uchumi wa kulikosesha Taifa mapato stahiki kwa kuruhusu kuzimwa kwa mita zilizokuwa zinapima kiasi cha mafuta yaliyokuwa yanaingia nchini ili serikali ipate mgao wake wa 50% kwa mujibu wa sheria? Hivi ni nani aliyenyamanzia kuunganishwa kwa bomba la siri kutoka kwenye mitambo ya kupokelea mafuta bandarini na kwenda moja kwa moja Kigamboni bila kupitia vipimo vyovyote?Mradi mkubwa kiasi hicho ulijengwaje ndani ya Jamhuri yetu tukufu kiasi cha wenye dhamana ya kusimamia ujenzi wasijuwe kwamba kuna bomba chini ya ardhi linalochepusha mafuta na kuyapeleka Kigamboni bila kupimwa?

Uozo wa serikali ya CCM hakuna asiyeujuwa,kashfa zilizolitafuna Taifa hili zipo nyingi mno tena zingine zilitokea ikulu.Ni Tanzania pekee ambako Rais anaweza kujigeuza mjasiliamali hadi kufikia hatua ya kufungua Kampuni ya ANBEN tena kwa anuani ya Ikulu na wanaojiita "WASEMAJI UKWELI" wakakaa kimya.

Serikali inayojinasibu kutumbua majipu,kwa nini isianze na wale waliogawana mabilioni ya Escrow hadharani na kuyabeba kwenye viroba mchana kweupe? Serikali yenye vyombo vyote vya ki- intelejensia imeshindwa kufumbua kitendawili hiki,badala yake vyombo vyake vimeishia kukamata vijana waliokuwa wanakusanya na kujumlisha matokeo ya Urais yaliyokusanywa kutoka vituo vya kupigia kura.

Ni kweli tumehitimu darasa ya ujinga na upumbavu kama ulivyotuita,lakini ujinga na upumbavu wetu hautufanyi tusione madhira ya serikali hii hata kama inajaribu kuturubuni kwa mambo machache.Pamoja na upumbavu wetu,bado tunaweza kupaza sauti ya juu kabisa kukemea mazingaombwe ya serikali,haiwezekani serikali ijinasibu inatowa Elimu bure,halafu ipeleke ruzuku ya sh.600 kwa kila mtoto kwa mwezi kughalamia Elimu ya masikini wa Taifa hili,halafu "WASEMAJI UKWELI" wapige makofi na vigelegele kwamba serikali inawajali masikini wa Taifa hili.

Ni bora upumbavu wa "kuhitimu darasani" unaotuwezesha kutambua kuwa sh.600 kwa mwezi kwa mtoto mmoja haziwezi kuwa muarobaini wa Elimu yetu ya msingi,kuliko busara zenu za kipumbavu zinazokubali ghiliba za aina hii.Hivi ni kweli katika hali ya kawaida kabisa ruzuku ya sh.600 kwa kila mwezi kwa mtoto inaweza kuleta mapinduzi ya Elimu ndani ya Jamhuri yetu tukufu ya Wadanganyika?Namshukuru Mungu aliyenipa ulofa na upumbavu,lakini akanipa pia uwezo wa kutambua ghiliba za wanasiasa na wapambe wao.

Kuitetea kihoja serikali ya CCM unapaswa ujitoe ufahamu,uwe zaidi ya msukule.Hakuna hata moja linalotokea leo ambalo halijaletwa/kusababishwa na serikali yenyewe,kuipigia makofi na kuishangilia katika yale iliyoyaumba kwa mikono yake nafikiri ni upumbavu zaidi ya upumbavu wenyewe.
 
Hawa tuliokuwa wengine tunawaona wazalendo kweli kumbe uzalendo wao unategemea mtu fulani anataka nini. Hawahawa zikija mada za ufisadi tena kwa reference za mabandiko yao na makala za magazeti yao wanaanza kutwist mada .....hawahawa sikuona wakihoji viongozi wao sababu ya kutwist ghafla na kuanza kumsafisha mtu waliyemchafua kisawasawa for years ....hawa nimegundua wanataka mtu "wao" ndio aende ikulu na nje ya hapo yeyote ni adui kwao na wamejiandaa kuwa adui wa yeyote hata afanye kazi gani . Hawa akina Mag3 na wenzake list of shame kutolewa kwenye tovuti ya chama si issue ila nawaambia ingeandikiwa makala 1000 kama hilo lingefanywa na CCM .....ndio maana wanalala wanaota namna ya kuja na mada kama hizi ili wapate cha kusema kwa JPM huku ujinga mwingi uliopo Chadema hawaugusi hata chembe ......huu ni unafiki na wanamtandao wengi akili zinawafunguka ndio maana wengi wameanza kuacha kushabikia vyama.
 
