Tukiacha kuhonga hakuna mwanamke atadanga

Tukiacha kuhonga hakuna mwanamke atadanga

Mkiacha kuwahonga wanawake mtashtukia nyie wanaume ndo mnahongwa na mtaanza kudanga. Hii kitu inaambukiza shauri lenu..

Msije kusema hamkuambiwa
Huyu anatutisha na hakuna kutishika . Mwanaume haogopi chochote.

Kauli ni moja hakuna kuwa honga ili wakae kwenye reli
 
Kuna mama ni fundi nguo mpaka sasa ana nyumba mbili

Ila wadangaji wengine kwasasa wanatumia dawa za kienyeji,tuweni makini
 
Vyoyote mtakavyo kubaliana Binafsi Mimi sitaacha kuonga
 
Wakuu

Nimetafakari sana , wanawake wana danga sana kutokana na sisi wanaume na wavulana kuhonga honga hovyo wanawake, unakuta kijana anapigika anapata kakipato kiduchu kama posho ya kibarua kwa siku ila ana honga asilimia 99% ya kipato chake kwa mwanamke kwa kuhofia kumpoteza .

Kijana yupo teyari kukaa njaa ili mradi tuu mpenzi wake akimuomba hela ampe, na hawa mabinti wamejua wazi kabisa kuwa tuna wahonga hela ndiyo maana kila siku wanazidi kuongezeka mitaani kudanga na kusaka wa hongaji.

Binti ana danga mtaa mmoja hadi mwingine kujitafutia fursa za wanaume wepesi wanao wabatiza kwa mihela badala ya kutulia na kutafakari mambo mengine ya muhimu ya kike yenye manufaa kwao


Mabinti wanasema kabisa huu mtaa una wanaume bahili ngoja nikatembee mtaa mwingine shida ipo kubwa sana hapa wanaume , sisi ndiyo source ya kuwafanya wadange .

Ili kuwazibiti mabinti / wanawake watulie kwenye ndoa zao / wawe na maadili na shauri tuache kuwa honga kabisa na hakuna kutoa hela yeyote kwao na kwa namna yeyote ile.

Pia na shauri kwa wazazi ukiona binti yako anamiliki kitu cha thamani , kasuka , kavaa mavazi au urembo wowote wa thamani nje na hela unazo mpatia mbane na akuambie amezipata wapi na ingali bado hajaolewa mbane haswa na hakuna mchezo kwa hili


Pia sisi wanaume / wavulana fedha tunazo tumia kuwa honga hawa mabinti tuziwekeze kujenga uchumi wetu imara kwaajili ya sasa na baadaye, mwanamke kama anakutaka usimuhonge mchukue muweke ndani na kama ni mpenzi wa pisi mbili tatu pia fanya hivyo na hakuna kuhonga kabisa,

Nawatakia jumapili njema.
Umeongea point kubwa na umenigusa kiufupi,mimi kuna demu mkali kinoma alinipenda sana yaani ila kabla sijatia neno tu zee moja likamuonga prado na ujenzi juu mpaka leo tulitawanyika ila mtoto akiniona tu anabadilika kabisa mpaka nilipohama mkoa still insta ananifuatilia kinoma ingawa hatujafolowliana ,wanaume tuache kuhonga huyu angekuwa wangu kabisa
 
Binafsi nachukulia ngono Kama starehe ya watu. Wa hali ya chini so kwangu ngono siwezi kuitengea bajeti nikaacha kunywa Jack Daniel ,Nyama ya mbuzi n.k nianze kuangaika na wanawake hiyo siwezi big no Mimi friji lazima likae full Nyama full foili yaani starehe zangu hazimuhusishi Mwanamke.
 
Labda vichwa vya chini visifanye kazi ndio wataacha kuhonga.
 
Labda vichwa vya chini visifanye kazi ndio wataacha kuhonga.
 
Haitatokea,Mimi mpaka leo namuhonga shemeji yenu na nimemuoa kabisaa,hawa wenzetu wameumbwa kupokea akikupa jua ni Mtego Au upendo kazi kwako kumbuka ya Adam na hawa.

Mhonge tu huna namna mzee,
 
Majuzi Kariakoo nikawa nanunua muhindi wa kuchoma kwa kijana wa Kiha (hawa jamaa kutoka Kigoma) wakati anaendelea kuuandaa vizuri nashangaa nae anaongea na simu biashara za kutumiana hela na mwanamke.

Nikamuuliza na hali yako hii dogo unahonga akaniambia “blaza huo ndiyo uanaume” niliishia tu kucheka maana yeye mwenyewe maisha yake mabovu but still anajipa mzigo hawa vijana ni wa kuhurumiwa.
Ulikosea sana. Wanaonekana hivyo kwa hali ya kazi yao. Alivaa suti huwezi kununua mahindi yake. Lakini jiulize. Auze mahindi 30. Kila hindi anapata 500. Kwa siku 15,000. Chakula anatafuna kipande cha muhimu wake na maji. Siku inapita. Ukiwa mwezi atabaki na ngapi? Kwa mwaka je?
 
Majuzi Kariakoo nikawa nanunua muhindi wa kuchoma kwa kijana wa Kiha (hawa jamaa kutoka Kigoma) wakati anaendelea kuuandaa vizuri nashangaa nae anaongea na simu biashara za kutumiana hela na mwanamke.

Nikamuuliza na hali yako hii dogo unahonga akaniambia “blaza huo ndiyo uanaume” niliishia tu kucheka maana yeye mwenyewe maisha yake mabovu but still anajipa mzigo hawa vijana ni wa kuhurumiwa.
Unakosea sana. Wanaonekana hivyo kwa hali ya kazi yao. Akivaa suti huwezi kununua mahindi yake. Lakini jiulize. Auze mahindi 30. Kila hindi anapata 500. Kwa siku 15,000. Chakula anatafuna kipande cha muhimu wake na maji. Siku inapita. Ukiwa mwezi atabaki na ngapi? Kwa mwaka je?
 
Mkiacha kuwahonga wanawake mtashtukia nyie wanaume ndo mnahongwa na mtaanza kudanga. Hii kitu inaambukiza shauri lenu..

Msije kusema hamkuambiwa
mbna wanahongwa na wanadanga pia? Au wahongwe na kudanga mara ngapii??
 
Back
Top Bottom