screpa
JF-Expert Member
- Sep 10, 2015
- 10,792
- 15,693
Muziki wa Bongofleva tangu uanze miaka ya 90 mwishoni umefanikiwa kuibua majina mengi makubwa, lakini tofauti na ilivyo sasa kipindi huu muziki unaanza ilikuwa ili utoboe ni lazima uwe na album. Utamaduni huu wa kutoa album ulipoteza umaarufu kuanzia kwenye miaka ya 2009 hivi ambapo wasanii wamekuwa wakilalamika mauzo kuwa hafifu kutokana na kuibuka wazee wa kudurufu kazi hizo na kuziuza kwa bei chee mtaani, pia mitandao ya kijamii imeathiri kwa kiasi kikubwa mauzo ya album. Baada ya kusema hayo machache tukumbushane wasanii waliofanikiwa kutoa album na majina ya album hizo, wasanii waliowahi kutoa album zikafanya vizuri ni kama Mr II 'Sugu', Profesa Jay Dudubaya, Lady Jaydee, Solo Thang, Gangwe Mobb Jay Moe , Juma Nature, Afande Sele, Crazy GK, TID, Dully Sykes, AY, Mwana FA, Caz T, Soggy Doggy Anter, Mangwea, Mr Ebbo, Banana Zoro, Bwana Misosi, Daz Nundaz,Wagosi Wakaya, Mike T Mnyalu, Bizman, Feruz, Daz Baba, Stara Thomas, Ray C, Noorah, Mr Paul, Parklane, MB DOGGY, Mandojo na Domokaya, Mr Nice, Fid Q, Matonya, Mr Blue, Mh. Temba, Madee, Alikiba, Diamond, n.k
*Album za wasanii wa mwanzoni kama Sugu nilikuwa nazisikiliza kwa mabraza, nikitembelea kwa mabro unakutana na album kama 'Ndani ya Bongo', 'Nje ya Bongo', 'Deiwaka', n.k na kwa Mara ya kwanza nikavutiwa kuupenda huu muziki wa 'kufokafoka', nakumbuka kipindi hicho nilikuwa mtoto wa primary.
**MACHOZI JASHO NA DAMU' ya Profesa Jay, hii Album nakumbuka nilimpiga sound Maza hadi akaninunulia. Ni bonge moja la Album, moja kati ya album bora kupata kutokea kwenye bongofleva yenye nyimbo kama Ndiyo Mzee, Bongo Dar es salaam, Niamini, Jina Langu, Tathmini, n.k
***ULIMWENGU NDIO MAMA' ya Jay Moe, hii nakumbuka nilikuwa form1 Sengerema Sec (boarding), kwa Mara ya kwanza nilitoa hela yangu mfukoni (pocket money) na kuinunua. Kwangu mimi hii ni Album bora kabisa kupata kutokea kwenye Bongo Hiphop, hakuna wimbo wa kuforward mule, utakutana na ngoma kama 'Bishoo', 'Kama Unataka dem', 'Majukumu', 'Maisha ya Boarding', 'Mvua na Jua' na nyingine nyingi. Ukitaka kumjua JayMo huyu ndio alikuwa JayMo wa kweli alikuwa anaandika hasa, sio huyu wa sasa wa 'Pesa ya Madafu', 'Tunakula Bata', huyu wa sasa simuelewi kabisaa, ila ndio hivyo siwezi mlaumu sana maana ni lazima aswitch aendane na hiki kizazi cha 'Instagram'.
****A.K.A MIMI ya Mangwea, huwezi taja album 5 bora za wakati wote kwenye list yako ukaiacha hii album utakuwa na matatizo. Ni moja ya album niliyotoa hela yangu mfukoni na kuinunua, ina nyimbo kali sana kama 'Mikasi', 'Ghetto langu', 'A.K.A Mimi', 'Mademu wangu', n.k
*****CINDERELA' ya Alikiba, Nilikuwa sipendi kabisa hawa watu wanaitwa 'wabana pua', ila kwa mara ya kwanza nikavutiwa, nikanunua album ya huyu jamaa, na ndio ikawa mwisho wangu wa kununua album, ilikuwa moja ya album nzuri sana, ina nyimbo nyingi na zote zinasikilizika, nyimbo kama 'Cinderella','Nalia', 'Njiwa', 'Nakshinakshi', 'makmuga', na nyingine nyingi nilizipenda sana though sahivi mimi ni team Diamond . Album nyingine kali kwa hawa wasanii wa kuimba ni ya Banana Zoro 'MAMA', kama hujawahi kusikiliza itafute hutajuta ina madude makali mno though ilikuwa underrated, haikuwa maarufu kama SAUTI YA DHAHABU ya TID, sikuinunua ila kuna mshkaji wangu alikuwa nayo.
