Tukatae ongezeko la matumizi ya utawala; Ni Juu ya pendekezo la CCM la kuanzishwa kwa SENETI

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
[h=2][/h]Ijumaa, Agosti 17, 2012 10:03 Na Balinagwe Mwambungu


IMERIPOTIWA kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinapendekeza kuanzishwa kwa Baraza la Seneti ambali litakuwa na marais wastaafu na wajumbe wengine wa kuchaguliwa. Taarifa hio zikiwanukuu baadhi ya wanumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Halmshauri Kuu (NEC) ya CCM, zilieleza kwamba imependekezwa kwamaba mfumo wa sasa wa Bunge ‘ufumuliwe’ na badala yake kuwe na Mabaraza Mawili—Bunge na Seneti.

Sababu ya kutaka kulifumua Bunge, hazikuelezwa na sababu za kutaka liwepo Baraza la Seneti hazina mashiko. Inaelezwa kwamba siku za usoni taifa litakuwa na marais wengi wastaafu, hivyo liundiwe Baraza la Seneti, ambamo wataingia kwa kuwa walikuwa marais, lakini pia inapendekezwa kwamba watachakuwamo wajumbe wengine wa kuchaguliwa.

Inaelezwa kwamba nchi kuwa na mabaraza mawili si jambo jambo geni na inatolewa mfano wa Marekani na Uingereza—ambako kuna Baraza la Wawakilishi (House of Representatives) na Senate—na Uingereza ambako kuna House of Commons na House of Lords. Mfumo huu haukubuniwa kwa sababu ya kutaka kukidhi matakwa ya kundi fulani, bali imetokana na historia ya nchi hizo.

Lakini si nchi hizo mbili zenye mfumo huu wa kuwa na mabunge mawili. Nigeria ina Baraza la Seneti, India ina mabaraza mawili ukiachia mbali mabunge ya majimbo. Kuundwa kwa mabaraza hayo kulitokana na sababu maalumu zilizosabisha kuwapo kwa mabaraza hayo.

Tuchukue mfano wa Marekani ili kuelezea dhana ya mabaraza mawili vizuri. Baraza la Wawakishi mara nyingine huitwa Congress, wajumbe wake huchaguliwa kutoka kila jimbo kufuatana na wingi wa watu. Hawa huchaguliwa kila baada ya miaka miwili (mid-term elections).

Kwahiyo, jimbo moja lenye watu wengi linaweza likawa na wawakilishi zaidi ya mmoja. Jimbo la California ndilo lenye watu wengi zaidi na lina Wawakilishi 53, kati ya wawakilishi 435. Na Baraza la Seneti (Upper House), lina maseneta 100, wawiwili kutoka kila jimbo (state) wanatumikia kwa muda wa miaka sita. Marekani ina jumla ya majimbo 48.

Kwa upande wa Uingereza, kutokana na historia yake kwamba ilitawaliwa kifalme, kulitokea mapinduzi na makabwela (common people) wakaunda Bunge lao (House of Commons) watawala wakabaki na Bunge na House of Lords. Wajumbe wake ni wateule wa kifalme.

Ni sababu zipi ambazo CCM wanataka kujenga mabaraza ya kitabaka ambayo nchi yetu ilikwisha yakataa kabla na baada ya uhuru? Kwamba kutakuwa na marais wengi wastaafu kwahiyo tuwaundie baraza, hapana. Tukitaka kupunguza idadi ya marais wastaafu, ama tuongeze umri si kupunguza, kama kigezo cha mtu kugombea urais ili kupunguza gharama za marais wastaafu au tuongeze muda wa kushika madaraka—badala ya miaka mitano, tufanye minane (8), ili kumpa muda wa kutosha kutekeleza aliyokusudia kufanya, hata kama atakuwa rais wa muhula mmoja.

Kwanza, katika mfumo wa sasa wa vyama vingi, tukiwapeleka marais wastaafu bungeni, wataumbuka. Maseneta wenzao watawabwatukia na kuwakosoa kutokana na mambo ambayo hawakuyasimamia vizuri. Hadhi ya urais itakuwa wapi? Tukifanya hivyo tutakuwa hatuwatendei haki. CCM walisema wanakusudia kuwaengua marais wastaafu na kuwaundia Baraza la Ushauri la CCM, hapana shaka wameona kuwa ni kuongeza gharama, sasa wanataka gharama hizi wazibebe walipa kodi. Hapana.

