Tukiacha unafiki, hadi leo utawala huu umeifanyia nini Tanzania?! Umewasaidia nini watanzania!?

kila siku naamini wewe ni mjinga.
haya uliyoandika yapo dar tena muhimbili tu.tanzania ni kubwa na nina uhakika weww hata kibaha hujawahi kulala.
umeambiwa taja mambo yaliyofanyika unataja mlonganzila? huna aibu? ilianza kujengwa lini? huna aibu yule mkuu wa wilaya ya muheza alikuwa anazungusha bakuli juzi la nini? wilaya nzima ya muheza ina kituo cha afya kimoja. kuwa na aibu wewe kuna hospitali za wilaya hata mortuary hazina mfano mafia. kuwa na aibu mkuu upatikanaji wa dawa uko wapi mbona maduka ya dawa yanazidi kuongezeka nje ya hizo hospital zenu? kuwa na aibu juzi nilimpeleka kijana wangu hoapital lugalo usiku nikauziwa dicloper kwenye mkoba hizo dawa ziko wapi? kituo cha afya sinza hakina hata standby generator sasa hata kama kimepandishwa hadhi yasaidia nini?
saa nyingine ficha usaha wako kichwani mkuu.
 
kata
VIWANDA:
Hadi sasa ni viwanda zaidi ya 3000 vimeanza kazi
Haipiti Mwezi Magufuli lazima apite mkoa flani kuzindua kiwanda...
Kama una muda pita SIDO wakakupe takwimu za viwanda vidogovidogo na uhitaji wa mashine mbalimbali.
karakana unaita kiwanda .kama kuna viwanda mbona hatuuzi nje sasa? mbona watu hawaajiriwi vijana wanashinda kwenye betting centres
 
um
umeongeza VAT wazungu hawaji wanaenda kwingine mwaka jana kwenye season watalii zaidi ya 8000 walikatisha safar zao. unajua mtalii mmoja angeingiza pesa za kigeni shiling ngapi? wewe jitekenye tu
 
Kwenye afya ni bora ungekaa kimya. Kwasababu Mosi, umeaacha kuzungumzia mambo ya maana kama Maternal morality, perinatal death na infant mortality badala yake unaabdika none sense hapa.
Pili, Uhaba wa vifaa tiba bado ni tatizo katika vituo vya afya na hospital za serikali, si ajabu kukosa vitu vidogovidogo kama syringes na gloves
Tatu, Vituo vya afya na hospitali za serikali ukiachilia mbali uhaba wa wauguzi na madaktari bado hata wengi waliopo hawana mafunzo toshelevu au mafunzo stahiki. Wengi ni wababaishaji kwa sababu wamewekwa kwenye nafasi ambazo hawakustahili, wanatumia trial and error. Kwa mfano ukiangalia Mtaala wa uuguzi, Muuguzi wa cheti (enrolled nurse) hufundishwa kumanage normal labour peke yake, abnormal labour tunawafundisha kumuandaa mama kwa referral. Sasa maajabu ya serikali inawaajiri hawa na inawapeleka hospitali za mikoa na shift anaingia yeye na medical attendant (ambaye si nurse)! Halafu mnataka eti muujiza utokee maternal deaths zipungue!!
Nne, Nurse patient ratio na doctor patient ratio ni kubwa mno! Mimi ninashangaa kwa nini wauguzi bado wanaendelea na kazi, sijui ni umasikini wao na familia zao. Nimebahatika kutembealea na kufanya kazi katika hospitali, vyuo na vituo vya afya tofauti tofauti, miongoni mwao vipo vya serikali na vya kanisa. Nilichojifunza ni kwamba matatizo ya vituo vya afya na hospitali za serikali yanafanana kote. Katika kituo kimoja nilikuta kazi wanazofanya manesi wanne na medical attendant wawili hospitali nilotoka, wao atafanya nurse mmoja au wawili!!! Kwa nini watu wasife??
Tano, sababu ya baadhi ya referrals ni za ajabu. Ati mama anakuwa reffered kwenda hospitali ya wilaya kisa ultrasound!!! Yaani unampandisha mama kwenye ambulance hadi hospitali ya wilaya kisa ultrasound!! Mmeweza kununua ambulance lakini kipimo kama ultrasound mmeshindwa hadi muingize siasa!!!
Sita, ile mishahara kuanzia Medical doctor hadi enrolled nurse inasikitisha! Ninashangaa kwa nini bado wanaendelea na kazi na wako comfortable kabisa.
Mwisho, ingawa serikali hii imeonyesha madhaifu mengi lakini kuna baadhi ya mazuri mh magufuli anastahili pongezi kwa upande wa kudhibiti upiga dili MSD na idara zingine.
Mwisho kabisa. Serikali haijawa serious na afya za watanzania thus why wao wanaenda India, ujerumani, Nairobi, South Africa, Ubelgiji na kwingine.
 
asante. umemaliza mkuu. kuna watu humu wanadhani tanzania ni dar tu.
 
Tatizo wengi tumekalia ushabiki na siasa za zilizo pitwa na wakati badala ya kuwa wakweli. Huyu kiongozi tutamwelewa tu.. Tumpe nafasi... Mabadiliko chamya hayaji siku moja. Tembeleeni nchi nyingine ( hasa majirani) kisha ndo mtajua tulipo na tunapo elekea.
 
Imeruhusu wanyonge kuuza bidhaa katikati ya barabara wakati mwenye gari ukipaki kushusha mtu 30000 inakuhusu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…