ndugu yangu huu ni mtihani wa imla kwa kiziwi ni ngumu kufaulu umeandika vizuri sana tatizo nani wakumwambia mfalme umechafua hewa ni busara tu zinatakiwa kijakazi mmoja ajitokeze kukubali hilo au wageni wote wa mfalme wakae kimya japo harufy inawakera lakini muda utafika waliotendwa nao wataliuliza ili kwa wananchi
 
Tutumie muda wetu kuangalia namna ya kutoa mawazo ya kumsadia JPM kujenga taifa letu. Kuna vitu watu wanapoanza kulalamika sasa unajiuliza mbona kipindi cha uchaguzi mlishindwa kuzitumia hoja hizi za ufisadi kushinda uchaguzi badala yake kipindi hicho muhimu mkafunika kombe mkiogopa "mnachokijua" then sasa ndio mnajifanya kuja na vimada hivi. Kwanza wahojini viongozi wenu kwanini walishindwa kujenga hoja ikiwemo hii (haikuguswa kabisa) ili wananchi wasimchague JPM wamchague "mtu safi" mliyemsafisha wenyewe? Hebu fanyeni ujasiri wa kuhoji viongozi wenu ili tujue mnaweza kuhoji yeyote bila kujali itikadi zenu.
 
Hawa tuliokuwa wengine tunawaona wazalendo kweli kumbe uzalendo wao unategemea mtu fulani anataka nini. Hawahawa zikija mada za ufisadi tena kwa reference za mabandiko yao na makala za magazeti yao wanaanza kutwist mada .....hawahawa sikuona wakihoji viongozi wao sababu ya kutwist ghafla na kuanza kumsafisha mtu waliyemchafua kisawasawa for years ....hawa nimegundua wanataka mtu "wao" ndio aende ikulu na nje ya hapo yeyote ni adui kwao na wamejiandaa kuwa adui wa yeyote hata afanye kazi gani . Hawa akina Mag3 na wenzake list of shame kutolewa kwenye tovuti ya chama si issue ila nawaambia ingeandikiwa makala 1000 kama hilo lingefanywa na CCM .....ndio maana wanalala wanaota namna ya kuja na mada kama hizi ili wapate cha kusema kwa JPM huku ujinga mwingi uliopo Chadema hawaugusi hata chembe ......huu ni unafiki na wanamtandao wengi akili zinawafunguka ndio maana wengi wameanza kuacha kushabikia vyama.





Inashangaza,kwako wewe kuiondoa orodha ya mafisadi katika tovuti ya Chadema ni kosa Kubwa zaidi kuliko kosa linalofanywa na tuliowapa dhamana la kutowachukulia hatua mafisadi waliopo kwenye hiyo orodha.

Pamoja na wengine,orodha iliwataja waliokuwa marais wa Tanzania,B.W.Mkapa na J.K.Kikwete,kama ishu ni orodha hiyo ni nani aliyechukuliwa hatua hadi sasa kupitia orodha hiyo? Hao niliowataja hapo juu si ndiyo waliotufikisha hapa tulipo?si ndiyo waliovilea vipele kabla havijawa vijipu uchungu na sasa ni majipu yanayotishia usalama wa mwili wa mama Tanzania?

Kama tunataka kuwa wakweli kwa Taifa letu hatupaswi kuuzunguka Ukweli kwa kutafuta utetezi mwepesi ili ionekane nchi hii imefikia hapa kutokana na uozo wa tovuti ya Chadema. Hakuna kiongozi hata mmoja aliyepo Chadema ambaye alitumia dhamana yake ya kuwa kiongozi wa Chadema,kufumbia macho ufisadi na ubadhirifu uliofikia kiasi cha kutia kinyaa unaofanywa na kiongozi waandamizi wa chama na serikali ya CCM.

Hakuna namna ya kuitenganisha Serikali ya ccm na chama chake na matakataka yote yanayoendelea nchini,hakuna.Unapochangia hoja jaribu kuwa mkweli walau kwa nafsi yako,hakuna Mwenye akili timamu anayeweza kuutenganisha uchafu huu na serikali ya CCM.
 
Back
Top Bottom