Itakuwa busara kama itaamuliwa kwamba tuwe na mabaraza matatu—Baraza la Wawakilishi (Zanzibar), Bunge la Tanganyika na Bunge la Muungano ambalo litakuwa na idadi ndogo wa wawakilishi—mmoja kutoka kila mkoa na watashughulikia mambo ya Muungano tu.

Viongozi wastaafu, wako juu ya Bunge au Baraza la Wawakilishii. Rais yeyote, ikiwa anataka, anaweza kuomba ushauri juu ya jambo lolote kutoka kwa viongozi wastaafu kuanzia wakuu wa wilaya, mikoa, mawaziri, mawaziri wakuu na marais na sio kuwaundia baraza maalumu.

Dhana ya kutaka Katiba mpya itamke idadi ya Wabunge ni njema, lakini pia itamke idadi ya Wizara, ili rais asiweze kuwapa vyeo marafiki, kama ilivyotokea kwa wanamtandao.

Katiba vile vile itamke kipindi cha uongozi wa kitaifa, lakini isimzuie mwakilishi wa wananchi kuchaguliwa tena na tena kama kazi yake ni nzuri na ikiwa wananchi waliomchagua, wanaona bado anafaa kuwa mwakilishi wao.

Kutamka kipindi cha ubunge, ni kuwanyang’anya wananchi haki yao ya kumchagua mwakilishi wanaye mpenda. Na kama Bunge kila mara linakuwa na kuwa wabunge wengi wapya halinogi, kwa sababu wabunge wapya kwa kipindi fulani, watakuwa wanajifunza kutoka kwa wabunge wakongwe.

Katiba pia isitamke umri wa mgombea ubunge au uwakilishi, kwa kuwa miaka ya mtu kupiga kura ni 18, lakini iweke ukomo wa umri wa wawakilishi wetu nchi za nje. Katika vipindi viwili tumeshuhudia watu waliostaafu utumishi kutokana na umri, wanateuliwa kuwa mabalozi wetu nchi za nje. Lakini itapendeza pia kama Katiba itambana rais na kutamka kwamba idadi ya mabalozi wanasiasa, iwe ni nusu ya watumishi kutoka serikalini.

Aidha, Katiba mpya pia itamke kwamba wakuu wa majeshi na vyombo vya Ulinzi na Usalama, majaji wastaafu, hawataruhusiwa kugombea urais. Wakitaka kugombea wafanye hivyo kabla ya kustaafu kwa maana ya kwamba itabidi wajiudhuru nyadhifa zao.

Katiba mpya itamke uwepo wa majimbo (hivi sasa mikoa) ambao yataongozwa na magavana wa kuchaguliwa. Hawa watabuni mipango ya maendeleo ya majimbo yao, watasimamia utawala na watakuwa na Mamlaka ya Kodi (TRA) itakusanya kodi ya mkoa. Hazina Kuu itakuwa inagawiwa sehemu ya mapato toka kila mkoa kutokana na ukubwa wa mapato. Katiba mpya iwe ufunguo wa maendeleo ya wananchi badala ya kuwakikwazo. Hivi sasa sehemu kubwa ya fedha inayohitajiwa kwa ajili ya maendeleo, inatoka Hazina. Tujifunze toka India.

Katiba mpya itamke kutakuwa na aina moja tu ya uwakilishi—uwakilishi wa kuchaguliwa. Hii itakuwa imefuta ubaguzi wa kijinsia—kuipendelea jinsia moja kwa kuipa nafasi maalumu.

Katiba itamke rasmi kwamba uchaguzi wowote, katika ngazi zote, ikiwa ni pamoja na ule wa rais, unaweza kupingwa mahakamani, isipokuwa uwekewe utaratibu maalumu kuepusha nchi kuingia katika mgogoro wa muda mrefu.

Hitimisho. Viongozi wetu wasiendelee kuigawa nchi katika vipandevipande kwa kukidhi matakawa ya kisiasa. Sehemu kubwa ya bajeti yetu—takriban asilimia-----inatumikakwa mambo ya utawala na asilimia……tu ndio bajeti ya maendeleo. Wakati umefika sasa kufanya mageuzi ya……

na kuubadili mfumo wa sasa, ili nchi yetu ipate kusonga mbele kiuchumi, kijamii na kimaendeleo. Tuondokane na mfumo unaowatumikisha wananchi, tuingie katika mfumo unaowatumikia wananchi. Tutapiga hatua kubwa mbele.