******.
NB: Sio kwamba album zote ambazo sijazinunua hazikuwa Kali, ni vile tu tatizo na kifedha lilinilazimu kuwa selective sana, ni Profesa Jay pakeyake ambaye nna album zake zote, wengine nilikuwa nachagua sana, na album nyingine nilikuwa nasikiliza kwa washkaji mfano album ya Ugali ya Nature ilisambaa sana kitaa, so sikuona haja ya kuinunua. Kiukweli nimemiss zama zile za album zilikuwa na raha yake. Sio sahivi wimbo mbovu, video kali, kiki kwa wingi. Kwa upande wako ni Album ipi umewahi kununua? Ni ipi album yako kali zaidi kwenye bongofleva?
*Album za wasanii wa mwanzoni kama Sugu nilikuwa nazisikiliza kwa mabraza, nikitembelea kwa mabro unakutana na album kama 'Ndani ya Bongo', 'Nje ya Bongo', 'Deiwaka', n.k na kwa Mara ya kwanza nikavutiwa kuupenda huu muziki wa 'kufokafoka', nakumbuka kipindi hicho nilikuwa mtoto wa primary.
**MACHOZI JASHO NA DAMU' ya Profesa Jay, hii Album nakumbuka nilimpiga sound Maza hadi akaninunulia. Ni bonge moja la Album, moja kati ya album bora kupata kutokea kwenye bongofleva yenye nyimbo kama Ndiyo Mzee, Bongo Dar es salaam, Niamini, Jina Langu, Tathmini, n.k
***ULIMWENGU NDIO MAMA' ya Jay Moe, hii nakumbuka nilikuwa form1 Sengerema Sec (boarding), kwa Mara ya kwanza nilitoa hela yangu mfukoni (pocket money) na kuinunua. Kwangu mimi hii ni Album bora kabisa kupata kutokea kwenye Bongo Hiphop, hakuna wimbo wa kuforward mule, utakutana na ngoma kama 'Bishoo', 'Kama Unataka dem', 'Majukumu', 'Maisha ya Boarding', 'Mvua na Jua' na nyingine nyingi. Ukitaka kumjua JayMo huyu ndio alikuwa JayMo wa kweli alikuwa anaandika hasa, sio huyu wa sasa wa 'Pesa ya Madafu', 'Tunakula Bata', huyu wa sasa simuelewi kabisaa, ila ndio hivyo siwezi mlaumu sana maana ni lazima aswitch aendane na hiki kizazi cha 'Instagram'.
****A.K.A MIMI ya Mangwea, huwezi taja album 5 bora za wakati wote kwenye list yako ukaiacha hii album utakuwa na matatizo. Ni moja ya album niliyotoa hela yangu mfukoni na kuinunua, ina nyimbo kali sana kama 'Mikasi', 'Ghetto langu', 'A.K.A Mimi', 'Mademu wangu', n.k
*****CINDERELA' ya Alikiba, Nilikuwa sipendi kabisa hawa watu wanaitwa 'wabana pua', ila kwa mara ya kwanza nikavutiwa, nikanunua album ya huyu jamaa, na ndio ikawa mwisho wangu wa kununua album, ilikuwa moja ya album nzuri sana, ina nyimbo nyingi na zote zinasikilizika, nyimbo kama 'Cinderella','Nalia', 'Njiwa', 'Nakshinakshi', 'makmuga', na nyingine nyingi nilizipenda sana though sahivi mimi ni team Diamond . Album nyingine kali kwa hawa wasanii wa kuimba ni ya Banana Zoro 'MAMA', kama hujawahi kusikiliza itafute hutajuta ina madude makali mno though ilikuwa underrated, haikuwa maarufu kama SAUTI YA DHAHABU ya TID, sikuinunua ila kuna mshkaji wangu alikuwa nayo.
******.
NB: Sio kwamba album zote ambazo sijazinunua hazikuwa Kali, ni vile tu tatizo na kifedha lilinilazimu kuwa selective sana, ni Profesa Jay pakeyake ambaye nna album zake zote, wengine nilikuwa nachagua sana, na album nyingine nilikuwa nasikiliza kwa washkaji mfano album ya Ugali ya Nature ilisambaa sana kitaa, so sikuona haja ya kuinunua. Kiukweli nimemiss zama zile za album zilikuwa na raha yake. Sio sahivi wimbo mbovu, video kali, kiki kwa wingi. Kwa upande wako ni Album ipi umewahi kununua? Ni ipi album yako kali zaidi kwenye bongofleva?