Tukizingatia Exchange, deni la taifa ilibidi lipungue

Tukizingatia Exchange, deni la taifa ilibidi lipungue

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
457
Reaction score
773
Deni la Taifa kwa sasa limepanda kutoka Trilioni 108 mwezi Mei hadi trilioni 116 Mwezi Agost. Hili ni ongezeko la 7.41% ndani ya kipindi cha miezi miwili tu. Deni hili linaweza kunasibishwa na taarifa kuwa exchange rate imezingua, lakini ieleweke kuwa thamani ya shilingi imeimarika kuanzia mwezi wa nane mwanzoni.
Graph.png


Mwezi wa tano, shilingi ya kitanzania ilifikia kuwa 2686 kwa dola moja ya Marekani ambapo hadi sasa shilingi imepanda thamani hadi kufikia 2458 mwanzoni mwa mwezi Agost.

Niiweke hii sawa, yaani kama tulikuwa tunadaiwa dola 100 mwezi wa mei maana yake tulikuwa tunadaiwa Tsh 268,600. Ikiwa hatujaongeza hela ya kukopa na tukabaki na deni hilo hilo la dola 100 mwezi august deni kwa shilingi lingekuwa Tsh 245,800. Yaani lingepungua kutokana na kupanda kwa thamani ya shilingi.

Hata kama tutaweka riba kwenye deni, haingewezekana kwamba deni liwe linapanda kwa 7% kwa miezi michache. Hii ni kusema kuwa kuna hela nyingi zimekopwa kwa kipindi cha miezi miwili, huku bunge likiwa halipo kuidhinisha matumizi ya fedha.

Nawasilisha.

Pia soma >> Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116
 
Kwa sasa wahuni wanatupiga sana kwenye deni kuna uzi nilianzisha nikilalamikia namna deni la taifa linavyotumika kuhujumu ila watu wakanijia juu.
 
Na rasilmali za nchi zinaendelea kupungua population ikiongezeka ni hatari
 
Na rasilmali za nchi zinaendelea kupungua population ikiongezeka ni hatari
 
Deni la Taifa kwa sasa limepanda kutoka Trilioni 108 mwezi Mei hadi trilioni 116 Mwezi Agost. Hili ni ongezeko la 7.41% ndani ya kipindi cha miezi miwili tu. Deni hili linaweza kunasibishwa na taarifa kuwa exchange rate imezingua, lakini ieleweke kuwa thamani ya shilingi imeimarika kuanzia mwezi wa nane mwanzoni.
View attachment 3452509

Mwezi wa tano, shilingi ya kitanzania ilifikia kuwa 2686 kwa dola moja ya Marekani ambapo hadi sasa shilingi imepanda thamani hadi kufikia 2458 mwanzoni mwa mwezi Agost.

Niiweke hii sawa, yaani kama tulikuwa tunadaiwa dola 100 mwezi wa mei maana yake tulikuwa tunadaiwa Tsh 268,600. Ikiwa hatujaongeza hela ya kukopa na tukabaki na deni hilo hilo la dola 100 mwezi august deni kwa shilingi lingekuwa Tsh 245,800. Yaani lingepungua kutokana na kupanda kwa thamani ya shilingi.

Hata kama tutaweka riba kwenye deni, haingewezekana kwamba deni liwe linapanda kwa 7% kwa miezi michache. Hii ni kusema kuwa kuna hela nyingi zimekopwa kwa kipindi cha miezi miwili, huku bunge likiwa halipo kuidhinisha matumizi ya fedha.

Nawasilisha.

Pia soma >> Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116
Mama anatorosha pesa uarabuni ... Mali za tanganyika zinateketea kwa kuuzwa....tenda za umma zote anawapa ndugu zake akina mwinyi kikwete rostam mifumo haina kazi kwake huyu bibi.....amefanya taasisi ziogope kufanyakazi
 
Deni la Taifa kwa sasa limepanda kutoka Trilioni 108 mwezi Mei hadi trilioni 116 Mwezi Agost. Hili ni ongezeko la 7.41% ndani ya kipindi cha miezi miwili tu. Deni hili linaweza kunasibishwa na taarifa kuwa exchange rate imezingua, lakini ieleweke kuwa thamani ya shilingi imeimarika kuanzia mwezi wa nane mwanzoni.
View attachment 3452509

Mwezi wa tano, shilingi ya kitanzania ilifikia kuwa 2686 kwa dola moja ya Marekani ambapo hadi sasa shilingi imepanda thamani hadi kufikia 2458 mwanzoni mwa mwezi Agost.

Niiweke hii sawa, yaani kama tulikuwa tunadaiwa dola 100 mwezi wa mei maana yake tulikuwa tunadaiwa Tsh 268,600. Ikiwa hatujaongeza hela ya kukopa na tukabaki na deni hilo hilo la dola 100 mwezi august deni kwa shilingi lingekuwa Tsh 245,800. Yaani lingepungua kutokana na kupanda kwa thamani ya shilingi.

Hata kama tutaweka riba kwenye deni, haingewezekana kwamba deni liwe linapanda kwa 7% kwa miezi michache. Hii ni kusema kuwa kuna hela nyingi zimekopwa kwa kipindi cha miezi miwili, huku bunge likiwa halipo kuidhinisha matumizi ya fedha.

Nawasilisha.

Pia soma >> Tanzania: Deni la Taifa lafikia trilion 116
Mpaka October litakuwa Trillion 130 maana wanakopa fedha bila kuzitumia ipasavyo,wanaziiba na kuzificha huko huko nje.
Matumizi hewa yanazidi tunachokusanya.Huu ni Mto hauwezi kutunza maji.
 
Wahuni washapiga hizo Trilioni 8! Na mpaka waondoke madarakani Tanganyika itakuwa inazadiwa zaidi ya Trilioni 450!
 
Back
Top Bottom