 
CCM Inatafuta kila Njia ya kuwapa Ulaji Viongozi wao Wastaafu kama ikitokea CCM imepoteza NGUVU za kutawala Tanganyika na Zanzibar
 
Duh!Mpaka nimechoka,mimi nafikiri wanapendekeza kumpunguzia mdanganyika umaskini kumbe wanazidi kumuongezea umaskini,wadanganyika kazi bado tunayo.
 
Duh!Mpaka nimechoka,mimi nafikiri wanapendekeza kumpunguzia mdanganyika umaskini kumbe wanazidi kumuongezea umaskini,wadanganyika kazi bado tunayo.

Hawa magamba kwa kweli wanastaajabisha sana. Kila siku inapokuja mambo ya msingi kama kuongeza mishahara na marupurupu kwa Wafanyakazi wanadai Serikali haina uwezo lakini kila kukicha wanakuja na sera fisadi za kuongeza gharama za uendeshaji ambazo hazina maana yoyote kama vile kuongeza idadi ya mikoa, wilaya, wabunge. Sasa wanataka kuongeza tena kuwepo kwa seneti ambalo hata kazi yake sijui itakuwa zipi zaidi ya kuongeza urasimu ambao tayari uko wa kutisha.

Bunge lililopo limekuwa hohehahe kiasi cha Wabunge kujihusisha na upokeaji wa rushwa badala ya kuwakilisha Watanzania na hivyo kuwaletea maendeleo wale wanaowawakilisha. Halafu tukiwasema vibaya hapa jamvini wanapandisha mori kumbe wanajitakia wenyewe na madudu yasiyokwisha!!!
 
CCM wanataka kuishi kama wachina na warussi ktk kujenga nchi kichama zaidi ya kiuchumi. waliisha wahi kuunda selikali ya chama ndani ya nchi na kuleta msemo chama chashika hatamu.kumbuka wakati ule katibu mkuu wa ccm alikuwa na nguvu zaidi ya waziri mkuu. ule ulikuwa ni ulaji tuu wa wansiasa wasiojua kujenga uchumi bali wao wanajua kulaghai umma na kuimarisha chama.

Leo hii wapo palepale pa kuchezea pesa za nchi, eti kuunda balaza la seneti na maraisi wastaafu wawemo. yaani hawafikilii kabisaa kujenga vyoo vya kuvuta kwa shule za msingi zote bara na visiwani. hawafikirii kabisaa kujengwa mabwawa ya kuogolea katika manispaa zote tanzania. hawafikilii kabisaa kujenga huduma za maktaba katika ngazi ya kata bara na visiwani. hawana mawazo ya kupanua viwanja vya michezo ya watoto.

kumbuka ndio hawahawa walioleta SUKITA. Jiulize sukita imekufa kwa ajili gani na iliacha deni la shilingi ngapi la umeme!Uruusi na china wana wese na wapo mbali kimapato, ndio maana wanweka mbalaza ya seneti. leo hii sweedn haipo kutusaidia, hizo ghalama atakuwa anlipaga nani?

CCM acha utani, tafuta ma investors waje kuleta ajira na uje jivunia kuwa unatwala watu wengi walio na kazi na sio wasio na kazi kama kule songea na maswa.
 
Hawa magamba kwa kweli wanastaajabisha sana. Kila siku inapokuja mambo ya msingi kama kuongeza mishahara na marupurupu kwa Wafanyakazi wanadai Serikali haina uwezo lakini kila kukicha wanakuja na sera fisadi za kuongeza gharama za uendeshaji ambazo hazina maana yoyote kama vile kuongeza idadi ya mikoa, wilaya, wabunge. Sasa wanataka kuongeza tena kuwepo kwa seneti ambalo hata kazi yake sijui itakuwa zipi zaidi ya kuongeza urasimu ambao tayari uko wa kutisha.

