Tujuzeni kinachoendelea Zanzibar

Tujuzeni kinachoendelea Zanzibar

Mliweka mpira kwapani leo mnajipendekeza un nyambafu mwacheni shein apige kazi nchi imetulia sana

Tuambie ukweli wa hicho kinachoendelea kama mleta mada alivyotonya jee kuna ukweli au si kweli? hilo ndio la msingi.


Masuala ya kuachwa dr Shein kupiga kazi hilo ni suala lengine. Taratibu za kupinga kilichofanywa ikiwa kuna hisia za kukosekana haki au kupindishwa mambo acha wahusika wafuate mkondo wa sheria. Ikiwa UN haki inapatikana ama vipi acha wahusika waendelee na michakato hio ndio demokrasia .
 
Yaani unauliza au umeainisha sala zako?

Yaani ni sawa na kupiga simu kwenu alafu akipokea nduguyo unaanza kumuuliza "enhe niambie....nasikia Baba yupo hoi, miguu imevimba, amegoma kula, anapumua kwa shida, Waganga wamemshindwa, hafungui macho, amekata kauli,anakufa lini?"....
 
Tetesi ni kuwa wananchi wa zanzibar wanafanyakazi na biashara kama kawa

sawa watu WANAENDELEA KUTAFUTA RIZIKI ZAO HATUKATAI. SASA NJOO KWENYE MADA. DAWA HAKUNA NA UKATA UNAENDELEA SERIKALINI

Aidha kuna taarifa CUf kutaka kufunguwa kesi ICJ ni kweli au si kweli ? jibu
 
Yaani unauliza au umeainisha sala zako?

Yaani ni sawa na kupiga simu kwenu alafu akipokea nduguyo unaanza kumuuliza "enhe niambie....nasikia Baba yupo hoi, miguu imevimba, amegoma kula, anapumua kwa shida, Waganga wamemshindwa, hafungui macho, amekata kauli,anakufa lini?"....

Kuna mambo nauliza na niliyaweka hapa Jf kama mjadala mwenye ukweli atwambie. Yengine nimefuatilia na kuthibitisha mwenyewe. Lile la kususia maziko na ukata wa dawa na fedha serikalini nalo lipo.

Hili la CUF kutaka kufunguwa kesi ICJ lipo The guardian IPP media la tarehe 12 Mei, 2016.

Usitoke kwenye mada. Kanusha au thibitisha
 
Actually mimi hatari ninayoiona ni hii ya maji ya Bahari kuanza kuingia nchi kavu.....Zanzibar ni kisiwa na Dunia inaathirika na Global warming....nimemsikia jamaa anajaribu kutolea ufafanuzi, lakini siku zote nature itabaki kuwa nature.

Na wale mnaopenda wimbo wa Muungano.......nadhani mngeanza kufikiria kuwa na familia Bara kabla hamjashtuka kuwa population inakuwa huku ardhi inapungua....badala ya nyimbo za cuf na ccm kila kukicha.
 
Actually mimi hatari ninayoiona ni hii ya maji ya Bahari kuanza kuingia nchi kavu.....Zanzibar ni kisiwa na Dunia inaathirika na Global warming....nimemsikia jamaa anajieleza lakini nature itabaki nature.

Na wale mnaopenda wimbo wa Muungano.......nadhani mngeanza kufikiria kuwa na familia Bara kabla hamjashtuka kuwa population inakuwa huku ardhi inapungua....badala ya nyimbo za cuf na ccm kila kukicha.

Umetusaiia taarifa nyengine.

Bado nenda kwenye mada jee kuna ukweli wa alichotonya mwandishi au hakuna?

Pengine mwenzetu una alergie ya CCM na CUF
 
Umetusaiia taarifa nyengine.

Bado nenda kwenye mada jee kuna ukweli wa alichotonya mwandishi au hakuna?

Pengine mwenzetu una alergie ya CCM na CUF
Huwa sipendi hii mijadala ya Zanzibara, sijui cuf hivi ccm hivi....
 
Loo inasikitisha sana mjomba wangu aliukwaa uwakilishi wa kitipeni kwa Cuf lakini bosi alipobadili mawazo katukosesha maisha basi tena labda uchaguzi urudiwe tena lnshallah
 
Ungetusaidia hayo ya kisonge kwa faida ya wasomaji na wachangiaji wa JF
Duh Kisonge unaisikia au basi? Kisonge ndio kilele cha hate speech Zanzibar. Statement moja tuu ya Kisonge hapa, tosha kupigwa life ban JF. Tuwaheshimu Wanzazibari kuonesha uvumilivu mbele ya matusi na kudhulumiwa mchana kweupu .
 
Kwa kweli maisha ya Zanzibar kuliko Dubai yaaaani rahaaaaa tuu hao wanaosema kua kuna maisha magumu hawaitakii mema nchi ya mfalme sheni
 
Wewe ushaambiwa ukiuziwa sukari zaidi ya sh 1800 kwa kilo toa taarifa watu wanyooshwe sio kulalamika

Wewe unanunua duka lipi kwani kwa bei hiyo ya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa?

Ni maduka haya haya yanayouza TZS 3,000 - 5,000?? Au nyie wenzetu LB46 FC mmeshapata mgawo wa bure kutoka kwa waliokamatwa wameficha hiyo sukari?

Na kama sivyo na mnanunua huku huku kwenye maduka tunayonunua sisi "tunaoisoma namba", mmetoa taarifa polisi? wamekamatwa wangapi eti??
 
huo ni uongo mkuu. Zanzibar mambo safi sana
Mimi niko Zanzibar na ni shwari kabisa. Sanasana miradi mbalimbali ya barabara inaendelea. Mataa yanafungwa barabara zote. Kwwaujumla maendeleoa ni kwa kasikwasasa!
 
Back
Top Bottom