Bunge lililopo limekuwa hohehahe kiasi cha Wabunge kujihusisha na upokeaji wa rushwa badala ya kuwakilisha Watanzania na hivyo kuwaletea maendeleo wale wanaowawakilisha. Halafu tukiwasema vibaya hapa jamvini wanapandisha mori kumbe wanajitakia wenyewe na madudu yasiyokwisha!!!
wakomunisti, wajamaa na wasosialist, hawajali raia zao bali kuimalisha chama.kumbuka hata kawawa aliwahi kusema kuwa ni vizuri kiongozi wa chama akachekiwe afya yake ulaya mara moja kwa mwaka wakati huo huo shule zote za msingi dar hazina madesk.Kumbuka mkurugenzi mkuu wa Tanzania filamu aliwahi kupendekeza kupiga marufuku sinema zote za west na kutaka tuwe tunaagiza sinema za kirusi tuu. Yaani nakuonesha kwa jinsi gani wanasiasa wetu walivyokuwa hawajali iinterrest za watu wao wnaowatawala
na kuziboresha bali kuleta maudhi tuu. leo hii hawafikirii umuhimu wa kuwa na mahakama kuu huru wanataka mpaka matokeo ya uchaguzi yawauwe watu ndipo wataona umuhimu wa mahakama kuu kuwa huru.

Nilidhania wangesema wanataka Takuru(PCCB) iwe huru na mkuu wake apigiwe kura bungeni au mahakama kuu iwe huru na isiwe chini ya raisi au cheo cha waziri wa mambo ya nje,ulinzi na wa fedha kipigiwe kura na bunge. Unaona jinsi mambo ya kumboreshea raia maisha yake yanavyokwepwa na wajamaa wetu?
 
Wizi ndani ya wizi. JK anatafuta ajira baada ya kuachia ngazi kama siyo sehemu ya kuponea ashitakiwe na wenzake kutokana na madudu waliyofanya kwa watanzania. Ukichunguza sakata la Loliondo na IPTL Ali Hassan Mwinyi haponi. Ukichunguza NBC na EPA Mkapa haponi. Ukichunguza kashfa ya Richmond na hata EPA Kikwete haruki. Ukienda kwenye kashfa ya bendera yetu kutumiwa na meli za Iran Zanzibar kutawaka moto. Tanzania imegeuzwa shamba la bibi kipofu huku kila jambazi akijitafutia ulaji kwa kutumia kila nafasi aliyopewa. Shame on them all!
 
Wazo la seneti siyo baya kwani wengi tumeshuhudia maamuzi mabovu yanayofanywa na bunge ambayo yamejaa ushabiki bila kuzingatia maslahi ya nchi na wakati mwingine yamekuwa yanazingatia zaid maslahiya chama ili kulinda serikali lakini nachopinga ni kuhusu muundo wa seneti kuhusisha viongozi wastaafu kwanza wengi wa viongozi wastaafu ndio waliosababisha uozo mkubwa wa nchi hii badala ya kulinda maslahi ya nchi watakuwa wanalinda maslahi yao binafsi mfano tuna watu kama profesa Shivji ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitetea kuhusu ardhi ya Tanzania tukiwa na watu wenye uchungu na nchi kwenye baraza hilo bunge litaacha kupitisha maamuzi ya ovyoovyo kama kujipangia posho kubwa ambazo haziendani na hali halisi ya nchi yetu
 
Badala ya kupinga moja kwa moja ni bora uka toa mbadala wa mawazo yao na co kutangaza vita ya kuwapinga
 
Chadema, Sera yenu ya majimbo inatekwa kama ya katiba.
Marais wastaafu ni watumishi wa umma wanatakiwa wakae na wajukuu zao. Kama hawakuweza wakiwa na nguvu hawawezi wakiwa na mikogojo.
Hivi Rais mstaafu mwizi anayewezaje kuushauri umma kuhusu wizi ikiwa yeye hana maadili ya kiroho 'moral authority'
Swali linarudi mambo ya muungano ni yapi?
 
Tutumie rasilimali zetu kuondoa Ujinga, Umasikini na Maradhi ambao ndio maadui zetu wakubwa. Miaka 50 ya Uhuru Elimu inashuka, Hospitali hakuna dawa, Wananchi umasikini unazidi. CCM na Serkali yake isaidie ya kuinua hali za Mtanzania vinginevyo watakuwa kama KANU au UNIP 2015.
 
Mwarobaini wa hili jambo ni Katiba Mpya ijayo kama haitachakachuliwa! (Naikumbuka "White paper" ya Mkapa ilivyochakachuliwa na kilichomsibu yule Jaji)
 
marais wastaafu ni wengine au ni hawa tunaao wajuwa kwa mambao yao...kagoda uswis nguzo za iringa nk
 
Mwinyi mzenji, soon watajitenga na tutamuondoa nchini. Huyu mwingine mchaafu sana, ana pesa Uswizi na alimuua baba wa taifa! Upuuzi huu
 
Back
Top Bottom